Dotto Makeyuji

Dotto Makeyuji

Share

I'm a 🇹🇿|🎓B.Ed. in PE&Sports Sciences.
|📚Sports Admin.|CAF Diploma D Coach.
|Sports Sciences & Football Analyst
|📚Studied at UDSM (2022-25)
|Mr.

Sports Sciences

19/05/2026

Hello Fans .

Kuna mtazamo unaoibuka kwamba hatua inayofuata ya Pep inaweza kuwa nchini Italia — mahali ambapo angeweza kufundisha moja ya klabu kubwa k**a AC Milan, kwa ushirikiano wa karibu na Shirikisho la Soka Nchini Italia na Baadae Kuinoa Timu ya Taifa ya Italia.

LENGO KUBWA?.. Sio mafanikio ya klabu pekee… bali kujenga mfumo wa Taifa Zima la Italia kisoka.

IDEA HII INALENGA: •....

✅Kuleta falsafa ya kipekee ya uchezaji (positional play) ndani ya mfumo wa Italia.

✅Kuunda “identity” ya pamoja kutoka klabu hadi timu ya taifa ya Italia.

✅Kuimarisha maendeleo ya vijana kwa mtazamo wa muda mrefu.

MATOKEO YANAYOTARAJIWA:..

Kizazi kipya cha wachezaji kitakachokuwa tayari kimkakati na kiakili kuipa nguvu kwa miaka ijayo.

Hii si tu ajira ya kocha… Ni project ya kitaifa yenye lengo la kubadilisha mfumo mzima wa soka la Italia.

Swali ni moja:...

Je, Italia wako tayari kumpa Pep mamlaka ya kubadilisha DNA yao ya soka?

19/05/2026

Hello Fans .

Mourinho atoa onyo kali kwa Wachezaji na Rais wa Real Madrid 🔥

Mourinho ameweka wazi falsafa yake ya nidhamu na kujitoa uwanjani:..

🗣️ “Mchezaji yeyote kwenye timu yangu lazima atoe kila kitu… akimbie kwa ajili ya timu. Ukishindwa kufanya hivyo — benchi linakusubiri.”

Huu ni ujumbe mzito unaoonyesha msimamo wa The Special One kuhusu:...

✅ Kujituma (Work Rate)
✅Nidhamu ya timu
✅ Uwajibikaji wa mchezaji

Kisayansi, Mourinho anasisitiza high-intensity effort na collective responsibility — vitu vinavyoamua mafanikio ya timu kubwa.

Je, falsafa hii bado ina nafasi kwenyesoka la kisasa?

19/05/2026

Hello Fans .

Inaelezwa kuwa pep Guardiola amekasirishwa sana na muda ambao taarifa za kuondoka kwake zimetoka hadharani — huku wachezaji wakibaki kwenye mshtuko mkubwa!

Cha kushangaza zaidi?...

Ni kwamba hadi Jumamosi iliyopita, kikosi kilihakikishiwa kuwa Pep Guardiola Haondoki kwenda popote!

Guardiola alilazimika kuitisha late-night group call na wachezaji wake kuthibitisha rasmi kuondoka kwake, huku akiomba radhi kwa namna taarifa hiyo ilivyovuja bila yeye kutarajia.

Ndani ya vyumba vya kubadilishia nguo, hali ni ya sintofahamu… kila mtu yupo kwenye absolute disbelief.

Hii si tu taarifa — ni psychological shock inayoweza kuathiri morali ya timu kuelekea mechi zijazo.

(Chanzo;SunSport)

19/05/2026

Hello Fans .

Joao Pedro ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MSIMU CHELSEA! 🔥

Mashabiki wa wamemchagua rasmi João Pedro k**a Mchezaji Bora wa Msimu (Player of the Season) baada ya kampeni bora yenye ushawishi mkubwa uwanjani!

Matokeo ya kura:..
1. Joao Pedro — kura zaidi ya 60%
2. Enzo Fernandez
3. Moises Caicedo

Akiwa na mchango mkubwa kwenye ushambuliaji na ubunifu wa timu, João Pedro ameonyesha ubora wa hali ya juu uliowavuta mashabiki wengi kumpa kura zao kwa wingi.

Je, huu ndio mwanzo wa enzi mpya Stamford Bridge?

Photos from Dotto Makeyuji 's post 19/05/2026

Hello Fans .

✅ 𝗢𝗙𝗙𝗜𝗖𝗜𝗔𝗟: Liverpool wamezindua rasmi jezi yao mpya ya nyumbani kwa msimu wa 2026/27! 🔴🔥

Muonekano mpya, lakini utambulisho uleule wa kihistoria unaobeba roho ya Anfield .

Jezi hii inaendelea kuakisi falsafa ya klabu — urithi, heshima, na ushindani wa kiwango cha juu.

Rangi nyekundu imebaki kuwa alama ya moto wa ushindi na mapambano yasiyokoma.

Mashabiki, mnasemaje kuhusu hii design mpya? Je, ni Jezi ya 🔥 au bado?

19/05/2026

Hello Fans .

Manchester City wametangaza rasmi: Enzo Maresca ndiye kocha mpya wa klabu hiyo kwa mikataba ya misimu 3 ijayo!

