nolly one

nolly one

Share

media personality || For Football
@simbasctanzania

Photos from nolly one's post 05/08/2026

✈️ Tukutane Dar es Salaam

•Simba day loading, tumalize maandalizi madogo tukutane siku ya utambulisho

Tusisahau tajiri kaweka namba 6 kwenye Insta story yake, wenye D mbili mshaelewa😎

05/08/2026

Mfano Simba day na Mayanga day ikafanyika uwanja wa Mkapa halafu pitch tu ndo isitumike match ikachezwa Uhuru kuna shida gani ? Hapo Shabiki atachagua aingie kushuhudia burudani ya Tamasha au aingie kuangalia match uhuru

Halafu wakati wa match unazuia watu wasitoke na wanapewa tangazo kabisa halafu uwanja wa Mkapa si saa moja match !? Unaweka ma big screen wakati match inaendelea Uhuru kule

Majukwa yapo tayari kwa mkapa si wangetumia tu majukwaa watu tukajazana tukapata vibr kisha match ichezwe hata KMC sawa tu baada ya Burudani ya utambulisho wachezaji wanatoka wanapanda helcopter inawarusha KMC kwaajili ya mchezo 😃🙌

Hili lilikuwa linawezekana kwa 💯 kabisa

Au mimi mawazo yangu ndo yapo 1986

05/08/2026

📌Mashabiki na wanachama wa simba msikubali kuendeshwa kilasiku, simameni na timu yenu ili badae msije mkafedheheka ni bora lawama kuliko fedheha nendeni na kaulimbiu yenu (NGUVU MOJA)

04/08/2026

📌 SIMBA SC INAHITAJI KUFANYA MABORESHO MAKUBWA KATIKA UONGOZI NA MFUMO WA UENDESHAJI WA KLABU. BAADHI YA VIONGOZI WALIOPO WANAONEKANA KUSHINDWA KUJENGA MSHIKAMANO NDANI YA TIMU, JAMBO LINALOSABABISHA MIGAWANYIKO NA KUKOSEKANA KWA USHIRIKIANO KATI YA VIONGOZI NA WANACHAMA.

🗣️ Ninachoamini ni kwamba mashabiki wanapaswa kusimama imara na kuipigania timu yao. Simba si mali ya mtu mmoja binafsi, bali ni klabu ya wanachama. Ndiyo maana mfumo wa umiliki umeweka wanachama kumiliki asilimia 51%, huku mwekezaji akimiliki asilimia 49%.

• Wanachama inabidi kufanya usahihishaji kwa upande wa uongozi wa wanachama maana hii ndio sehemu kuu ya kuendesha timu na k**a hapa hapaeleweki timu itakuwa ya kihuni tuh na kuendeshwa kifisadi, na ubingwa tutaishia kuusikia tuh.

🙌 Ila kwasasa ngoja nishabikie wachezaji tuh, nyie mtajua wenyewe!!!!!!

03/08/2026

👑KING KIBA, LIVE SIMBA DAY 2026

🚨Bado siku chache tukutane Simba Day tukaone wachezaji wetu wapya na wazamani wakitambulishwa na kutizama ubora wao katika mechi ya kirafiki tutakayocheza na Tusker Fc ya pale kenya.

✍️ Patakuwa na wasanii wa mziki na waigizaji pia bila kumsahau Dj wetu Sinyoritaaa, Ila Mfalme lazima awe mkuu wa show hii na atatumbuiza masaa ya kutosha tuh. Zitapigwa hit song zote unazozijua wewe🔥

Kuna viduduwatu vinasema nyimbo imechuja, sasa hapo mtajua wenyewe ila sisi hiyo ndio nyimbo yetu tunayo tamba nayo mtajua wenyewe takataka nyie🛃

📌 MWANASIMBA HUSIKUBALI KUKOSA/HII IMEENDA..........!!!

02/08/2026

👑🎤 MBOSSO KHAN, LIVE SIMBA DAY 2026

🚨Bado siku chache tukutane Simba Day tukaone wachezaji wetu wapya na wazamani wakitambulishwa na kutizama ubora wao katika mechi ya kirafiki tutakayocheza na Tusker Fc ya pale kenya.

