07/04/2025
SIMULIZI: SECRET
MUANDISHI: ALLY H.
Cont: 0677861890
SEHEMU 05
Upepo uliotokea baharini ulileta harufu ya chumvi na maua, na sauti ya muziki wa taarab uliokuwa ukipigwa taratibu kutoka kona ya mgahawa uliongeza mvuto wa mazingira.
Ndani ya mgahawa huo wa kifahari, macho ya Ibra yalimnasa Dabrina mara moja. Alikuwa nyuma ya kaunta ya vinywaji, akihudumia wateja kwa ustadi wa kazi aliyoiweza. Lakini alipoona sura ya mwanamke huyo mrembo, kila kitu kilisimama kwa sekunde chache.
Kulikuwa na huzuni iliyojificha nyuma ya macho yake ya kahawia, lakini bado tabasamu lake lilikuwa na joto la kuweza kuyeyusha barafu.
Ibra alichukua menyu na kujipeleka moja kwa moja mezani alipokaa Dabrina.
“Habari za jioni!". Ibra alisema kwa sauti yenye utulivu lakini iliyokuwa na chembe ya ucheshi.
"Nzuri habari yako nawe!". Kwa upole Dabrina alijibu.
“Habari ni njema kabisa, kwa jina naitwa Ibra, kwa huduma nzuri na ucheshi wa bure karibu sana.”
Dabrina alicheka kidogo. “Asante Ibra. Mimi naitwa Dabrina.”
“Jina zuri sana,” Ibra alijibu huku akiinamisha kichwa kwa heshima. “Karibu Zanzibar, Dabrina.”
"Asante sana!". Dabrina alijibu kisha akatulia na kumtupia jicho muhudumu huyo aliyesimama mbele yake.
“Naomba nikukaribishe kwa mara nyengine kwenye mgahawa wetu kwa chakula kitamu zaidi visiwani Zanzibar. Hapa tunahakikisha huondoki bila tumbo lako kushukuru.”
Dabrina alitabasamu kidogo, lakini hakutaka kuonekana k**a alikuwa akivutiwa. “Sawa, hebu nione kwenye menyu,” alisema huku akichukua orodha ya chakula.
Ibra alitabasamu na kuinamisha kichwa kidogo. “Ningependekeza uanze na supu yetu ya n**i na kamba, inasemekana ikigusa ulimi, unajikuta unarudi hapa kila siku.”
Dabrina alimtazama kwa macho ya kutilia shaka, “Una hakika?”
Ibra alitikisa kichwa. “Mimi siwezi kudanganya mteja mzuri k**a wewe. Na k**a haitakuwa tamu, nitakulipia chakula chote usiku wa leo.”
Dabrina alitikisa kichwa kwa tabasamu dogo. “Sawa, nitakula hiyo. Halafu nataka samaki wa kupaka na wali wa n**i.”
Ibra alipiga makofi kimzaha. “Umechagua sahihi! Chakula hiki kilichangia ndoa nyingi visiwani Zanzibar hasa wali wa n**i, ukisikia harufu yake tu, moyo wako unayeyuka!”
Dabrina alicheka kidogo. Hakuamini k**a mhudumu angeweza kuwa na ucheshi kiasi hicho.
“Na kwa vinywaji?” Ibra aliuliza.
“Juisi ya nanasi,” alijibu..
Muda haukupita, chakula chake kililetwa. Harufu nzuri ya n**i na viungo vya Zanzibar ilijaza hewa, na Dabrina alihisi furaha isiyoelezeka alipouonja ule wali.
“Mmmh… ni kweli, chakula hiki kina mvuto wa ajabu,” alisema huku akimtazama Ibra kwa jicho la pili.
Ibra alitikisa kichwa kwa tabasamu. “Nilikwambia, ukiondoka hapa kesho, moyo wako utabaki kwenye hii hoteli.”
Dabrina hakusema chochote, lakini kwa namna fulani, alihisi k**a maneno ya Ibra yalikuwa na maana zaidi ya chakula.
Baada ya chakula, alikaa kwa muda akitazama mawimbi ya bahari kupitia dirisha kubwa la mgahawa. Miale ya jua iliyokuwa ikizama baharini ilitengeneza mandhari ya kupendeza, k**a picha ya tumaini iliyochorwa juu ya huzuni yake. Kulikuwa na hali ya utulivu ambayo aliihitaji sana usiku huo.
***********************************
Asubuhi ilipofika, anga lilikuwa na mawingu mepesi na upepo wa bahari ulikuwa bado wa upole. Dabrina aliamka mapema, akajifungasha kwa ajili safari.
