05/12/2025
KwetuHabari
Media
Breaking news|Current news|Sports|entertainment. We will Update you 24/7
05/12/2025
📌VIDEO
Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba akiwajibu wanaharakati wa mitandao wanaosema anaweza kuwa Waziri Mkuu atakayekaa kaa muda mfupi madarakani.
📌VIDEO:
Washirika wa Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Askofu Joseph Gwajima wakifanya usafi baada ya kuruhusiwa Serikali kuendelea kufanya ibada.
📌VIDEO:
Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.
Hayo yameelezwa Jijini Dodoma Novemba 25, 2025 wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba na Menejimenti ya REA kilicholenga kujadili utekelezaji wa miradi inayosimamiwa na REA.
VIDEO:
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, amelaani vikali tabia ya baadhi ya watu kueneza taarifa za uongo na zisizofanyiwa uchunguzi, akisema hatua hiyo imefika kiwango cha kuwaumiza na kuwavuruga wananchi.
22/09/2025
🆕️
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mkwawa, ambaye pia ni Mdhamini Mkuu wa mashindano ya Mkwawa Rally of Tanzania yanayohusiana na kalenda ya African Rally Championship (ARC) Ahmed Huwel Mkwawa, ameweka wazi dhamira yake ya kukuza na kuendeleza vipaji vya madereva chipukizi wa mbio za magari hapa nchini.
Huwel amesema lengo la mashindano hayo ni kuwawezesha kushiriki kwenye mashindano ya kimataifa na hatimaye kuliletea taifa heshima na ushindi.
Akizungumza mkoani Morogoro wakati wa kufunga mashindano hayo yaliyodumu kwa muda wa siku tatu, Ahmed amesema kuwa, Tanzania imebarikiwa kuwa na vijana wengi wenye vipaji ambao wakipewa nafasi, mafunzo na msaada wa kutosha, wana uwezo mkubwa wa kung'ara kimataifa.
Katika mashindano hayo, Ahmed pia ameshiriki na kuibuka mshindi wa tatu, jambo lililoonyesha dhamira yake sio tu k**a mdhamini bali pia k**a mshiriki mwenye uwezo mkubwa.
Ahmed ameongeza kuwa yeye pamoja na makampuni yake wako tayari kushirikiana na vijana wanaoonyesha vipaji katika mchezo wa mbio za magari, kwa kuwapatia mafunzo, vifaa na kuwafungulia fursa za kushiriki mashindano mbalimbali huku akitoa wito kwa taasisi za serikali, mashirika binafsi, kampuni na wadau wengine wa michezo kuungana katika juhudi hizo ili kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na mashindano yenye viwango vya juu kimataifa.
22/09/2025
🆕️
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ameiagiza Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira Wilaya ya Karatu kuongeza kasi katika mchakato wa kumpata Mkandarasi wa kupeleka Maji kwenye Matenki pamoja na usambazaji wa maji kwa wananchi wa Wilaya ya Karatu Mkoani Arusha kutoka kwenye chanzo cha Maji cha Bwawani.
CPA Makalla ametoa maelekezo hayo leo Jumatatu Septemba 22,2025 Mjini Karatu kwenye ziara yake ya kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo, akitembelea na kukagua chanzo cha Maji cha Bwawani, Karatu Mjini, Chanzo ambacho kiliharibiwa na Mafuriko ya Mvua na kuathiri upatikanaji wa maji Karatu na hivyo kulazimu serikali kutenga fedha ili kunusuru chanzo hicho cha Maji ambacho kimekuwa tegemeo la uzalishaji maji kwa Mji wa Karatu pamoja na maeneo ya jirani.
Mhe. Makalla pia ameipongeza Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira Karatu kwa usimamizi mzuri wa utoaji wa huduma za Maji kwenye Wilaya hiyo ambao umefikia asilimia 71 kwasasa, akihimiza Jamii pia kushirikishwa na kupewa elimu katika utunzaji wa vyanzo vya maji vilivyopo kwenye maeneo yao.
"Niwasihi tushirikiane pia na wananchi wa maeneo haya kuona kwamba tunatunza vyanzo vya maji lakini pia na sisi wenyewe k**a Mamlaka ya Maji kuendelea kutoa elimu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na kutokuchafua vyanzo vya maji." Amesisitiza CPA Makalla.
Awali katika taarifa yake, Meneja wa Mamlaka ya Maji Karatu Injinia Steven Siayi, amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa serikali imeshatoa zaidi ya Milioni 145 kwaajili ya kufikisha maji kutoka kwenye chanzo hicho kwenda kwenye tenki la ujazo wa maji Lita 225, 000 na baadae kusambaza Maji kwa wananchi, akisema kisima hicho kilichonusuriwa kina uwezo wa kuzalisha Maji Lita 28,000 kwa saa.
22/09/2025
🆕️
Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba SC, Fadlu Davids, ametangaza rasmi kuachana na timu hiyo akieleza hisia zake za dhati kwa uongozi, wachezaji na mashabiki wa klabu hiyo.
Kupitia ujumbe wake aliouandika kwenye Instagram page yake, Davids amesema tangu alipowasili alihisi mapenzi makubwa ya klabu hiyo na mashabiki wake, akibainisha kuwa walipambana pamoja, kusherehekea pamoja na kushinda changamoto kwa mshik**ano.
Aidha, ameishukuru kwa dhati uongozi wa klabu chini ya Rais Mohammed Dewji (Mo Dewji) kwa uongozi wake wa mfano na msaada mkubwa alioupata katika kipindi chake. Vilevile, amewataka wachezaji waendelee kupigania heshima ya jezi ya Simba, huku akiwapongeza wafanyakazi na benchi la ufundi kwa kujitolea kwao nyuma ya pazia.
Davids pia hakusita kuwashukuru mashabiki wa Simba SC akiwaita "moyo wa klabu," akibainisha kwamba nyimbo na shangwe zao vitabaki katika kumbukumbu zake, amehitimisha kwa kusisitiza kuwa Simba SC itaendelea kubaki sehemu ya maisha yake na kuitakia klabu hiyo mafanikio makubwa na mataji zaidi siku za usoni.
22/09/2025
📌Yanapunguza sumu ya mkaa kwa watumiaji
📌 Ni rafiki kwenye utunzaji wa mazingira
📌Majiko banifu 1000 kuuzwa kwa bei ya ruzuku katika Maonesho ya Madini Geita
📍GEITA:
Imeelezwa kuwa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni majiko yanayotumia kiasi kidogo cha mkaa kulinganisha na majiko mengine ya mkaa.
Hayo yamebainishwa na Wataalam kutoka REA wanaoendelea kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita.
Aidha, majiko banifu yametengenezwa kwa teknolojia ya kisasa yenye uwezo wa kupunguza sumu ya mkaa (carbon monoxide) hivyo inasaidia kupunguza madhara ya kiafya yatokanayo na nishati ya mkaa.
Halikadhalika, majiko banifu yanasaidia utunzaji wa mazingira, ni rahisi kwa matumizi yanadumu kwa muda mrefu bila kupata changamoto ya kuharibika kwa watumiaji.
Katika mkoa wa Geita kampuni inayosambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku ni Geita Millenium Star Company Limited.
Majiko banifu yanatolewa kwa bei ya ruzuku ya shilingi 6,195 kwa kuwa Serikali imeweka ruzuku ya bei katika majiko hayo ili wananchi waweze kuyatumia na kuyapata kwa urahisi ambapo kabla ya ruzuku yalikuwa yanauzwa kwa shilingi 41,300.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam