Tanzania Paralympic Committee

Tanzania Paralympic Committee

Share

Tanzania Paralympic Committee (TPC) is the organization which enhances sports and athletes for Tanza

22/07/2026

πŸ‡ΉπŸ‡Ώ KARIBU TPC! πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Tunayo furaha kubwa kumkaribisha Coach Bahati Mgunda k**a Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Tanzania Paralympic Committee (TPC).

Coach Bahati analeta uzoefu mkubwa katika maendeleo ya michezo ya watu wenye ulemavu, akiwa na weledi katika ukocha, ujenzi wa uwezo wa wanamichezo na makocha, pamoja na kuhamasisha ushiriki jumuishi kupitia michezo.

Tunaamini mchango wake utaendelea kuimarisha safari ya kukuza na kuinua michezo ya Paralimpiki nchini Tanzania, huku tukiwajengea wanamichezo wetu mazingira bora ya kufikia mafanikio ya kitaifa na kimataifa.

Karibu sana Coach Bahati Mgunda!
Pamoja tutaendelea kujenga Tanzania yenye usawa, fursa na mafanikio kupitia michezo.

πŸ“² Follow us:

15/07/2026

Karibu sana Coach Innocent Maseke Jonas kwenye Kamati ya Ufundi ya TPC.

11/07/2026

Day 3: Sitting Volleyball Training Camp!

Mafunzo ya mpira wa wavu (Sitting Volleyball) yanaendelea leo ikiwa ni siku ya tatu ya kishindo hapa chuo kikuu cha Dar es Salaam!

Leo washiriki wamejikita kwenye mbinu za kiufundi uwanjani: kuanzia jinsi ya kucheza, kufanya service, set-up, kublock, hadi namna ya kufanya maamuzi sahihi wakati wa mchezo.

Ni dhahiri Para Volleyball wameanza kwa mguu wa kulia katika kuinua michezo ya watu wenye ulemavu nchini. Kazi inaendelea! πŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Paralympic Committee

11/07/2026

Chama cha ParaVolley Tanzania (Tanzania ParaVolley Association) kimeingia kazini kwa nguvu zote kuhakikisha mchezo wa Sitting Volleyball unakuwa na unaleta tija kwa jamii ya watu wenye ulemavu nchini.

Hivi sasa, mafunzo makali na ya kitaalamu yanaendelea ndani ya viunga vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Mafunzo hayo yanaongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho, ambaye pia anashikilia wasifu mkubwa wa kimataifa k**a World ParaVolley Coach and Referee Level 2. Akiwa bega kwa bega na Katibu Mkuu wake, Dr. Janet Mlay, wamejichimbia UDSM kusimamia mafunzo hayo kwa weledi wa hali ya juu.

Mchezo wa Sitting Volleyball unaleta hamasa, unajenga afya, na unafungua milango ya fursa nyingi za kitaifa na kimataifa. Tunatoa wito kwa wadau wote wa michezo, mashirika, na jamii kwa ujumla kuunga mkono juhudi hizi kubwa.

09/07/2026

Kamati ya Olimpiki ya Walemavu Tanzania (TPC) inapenda kuwajulisha kuwa leo kumefanyika ufunguzi rasmi wa mafunzo ya mchezo wa Paravolley nchini. Mafunzo haya yanafanyika katika Idara ya Sayansi ya Michezo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), chini ya usimamizi na uratibu wa Mkurugenzi wetu wa Ufundi, Dr. Janeth Mlay amabae pia zkatibu Mkuu wa Tanzania Paravolley Association.

Siku ya kwanza imekuwa na mwitikio mkubwa na wa kuridhisha, ikihusisha wanafunzi wa mwaka wa pili wa idara hiyo pamoja na washiriki wenye ulemavu. Huu ni hatua kubwa katika mikakati yetu ya kuendeleza michezo ya walemavu na kuongeza wataalamu wa mchezo huu nchini.

Mafunzo haya yataendelea kesho na yatadumu hadi tarehe 13 Julai 2026. Tunawakaribisha wadau wote wa michezo, wapenzi, na umma kwa ujumla kufika UDSM kujionea namna mchezo huu unavyochezwa na kujifunza sheria na kanuni zake.

Huu ni mwanzo mpya wa Paravolley nchini Tanzania! Kozi njema kwa washiriki wote.

07/07/2026

Habari njema kwa wadau wote wa michezo!

Mafunzo ya Ukocha na Uamuzi (Coaching and Officiating) ya Para Volleyball sasa yatafanyika rasmi kuanzia tarehe 09.07.2026 hadi 13.07.2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Hii ni fursa ya kipekee ya kujifunza, kuongeza ujuzi, na kuunga mkono harakati za kukuza michezo ya watu wenye ulemavu nchini. Wadau wote mnakaribishwa sana mje tushirikiane kusukuma mbele gurudumu hili!

Weka alama kwenye kalenda yako, usipange kukosa!

30/06/2026

Karibu Ndani ya Familia ya TPC, Dr. Janeth Mlay!

Mstari wa mbele kuelekea mafanikio mapya unazidi kuimarika! Kamati ya Paralympic Tanzania (TPC) tunafarijika na kufurahia sana kukukaribisha Dr. Janeth Mlay katika familia hii kubwa ya Para-Sports ukiwa ni Mkurugenzi wa ufundi na mjumbe wa k**ati ya utendaji ya TPC..

Tunaamini kwa pamoja tutaandika historia mpya ya mafanikio, kuibua vipaji, na kuweka viwango vya juu vya kiutendaji na kiufundi katika michezo ya watu wenye ulemavu nchini.

Kazi ndio kwanza inaanza! Let’s make history together! πŸš€πŸ”₯

PamojaTunaweza

29/06/2026

SAVE THE DATE! πŸ—“οΈπŸŠβ€β™‚οΈπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Kamati ya Paralympic Tanzania (TPC) ikishirikiana na Tanzania Para Swimming Association (TPSA) inakuletea Tanzania National Para Swimming TALENT Identification Gala

Hii ni fursa ya dhahabu ya kuibua na kukuza vipaji vya waogeleaji wenye ulemavu nchini, kuelekea maandalizi ya mashindano makubwa ikiwemo LA 2028!

Usipitwe na tukio hili kubwa la kihistoria. Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi za jinsi ya kushiriki na kujisajili!

22/06/2026

Chama cha Sitting Volleyball kinaendesha mafunzo maalum katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Hii ni fursa ya kipekee kwa wote wenye nia na shauku ya kuendeleza mchezo wa Paravolley nchini!

Michezo ya watu wenye ulemavu inahitaji nguvu yetu sasa hivi. Ni wakati wetu wa kuamka, kuwajibika, na kuonyesha uwezo wetu.

Tarehe: 24 - 28 Mahali: Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

Usikae pembeni! Jiunge nasi sasa tufanye mapinduzi kwenye Paravolley. Karibuni wote! πŸ™ŒπŸ”₯

18/06/2026

UONGOZI MPYA: KARIBU KATIBU MKUU! πŸ””

Tunapenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa dhati Ndugu Ramadhan Namkoveka kwa kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa Kamati ya Utendaji ya Tanzania Paralympic Committee (TPC).

Udumu katika kuiongoza michezo ya walemavu na kuifikisha katika kilele cha mafanikio nchini na kimataifa. Kila la heri katika majukumu haya mapya ya kujenga na kuendeleza vipaji!

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Address

Studio, Kinondoni
Dar Es Salaam