π—žπ—’π— π—žπ—¬π—”

π—žπ—’π— π—žπ—¬π—”

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from π—žπ—’π— π—žπ—¬π—”, komkya01@gmail. com, Dar es Salaam.

1.Graphics&Design
▢️Logo design, posters, cv-writing, B.cards
▢️Calendar, certificate, invoice design.
▢️Ghostwriter, online typing, IT issues.
2.Online Applications
▢️NIDA, RITA, BRELA, TIN applications.

03/09/2026

Mimi bwana nilikuaga na mpenzi wangu anaitwa Sam 😁 tulipendana sana tu tena kipindi hicho me ndo Bado binti yani Bado mbichiiii.. Sam tulikutana ghafla sio kwamba tulikua ni watu tuliofahamiana sana yeye ni boda Sasa me nikawa naenda sehemu kusalimia ndugu zangu ikabidi wampe Sam namba yangu ili anipokee stend......

Nilifika akanipokeaga na kunipeleka mpka home na kiukweli Sam ni handsome japo me wakati huo sikumuwazia nikamchukulia k**a boda tu 😊😊 zilipita k**a siku tatu kule nilipoenda kulikua na dada wa kazi Sasa nilikuaga nalala nae hiyo siku yule dada akanambiaga anaomba sim amtafute mtu mi nikampa.. akanambia me sijui kusoma Wala kuandika naomba niandikie af mtumie msg ya "mambo"

Katika kuandika si nikakuta ni namba ya Sam boda bwana me nikatuma k**a alivyonielekeza πŸ˜‚πŸ™Œ akajibu poa me hapo nikataja jina la huyo mdada akanambia mwambie nakusalimia nikatuma, hiyo hakujibu kesho yake akaja kunibeba maan nilikua nilikua napeleka chakula hospital kulikua na mgonjwa Sasa usiku si ndo akaanza kunichatisha Mimi akanitongoza pale na me nilikua single af nikiangalia kaka mwenyewe mzuri anavutia we nikakubari 🌚

Mida wote nilokaaga pale kwa mama angu mdogo sikuwahi kwenda kwa Sam Wala kukutana faragha zaid ya kuwasiliana tu na lbd akiagizwa aje nyumbani ndo tunaonana hivyo tu basi mi nilirudi kwetu huku tukiwa tunawasiliana mpk siku hiyo ananiambia anatuma nauli niende,,,,,, Sasa me kwakuwa nimempenda af nikiangalia naaga vip nyumbani Sam namtaka na nyumbani naagaje si nikatoeokaga bhna πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜† aaaaah!!! Jaman! ACHA kabisa πŸ™Œ

Mie huyo nikaenda mpka kupanda gari huyo kwa Sam nakwambia mapenzi yamenoga sam kanipeleka kwao hiyo siku siwezi kusahau nilivaa vitenge ilihali sikuwahi kujifunga funga vitenge nyieeeeee πŸ™ŒπŸ˜‚ nakwambia penzi tu lilikuaga Lele Lele 😊 mama nae alipoa baada ya kuanza kutumiwa viela vya kulipa vikoba uko akawa kimya mpole na Mimi si ndo nikaona hapa ndo hapa... Baby anaondoka asubuhi akijisikia upwiru Anarudi mbio mbio mpaka home mchana wa jua Kali nampooza kazi zinaendelea,

SASA SIKU HIYO BWANA KARUDI MCHANA UPWIRU UMEMSHIKA K**A KAWAIDA TUKAWA TUPO CHUMBANI TUNAPETIANA PETIANA SI MLANGO UKAGONGWA, SAM AKAENDA KUFUNGUA NA MBABA UMESIMAMA ME NIKAWA ZANGU CHUMBANI HAPO NIMEPANDISHWA MORI NASUBIRI WAONGEE AONDOKE BABY WANGU AJE NDANI TULIANZISHEEE πŸ˜‚πŸ™Œ

