03/06/2026
Mmeanzisha Vita ya Magari sasa twendeni kazi
Mwaka 2012 Simba na Yanga tulipewa Magari aina ya YOUTONG F11 na Kampuni ya TBL ambayo ilikua mdhamini Mkuu wa Vilabu hivyo kupitia kinywaji cha Kilimanjaro
Hilo Bus la kizamani mpaka leo Yanga wanalo wamewapa Yanga Princess wanahangaika nalo mvua yao jua lao
Mwaka 2021 Simba tukanunua Bus jipya aina ya TATA, Yanga nao wakaiga wakaenda kichwa kichwa wakaunua gari hilo hilo
Simba tukatumia Bus hilo kwa muda wa mwezi mmoja tuu, tukaachana nalo takanunua Bus jipya aina ya DRAGON Mnyama ambayo tunayo mpaka sasa
Wenzetu bado wanakomaa na TATA yao, Wakienda Mikoa ya Karibu k**a Tanga hawaendi nalo wanakodi Mabasi kutoka makampuni mengine sielezi kwanini nisije kuharibu Biashara ya watu
Tukiwa bado tunatamba na Bus la kisasa na kifahari la DRAGON tuliyonunua fedha zetu wenyewe, Leo Tunabadilisha Bus na sasa tunaingia kwenye Standard ya Dunia ya Irizar
Kwa historia hii fupi unaelewa kwanini Nyuma Mwiko wamechanganyikiwa sana na ujio wa Irizar kwa sababu tumezidi kujitofautisha sisi na wao
Kioo cha mbele cha Irizar yetu mpya unauanua gari ya Yanga
Msiumie Wanetu Mwambieni Boss wenu awabadilishie Bus contact za Irizar anazo
24/05/2026
24/05/2026
24/05/2026
24/05/2026
21/05/2026
21/05/2026
21/05/2026
21/05/2026