22/04/2026
MATCHDAY IN ZANZIBAR ⚽️
⛳️ KVZ FC 🆚️ AZAM FC
🏟 Amaan Complex
⏲️ Saa 1:15 usiku
🏆 Muungano Cup
Ligi Zetu | Tanzania Football
Monitoring football competitions across Tanzania.
22/04/2026
MATCHDAY IN ZANZIBAR ⚽️
⛳️ KVZ FC 🆚️ AZAM FC
🏟 Amaan Complex
⏲️ Saa 1:15 usiku
🏆 Muungano Cup
21/04/2026
Shekhan Khamis akiwa kwenye ardhi ya nyumbani kabisa (Zanzibar) amehusika kwenye magoli mawili kati ya manne ambayo Yanga SC wameyapata kwenye ushindi wa goli 4-0 dhidi ya Muembe Makumbi City.
Shekhan Khamis amefunga goli moja na kutoa Assist moja kwenye mchezo huu.
21/04/2026
MATCHDAY IN ZANZIBAR ⚽️
⛳️ Yanga SC 🆚️ Muembe Makumbi City
🏟 Amaan Complex
⏲️ Saa 1:15 usiku
🏆 Muungano Cup
21/04/2026
Michuano ya Muungano Cup inaanza rasmi leo visiwani Zanzibar, mchezo wa ufunguzi ukiwa ni kati ya Yanga SC 🆚️ Muembe Makumbi City utakaopigwa kwenye dimba la Amaan Complex, Saa 1:15 usiku.
Michuano hii ya Muungano Cup inazihusisha jumla ya timu nane (8), timu nne (4) kutoka visiwani Zanzibar na timu (4) kutoka Tanzania Bara.
Timu shiriki kutoka Zanzibar:-
• Muembe Makumbi City
• Mlandege FC
• Mafunzo FC
• KVZ FC
Timu shiriki kutoka Tanzania Bara:-
• Yanga SC
• Simba SC
• Azam FC
• Singida BS
20/04/2026
Klabu ya Simba SC imetozwa faini ya jumla ya kiasi cha shilingi Milioni Ishirini (20,000,000/=) kutokana na makosa matatu yaliyofanywa na mashabiki pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa klabu hiyo kwenye michezo miwili ya ligi kuu.
• Kosa la Kwanza (Mashabiki wa Simba SC)
Simba SC wametozwa faini ya Sh. 10,000,000/= (milioni Kumi) kwa kosa la mashabiki wake kumrushia chupa za maji mwamuzi msaidizi kwenye mchezo wa Simba dhidi ya Azam uliomalizika kwa sare ya 0-0
• Kosa la Pili (Benchi la ufundi & Wachezaji wa Simba)
Simba SC imetozwa faini ya Sh. 5,000,000/= (Milioni Tano) kwa kosa la viongozi wa Benchi la ufundi na Wachezaji wa Simba kutumia mlango usio rasmi kuingia uwanjani kwenye mchezo wao dhidi ya Azam FC uliomalizika kwa sare ya 0-0
• Kosa la Tatu (Walinzi/Mabaunsa wa Simba SC)
Simba SC imetozwa faini ya Sh. 5,000,000/= (Milioni Tano) kwa kosa la Walinzi wao kupigana (yaani kuzichapa kavu kavu) na Walinzi wa timu ya TRA baada ya timu kuwasili uwanjani kwenye mchezo wao dhidi ya TRA United uliomalizika kwa sare ya 0-0
Kulingana na makosa na adhabu zote zilizotolewa, klabu ya Simba SC imekutana na rungu la faini ya Shilingi Milioni Ishirini.
20/04/2026
Kiungo wa Yanga SC, Mudathir Yahya amefungiwa mechi tatu (3) na kutozwa faini ya Shilingi Milioni Moja (1,000,000/=) kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa Pamba Jiji, Ibrahim Abraham kwenye mchezo ambao Yanga SC walipata ushindi wa goli 3-0 dhidi ya Pamba Jiji.
Baada ya adhabu ya Djigui Diarra kumalizika sasa ni wakati wa Mudathir Yahya kuingia adhabuni.
Anicet Oura ni moja ya sajili bora sana ambayo Simba tumeifanya na tangu amefika Simba SC hajawahi kucheza vibaya.
Maneno ya Ahmed Ally (msemaji wa Simba SC)
Semaji la Mnyama Ahmed Ally akimwaga maua kwa wachezaji wa Simba SC baada ya ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Namungo FC
Mnyama anatamba kuendeleza kichapo kwa kila atakaekatiza kwenye anga zake 😁
19/04/2026
Elie Mpanzu amewatungua Wauwaji wa Kusini na kufanya ubao usome goli 3 kwa upande wa Mnyama.
WHAT A GOAL 🔥⚽️
19/04/2026
Wauwaji wa Kusini nao wanaitaka mechi k**a ilivyo kwa Mnyama, hakuna anaebaki nyuma kila timu inacheza, kila timu inatengeneza nafasi na kila timu inashambulia.
Moja ya mechi yenye ushindani na burudani kwa 100%