CHA KUSHANGAZA NIKAWA NASIKIA ANAMGOMEA KUINGIA CHUMBANI WAKAWA WANABISHANA BWANA πŸ₯± ME NIKASEMA WATAJUA WAO ME NIKACHUKUA SIM NIKAANZA KUSIKILIZA ZANGU KWAYA MARA NIKASIKIA SAM ME KICHWA KINAUMA KANINUNULIE PANADOL πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€£ YANI WANANGU HAPO ME SIJASHTUKA WALA ET NIENDE SEBLENI NIKAONE YANAYOENDELEA NIKAWA NIMETULIA NACHEZEA SIM TU.... SAMA AKAMWAMBIA HELA HII HAPA KANUNUE YULE DADA AKAKATAA BASI WAKATULIA ASA YEYE BWANA BAADA YA KUONA KAVURUGA IKABIDI AMPIGIE RAFIKI AKE MMOJA HV BODA MWENZIE AMBAE TUMETOKA MKOA MMOJA KWAHY SAM ALIPOANZA KUWA NA MIMI AKAANZAGA KUMWITA YULE SHEM, AKAMPIGIA SHEM WAKE AJE KUMSAIDIA.. YULE KAKA BAADA YA KUFIKA AKAMWAMBIA WE CHA MSINGI CHAGUA MMOJA TU HAPO MAAN HUNA NAMNA πŸ€”πŸ™„ ME NIKADAKIA NIKASEMA KABLA HAJACHAGUA ME NAOMBA TU ANIPE NAULI NIONDOKE COZ SIWEZI KUWA NA MTU MWENYE TABIA K**A ZAKE AKAKATAAGA SI AKAMPIGIA NDUGU YAKE HV AJE AMTOE HUYO DADA MAAN MPKA USIKU ULIINGIA YULE DADA ALIKUA BADO KAKAA PALE TU πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

MIMI NILIPOONA HATOKI IKANIBIDI NITOKE NIKAWA NAPUNGA UPEPO NJE NAJIZUNGUSHA NJIAN NAENDA NARUDI NAENDA NARUDI SAM NAE AKAJA SIJUI ALIJUAGA NIMEENDA KUJIUA AKANIBEMBELEZAAA WEEEE ME NIKAKUBARI KURUDI YULE DADA NAE AKAAMBIWA NENDA NYUMBANI USIKU UMEINGIA NDO AKATOKAGA PALE NA MIKWALA K**A YOTE 🀣🀣🀣

SASA SIJUI NINGEAMBIWAGA MIMI NDO NIRUDI SIJUI INGEKUAJE NA NYUMBANI NILITOROKAGAA ILA TULISOLVE SAM AKANAMBIAGA NIMPELEKE HOME TUKAENDAGA MPAKA HOME AKAJITAMBULISHA TUKAENDELEA NA MAHUSIANO MPKA TULIPOKUAJA KUCHOKANA KILA MTU AKAFATA NJIA YAKE πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ KINA SAM AISEEEE WAPUUZI SANA ASIKWAMBIE MTU

~Mdada wa MbaliπŸ˜†

02/09/2026

Ndio sasa wanashindana na millenial hawa Gen~z ,kwa sasa wanajidahi ndio kam wameianzisha dunia wao, they know each and everything kuwazidi waubwa zaoπŸ˜†

01/09/2026

Ni swali tu

30/08/2026

Dizasta Vina
Select Page
Articles
Ndugu Wa Mbali
πŸ“… Aug 30, 2026
|
✍ By Dizasta Vina
Ndugu Wa Mbali
← Back
Kila ifikapo mwezi wa nane kuelekea mwezi wa tisa, maelfu ya wanyama pori huvuka anga, vilindi vya mito na vichaka vya Serengeti kuelekea kusini mwa nchi ya Kenya kutafuta malisho mapya katika maeneo ya mbuga ya Maasai Mara. Safari hii kubwa ambayo imejirudia kwa vizazi visivyohesabika ni sehemu ya mzunguko wa asili unaounganisha mbuga hizi kubwa za Serengeti na Maasai Mara, licha ya kuwa maeneo haya yamegawanywa na mipaka ya nchi mbili.