Msanii wetu pendwa wa mudawote Mbosso k**a kawaida, yani hapa inapigwa DJ hujakaa sawa inapigwa OZALIMA kidogo tena tunarudi Darasa la 7 alafu tunamaliza na Aviola vibe la kutosha yani🔥

📌 MWANASIMBA HUSIKUBALI KUKOSA..........!!!

01/08/2026

SIMBA DAY 8/8 – UHURU STADIUM ❤️🤍🔥

Miaka imepita tangu jina la Diamond Platnumz lihusishwe kwa nguvu na Simba Day. Kila mwaka mashabiki wamekuwa wakilitaja na kulisubiri kwa hamu, na mwaka huu mjadala umeongezeka zaidi kuliko wakati wowote.

Kwa mafanikio makubwa ya Diamond na hit songs zake zinazoendelea kutikisa Afrika, wengi wanaamini kuwa k**a angeonekana kwenye jukwaa la Simba Day, ingekuwa moja ya show kubwa zaidi kuwahi kufanyika kwenye tukio hilo.

Tarehe 8/8, macho yote yataelekezwa Uhuru Stadium.

Je, k**a utakuja kutakuwa na mshangao ambao mashabiki wamekuwa wakiusubiri kwa muda mrefu?🤔

01/08/2026

📌Tuache masihara kwa huu u*i jamani ata Million 1 nanunua jamn🙌

Rushine De Reuck 🇿🇦 u*ii umekaa kabisa kwenye body, nyie wenye wivu toeni nanyie matambala yenu tuyaone🥱

🚨Simba Day Loading.......... tukutane uhuru Wanamsimbazi

01/08/2026

🚨BREAKING NEWS

🚩Taarifa mpya kuhusu Neo Maema x Simba SC x Mamelodi Sundowns:

Mkataba wa mwaka mmoja wa Neo Maema akiwa na Simba SC umefikia mwisho.
Kocha wa Simba, Barker, anataka kiungo huyo aendelee kuwa sehemu ya kikosi chake msimu ujao, lakini Mamelodi Sundowns wametumia kipengele cha kuongeza mkataba wake kwa miaka miwili.

Hii ina maana kwamba Simba italazimika kufanya mazungumzo mapya na Sundowns ikiwa itataka kumbakisha Maema, Hata hivyo, mahitaji ya mshahara ya Maema yamekuwa kikwazo kikubwa katika mazungumzo hayo.

Maema ni miongoni mwa wachezaji wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi ndani ya Simba, jambo linalofanya kufikiwa kwa makubaliano kuwa kugumu hadi hivi sasa.

Kwa sasa, kiungo huyo raia wa Afrika Kusini yupo nchini Afrika Kusini na hajaungana na kikosi cha Simba kilichopo Kigali kwa ajili ya mashindano ya CECAFA Kagame Cup.

Je nibora Neo Maema abaki au aondoke tuh🤔?

31/07/2026

🚨 TAARIFA ZA USAJILI | SIMBA SC 🔴

Simba SC wanaendelea kusaka nyota wa kuongeza makali kikosini kuelekea msimu mpya, huku jina la winga mwenye uzoefu Percy Mu*i Tau (32) likitajwa kwa nguvu katika rada za Wekundu wa Msimbazi.

Tau, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Thep Xanh Nam Dinh ya Vietnam, anaripotiwa kuwa tayari kujiunga na Simba. Hata hivyo, inaelezwa kuwa anahitaji kupata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza kabla ya kufikia makubaliano ya mwisho.

Aidha, zinaripotiwa tetesi kuwa tajiri na mdhamini wa Simba, Mo Dewji, yupo tayari kuwezesha dili hilo kwa gharama zinazokadiriwa kufikia Tsh bilioni 2.5, huku pia ikidaiwa kuwa mchezaji huyo anaweza kulipwa mshahara wa takribani Tsh milioni 80 kwa mwezi endapo makubaliano yatakamilika.

Je, Percy Tau atakuwa usajili sahihi kwa Simba?🤔

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address

Dar Es Salaam
11101