16/10/2023
Mjumbe wa Kamati ya utendaji ya TANZANIA Paralympic Committee ndugu Ernest Nyabalale alikuwa ni miongoni mwa wachezaji walioiwakilisha timu ya kuogelea ya TPC. TPC imeshiriki ikiwa ni miongoni mwa timu 11 zilizoshiriki Mashindano ya kuogelea ya kwanza ya Taifa kwa watu wenye ulemavu Tanzania 🇹🇿. Ernest ameshika nafasi ya tatu baada ya kutanguliwa na wachezaji wawili wa timu ya ZANZIBAR Talent Swimming CLUB kutoka Zanzibar katika mtindo wa freestyle katika bwawa la GYMKHANA CLUB DAR ES SALAAM.
16/10/2023
Mashindano ya kuogelea kwa watu wenye ulemavu yamefanyika kwa mara ya kwanza Tanzania 🇹🇿. Ni furaha iliyoje kuona wachezaji 82, vilabu 11 na makampuni na taasisi zaidi ya 14 zikifanikisha mashindano haya. HONGERA pia kwa Baraza la Michezo la Taifa BMT na pia Baraza la Taifa la michezo ZANZIBAR kwa mchango wenu na ushirikiano mliotoa na kufanikisha Chama cha Kuogelea kwa watu wenye ulemavu Tanzania TPSA wakaweza kufanikisha mashindano haya.
26/07/2023
Ni tukio la kihistoria, tarehe 14.10.2023 tunza tarehe hii siku ya Nyerere hapa Dar es Salaam kutakuwa na mashindano ya kutafuta vipaji vya kuogelea kwa watu wenye ulemavu.
Hili tukio si la kukosa kabisa, watu wenye ulemavu ni muda wa kujiandaa na mazoezi kuanzia sasa hadi siku ya tukio.
Taarifa zingine MUHIMU zinafuata
11/05/2022
*Tanzania Kushiriki Mashindano ya Ulaya - Poland kuelekea Kombe la Dunia 2022.*
Timu ya Taifa ya Tanzania kwa mpira wa mguu kwa walemavu Tembo Warriors imepata mwaliko rasmi wa kushiriki mashindano ya ulaya nchini Poland. Mashindano hayo yanayojulikana k**a *Amp-Futbal Europe 2022* yanayo tarajia kufanyika mwezi wa sita kati ya tarehe 10 hadi 13 katika mji wa *Warsaw Poland.*
Mashindano haya yanatajia kushirikisha nchi nne, nchi tatu kutoka bara la ulaya (England, Italy na Poland) na nchi moja kutoka Africa. Tanzania ndiyo nchi pekee ya africa iliyopata mwaliko kati ya nchi 18 za Africa na nchi ya pekee kati ya nchi nne za Africa zilizofuzu kwenda kombe la Dunia.
Rais wa Shirikisho TAFF ndg. Peter Sarungi amesema kwamba Tanzania inazidi kung'ara katika mchezo huu na hii inatokana na ushiriki wa Serikali yetu na wadau wengine kusaidia kulea na kuhudumia mchezo huu nchini. Mfano mzuri uliochukuliwa na mataifa mbalimbali ya nje ni utayari na ukubali wa *Rais Samia Suluhu na Serikali yake* kugharamia na kuandaa mashindano ya Africa (CANAF 2021)
05/05/2022
Kamati ya Paralimpiki Tanzania na Chama cha Riadha Tanzania kwa watu wenye ulemavu (Tanzania Para Athletic Association-TPAA) imeteua makocha wa Timu ya Taifa.
Tunawatakia kila heri na mafanikio makubwa na kuweza kuinua viwango vya wachezaji wetu.
Hongera Kocha Iddi Muhunzi na Kocha Bahati Mgunda.
10/12/2021
"Sports associations for people with disabilities hail President Samia"
Sports associations for people with disabilities hail President Samia
​​​​​​​A day after President Samia Saluhu Hassan hosted Tanzania's amputee football team 'Tembo Warriors' players and officials in a function,which took place in Dar es Salaam early this week, some leaders of sports associations for people with disabilities have hailed the President fo...
18/11/2021
Rais wa TPC ndugu Tuma Dandi akiwa picha ya pamoja na Rais wa International Paralympic Committee ndugu Andrew Person (right).
Ni furaha kubwa kukutana na Rais wa IPC kwa ajili ya maendeleo ya michezo ya watu wenye ulemavu nchini Tanzania na duniani kwa ujumla.