26/08/2026
Kila siku tunapewa nafasi ya kuanza upya, Makosa ya jana hayapaswi kuwa sababu ya kukata tamaa, bali yawe somo la kutusaidia kubadilika.
Muhimu ni kutambua makosa, kujifunza kutokana nayo na kufanya juhudi kuwa mtu bora zaidi leo kuliko ulivyokuwa jana.
Babu Kijana 🇹🇿
19/08/2026
🚨 Usajili wa Manchester United msimu uliopita 2025/26
Matheus Cunha
Benjamin Šeško
Bryan Mbeumo
Senne Lammens
Safu ya ushambuliaji na golikipa imekamilika. ✅
Usajili wa Manchester United msimu huu 2026/27
Andrey Santos
Youri Tielemans
Carlos Baleba (K**a litakamilika)
Kiungo kimekamilika. ✅
Kwa sasa, hakuna anayejua INEOS na timu yake ya usajili wanapanga nini kinachofuata hata waandishi bora kabisa wa habari za soka hawana taarifa kamili wanashtukia dili lina karibia kukamilika
Naipenda sana hii style yao. Hakuna kuhusisha sana vyombo vya habari, hakuna hype zisizo na maana, hakuna kuongeza bei kwa sababu ya kelele za media ni mipango safi, tulivu na biashara halisi ya kisoka. 💪
Hivi ndivyo usajili unavyopaswa kufanyika. 🔥
19/08/2026
🚨💣 TAARIFA KUBWA: Manchester United iko mbioni kukamilisha dili la kumsajili Carlos Baleba kutoka Brighton.
United imetoa ofa ya pauni milioni £60m pamoja na nyongeza ya £5m, ambayo bado iko chini ya thamani iliyowekwa na Brighton.
Hata hivyo, mazungumzo yanaendelea kwa hali nzuri, huku pande zote zikifanya kazi kuhakikisha makubaliano yanafikiwa.
25/06/2026
Kila jambo kwenye maisha lina kusudi liwe zuri au baya linasababu yake la maana ni kukabiliana na lolote kwa nguvu zote bila kuwa na hofu na mashaka usiache kushukuru kwa kila jambo chini ya jua.
15/12/2025
Thamani yako haipimwi kwa maneno yao au mtazamo wao juu yako. Kila mtu anapaswa kukuheshimu k**a binadamu kabla ya chochote kingine.
16/04/2025
Hata vile vilivyochakaa, Mwenyezi Mungu ana uwezo wa kuving'arisha