Taarifa hii imeweka wazi mustakabali mpya wa mabingwa hao wa England, huku Maresca akipewa jukumu kubwa la kuendeleza falsafa ya ushindi na soka la kisasa ndani ya Etihad Stadium. 🔥

Mashabiki sasa wanabaki na swali moja kubwa…

Je, Maresca ataweza kuendeleza legacy ya mafanikio makubwa iliyoachwa na Pep Guardiola?

19/05/2026

Hello Fans.

Msimu wa Championship.

1. Geita gold FC...pts 64
2. Kagera Sugar..pts 61
3. Mbeya kwanza...pts 54
4. Polisi Tanzania...pts 54

Mechi Tano Zimebakia Kuamua Hatima🔥

Nafasi ya 1 na 2 Watacheza kuwania Bingwa wa Championship.

Nafasi 1 na 2 watapanda Ligi Kuu Moja kwa Moja.

Nafasi ya 3 na 4 watacheza Playoff ya Kuwania Nafasi ya Kufuzu Ligi kuu 📌

19/05/2026

Hello Fans .

| BREAKING NEWS

Manchester City inasemekana ipo kwenye mipango ya kipekee ya kumuenzi kocha wao mkuu Pep Guardiola kwa kumpa heshima ya hali ya juu — ikiwemo kubadilisha jina la moja ya “stands” ndani ya Etihad Stadium kwa jina lake.

Hatua hiyo inatajwa kuwa ni ishara ya kuthamini mchango mkubwa wa Guardiola katika historia ya klabu hiyo, baada ya kuibadilisha Man City kuwa moja ya timu bora zaidi duniani.

Wakati huo huo, ripoti zinaeleza kuwa Guardiola ana kipengele (clause) kwenye mkataba wake kinachomruhusu kuondoka klabuni mwaka mmoja kabla ya muda wa mkataba kuisha.

Mmoja wa wafanyakazi wa klabu ameeleza kuwa: “Ni siri mbaya kabisa kufichwa kwenye soka kwamba Guardiola anaweza kuondoka majira haya ya joto.”

Hali hii imezua mjadala mkubwa ndani ya klabu na mashabiki kuhusu mustakabali wa enzi ya Guardiola Etihad.

19/05/2026

Hello Fans .

Kocha wa Burnley, Michael Jackson amezungumza kwa hasira baada ya mchezo akilalamikia uamuzi wa mwamuzi dhidi ya Kai Havertz:..

🗣️ “Havertz alipaswa kupewa kadi nyekundu; huo ulikuwa uamuzi ambao ungeweza kubadilisha mchezo na kutupa sisi faida.”

🔥 Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa mitandaoni, mashabiki wakigawanyika kuhusu tukio hilo la utata lililoonekana kuwa na athari kubwa kwenye mwelekeo wa mchezo.

Burnley wanaamini tukio hilo lilikuwa hatua ya mabadiliko (turning point) ya matokeo, huku upande wa Arsenal wakiona uamuzi wa mwamuzi ulikuwa sahihi.

VAR na maamuzi ya mwamuzi bado ni mjadala mkubwa baada ya mchezo huo kuisha kwa utata.

19/05/2026

Hello Fans .

Mitaa mbalimbali ya Brazil imetikiswa na shamrashamra kubwa baada ya jina la Neymar kujumuishwa rasmi kwenye kikosi cha Kombe la Dunia!

Maelfu ya mashabiki wamefurika barabarani wakishangilia, wakipeperusha bendera za Brazil 🇧🇷 huku wakifurahia kurejea kwa nyota wao mkubwa katika hatua ya dunia.

🔥 Furaha, vicheko na msisimko mkubwa umeonekana kote nchini, ambapo mashabiki wanasema huu ni “muda wa historia mpya ya Brazil”.

📺 Via: TNT Sports BR

🇧🇷💚💛 Brazil iko tayari kwa vita ya dunia — na Neymar yupo tayari kuongoza safari!

19/05/2026

Hello Fans .

🚨💔 𝐉𝐨𝐚̃𝐨 𝐏𝐞𝐝𝐫𝐨 AFUNGUKA BAADA YA KUACHWA KIKOSI CHA BRAZIL!

Ndoto ya kucheza Kombe la Dunia imeahirishwa… 🇧🇷😔

🗣️ “Nilijaribu kutoa kila kitu muda wote. Kwa bahati mbaya, haikuwezekana kutimiza ndoto ya kuiwakilisha nchi yangu kwenye World Cup.”

“Ninabaki mtulivu na focused k**a kawaida… Furaha na maumivu ni sehemu ya mpira wa miguu.”

“Kuanzia sasa, nawapa kila la kheri waliopo kikosini. Nitakuwa shabiki mwingine tu nikisapoti walete kombe la sita nyumbani!”

Hii ni sauti ya mchezaji mwenye ukomavu wa kiakili (mental resilience) — anakubali maumivu lakini anaendelea kusonga mbele.

🔥 Je, unadhani João Pedro alistahili kuitwa? Tuambie maoni yako!...

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address

Dar Es Salaam