Si wanyama wote hufika, wengine hufia njiani kwa maradhi, majeraha au kushambuliwa na wanyama wengine kwa ajili ya chakula. Wengine huangukia mikononi mwa majangili. Msafara hausimami kupisha maombolezo, wanyama waliobaki huendelea na safari, hawarudi nyuma kwa sababu ya kupoteza mwenzao. Wanyama hawa hutambua kitu kimoja, shida ipo nyuma, changamoto zipo katikati na nuru ipo mbeleni.

Ni uhalisia wa kusikitisha lakini pia ni ukumbusho kwamba dunia inaendelea kusonga. Kila mmoja ana safari yake, hivyo ni muhimu kutambua kesho yako ipo mikononi mwako mwenyewe.

Kwa maelfu ya miaka, mbuga za Serengeti na Maasai Mara zimekuwa zinaunganishwa na tukio hili la uhamaji wa ndege na wanyama pori, hivyo kufanya Tanzania na Kenya kuwa k**a ndugu. Haifahamiki idadi ya mbegu za mimea na viumbe mbalimbali zilizosafiri kutoka upande mmoja kwenda mwingine, ila udugu wa asili wa nchi hizi utabakia milele kihalisia na kifumbo.

Nyumbu wakivuka Mto Mara katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti – Tanzania.
(Picha na mtandao).

Katika maisha yetu, safari hizi zinaweza kusomeka k**a ishara ya ari ya kupambana kufikia malengo, utayari wa kubadilika na ashki ya kushinda uvivu na kubweteka kabla ya matatizo kufika. Lakini pia hutukumbusha thamani ya ujirani mwema, maana madhira yakiwadia basi pako pahala pa kukimbilia.

Nje ya madarasa na waadhiri waliotuzunguka, ni wanyama ndio wanaotukumbusha ujirani wetu, wanatukumbusha kuwa mipaka ya kiutawala, kiitikadi, kiutamaduni na kidini, tofauti za madaraja ya uchumi na utofauti wa rangi za bendera zetu, ambavyo vingi huishi kwenye fikra zetu tu bado tunahitajiana kwa sababu matatizo makubwa yakifika hayaangalii utofauti wetu..

Kabla hatujawa Watanzania na Wakenya, tulikuwa wanyama.
Kabla hapajakuwa na nchi, palikuwepo ardhi.
Sisi ni ndugu wa mbali.

Ndugu Wa Mbali

Ni katika roho hii ya udugu wa mbali ambapo Dizasta Vina (Tanzania) na Kaa La Moto (Kenya) wanakutana. K**a vile wanyamapori wanavyovuka mipaka bila kujali alama za ramani, sauti zao kutoka pande mbili za mpaka uleule, zinaungana kusimulia hadithi moja kupitia muziki.

Huu si mkutano wa wasanii wawili kutoka nchi mbili tu. Ni mkutano wa historia, lugha, utamaduni kwa ujumla. Uzoefu na fikra zilizokua katika pande mbili za ardhi moja.

NDUGU WA MBALI si EP tu.

Ni kumbukumbu ya kimuziki ya uhusiano wa asili kati ya Tanzania na Kenya – uhusiano uliojengwa kwa miaka mingi kupitia utamaduni, historia na asili yenyewe.

Ni safari ya sauti inayovuka mpaka.

Ni hadithi ya watu wawili kutoka pande mbili za mpaka uleule, pande mbili zinazosahau kuwa wao ni NDUGU WA MBALI.

D.V & K.L.M

Share this:
FacebookEmailWhatsAppMessengerTelegramXShare

Join Dizasta Vina
Terms & Conditions
Β© 2026 PANORAMA AUTHENTIK. All Rights Reserved.

28/08/2026
27/08/2026

watu wa afya kazi hiyo hapo

26/08/2026

??

25/08/2026

Punga mkono k**a umeona data analyst imevaa buti nyeupe inachakata dataπŸ˜‚πŸ˜‚
Mashine za DNA zikiwa kazini

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Website

Address

Komkya01@gmail. Com
Dar Es Salaam