Alilipa bili yake mapokezi, akavua hereni zake kubwa na kuzihifadhi, kana kwamba alitaka kusahau kila kitu kilichompendezesha usiku uliopita. Mapema sana alowahi bandarini kuchukua boti ya mapema kuelekea Tanga, akiwa na mzigo mmoja wa nguo lakini mzigo mkubwa zaidi ulikuwa moyoni mwake.
Asubuhi hiyo ilikuwa tofauti kwa Ibra. Alipoamka, alijikuta akifanya maandalizi ya kwenda kazini kwa haraka lakini kwa hisia mpya ambazo hakuwa nazo siku zilizopita.
Alitembea kuelekea hotelini huku moyo wake ukiwa na shauku isiyoelezeka. Kila hatua ilimbeba kwenye matarajio ya kumuona tena mrembo yule aliyempokea jana usiku. "Dabrina" alijiambia kimoyomoyo, jina lake likiingia kwenye fikra zake k**a wimbo wa taratibu wa baharini.
“Hakika, ni mwanamke mzuri kuwahi kutokea mbele ya macho yangu,” alijiwazia.
Alipofika hotelini, alikutana na taarifa ambayo hakuitarajia. Dabrina alikuwa ameshaondoka.
Moja kwa moja, alielekea sehemu ya mapokezi ya wageni. Akapitia orodha ya wageni kuona k**a angebahatika walau kupata mawasiliano lakini kwa bahati mbaya juhudi zake ziligonga mwamba, aliziona namba za Dabrina lakini kulikosekana tarakimu moja, namba za simu alizotafuta hazikutimia zilikuwa tisa tu. Inaonekana aliandika kwa haraka, au labda kwa kuchanganyikiwa wakati wa kujaza fomu alisahau kumalizia.
Ibra alisimama pale kwa muda, akinyamaza huku macho yake yakikodolea jina lake tu.
"Namba haijakamilika..." alijisemea kwa sauti ya chini, k**a akizungumza na hewa. Akaweka daftari chini kwa upole, k**a vile lina mabaki ya mtu aliyekuwa muhimu.
Alijikuta akienda kukaa kwenye meza ile ile ambayo Dabrina alikalia. Alijishika kichwani kwa mkono mmoja, akihema taratibu. Hakujua kwa nini alihisi pengo hilo kubwa. Alijilaumu, "Kwa nini sikuuliza namba yake? Kwa nini niliruhusu aondoke bila kusema lolote?"
Kulikuwa na huzuni isiyoelezeka machoni pake. Mgongoni mwake palijaa uzito wa jambo ambalo hakuwa nalo tena nafasi iliyompita, kimya kilichomuuma zaidi kwa sababu hakikutoa nafasi ya pili.
"Nitamwona tena?". Alijiuliza bila kuwa na jibu sahihi.
****************************
Upande wa pili, Dabrina alikuwa ameketi karibu na dirisha la boti ya kisasa iliyokuwa ikielekea Tanga. Wakati huo bahari iling’aa kwa miale ya jua la asubuhi.
Dabrina alikuwa kimya, lakini ndani ya moyo wake kulikuwa na tafakari nyingi. Alijisikia vizuri kwa namna alivyopokelewa Zanzibar. Huduma ya hoteli ilikuwa ya kuvutia, vyumba safi na vyenye harufu ya maua, chakula kitamu kilichojaa viungo vya pwani lakini zaidi ya yote, huduma ya mhudumu mmoja wa mgahawa ambaye hakumsahau hata baada ya kuondoka.
Aliukumbuka ucheshi wa Ibra vile alivyomwelezea supu ya kamba na n**i, ahadi yake ya kulipia chakula endapo hakingekuwa kitamu, na maneno yake ya mwisho kuhusu juisi ya limau kusababisha ndoto za ajabu.
Alitabasamu mwenyewe, halafu akatikisa kichwa.
“Yule mhudumu alikuwa na ucheshi wa ajabu... sijui kwa nini? ananikumbusha namna mtu anatakiwa kuwa na utu, hata kwa wageni,” alijiambia kimoyomoyo.
Alihisi furaha ya ndani, si kwa sababu ya Ibra tu, bali kwa sababu kwa mara ya kwanza katika siku nyingi, alihisi kuguswa na utu wa mtu asiyejua chochote kuhusu maumivu yake ya moyo.
Alikumbatia mkoba wake kifuani, akajiinamia, akitazama bahari nje ya dirisha. Safari ya kurudi Tanga haikumaanisha tu kurudi nyumbani ilimaanisha pia kuondoka sehemu iliyomgusa kidogo zaidi ya alivyojiandaa.
Lakini moyoni, alikuwa na hisia kwamba siku moja, k**a bahari haikumsahau, basi huenda atarudi tena Zanzibar.........
ITAENDELEA.......
USIKOSE SEHEMU INAYOFUATA........
06/04/2025
05/04/2025
04/04/2025
04/04/2025