07/04/2026
Hongera wanamichezo wote kwa juhudi kubwa mlizoonyesha uwanjani! πͺβ½
Mchezo kati ya Magunga 0 dhidi ya Milani 1 umehitimishwa, na licha ya matokeo, bado mmeonesha moyo wa kupambana, nidhamu na uzalendo wa hali ya juu. Kumbukeni, ushindi sio mwisho wa safari bali ni hatua, na kushindwa sio mwisho bali ni funzo la kujijenga zaidi.
Kwa timu ya Magunga, pigeni moyo kondeβkila changamoto ni nafasi ya kujirekebisha na kurudi imara zaidi. Kwa Milani, hongereni kwa ushindi, endeleeni kudumisha kiwango na nidhamu.
Twendeni tukazidi kushirikiana, kujifunza na kuendeleza vipaji vyetu kwa ajili ya maendeleo ya mpira wetu wa wilaya. π₯β½
Mpira unaendelea, safari bado ndefu!
04/04/2026
Matokeo ya mchezo uliochezwa katika uwanja wa TTC yamekamilika k**a ifuatavyo:
Rising Stars 1 β 3 Golden Generation
Kwa leo ikiwa ni siku ya ufunguzi, mchezo umehitimishwa rasmi.
Tunawakaribisha wadau wote wa michezo kuendelea kujitokeza kwa wingi kesho kwa mchezo mwingine utakaoendelea.
Karibuni sana! β½π₯
18/05/2025
Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Korogwe (KDFA) kinapenda kuwataarifu wadau wote wa michezo na wapenda soka kuwa kutakuwa na Kozi ya Ukocha wa Mpira wa Miguu Ngazi ya Awali (Basic Coaching Course) itakayofanyika hivi karibuni.
Kozi hii inalenga kuwajengea uwezo watu wanaotamani kuwa makocha wa soka kwa ngazi za awali na kuanza safari yao ya ukocha kwa ufanisi
04/04/2025
Ndio, Manchester FC wameibuka kidedea baada ya kushinda kwa mikwaju ya penalti 5-4 dhidi ya Magoma FC katika uzinduzi wa ligi ya wilaya ya Korogwe.Ulikuwa mchezo wa kusisimua!
03/04/2025
π’ LIGI YA WILAYA YA KOROGWE KUZINDULIWA RASMI! β½π₯
Leo ni siku kubwa kwa soka la Korogwe! Tunafungua rasmi Ligi ya Wilaya ya Korogwe katika Kata ya Magoma, tukishuhudia vipaji vya mpira wa miguu kutoka wilaya yetu.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huu ni Mbunge wa Korogwe Vijijini, Mheshimiwa Mzava. Tunamkaribisha kwa heshima kubwa kushiriki nasi katika tukio hili muhimu kwa maendeleo ya soka letu.
Wananchi wote mnakaribishwa kuja kushuhudia mechi za kusisimua na kuunga mkono vijana wetu! πβ½
03/04/2025
π’ LIGI YA WILAYA YA KOROGWE KUZINDULIWA RASMI! β½π₯
Leo ni siku kubwa kwa soka la Korogwe! Tunafungua rasmi Ligi ya Wilaya ya Korogwe katika Kata ya Magoma, tukishuhudia vipaji vya mpira wa miguu kutoka wilaya yetu.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huu ni Mbunge wa Korogwe Vijijini, Mheshimiwa Mzava. Tunamkaribisha kwa heshima kubwa kushiriki nasi katika tukio hili muhimu kwa maendeleo ya soka letu.
Wananchi wote mnakaribishwa kuja kushuhudia mechi za kusisimua na kuunga mkono vijana wetu! πβ½
22/12/2024
β½ FAINALI YA KDFA POST UCHAGUZI CUP! π
π Uwanja wa Magereza Stadium, Korogwe
π
Tarehe: Jumatatu, 23 Desemba 2024
β° Muda: Saa 9:30 Alasiri (15:30 EAT)
π₯ Ni vita ya mwisho! Mombo Mji π Manundu katika pambano la kukata na shoka!
π Mgeni Rasmi: Ndg. Athumani Nyamlani, Makamu wa Kwanza wa Rais wa TFF
π Mashabiki wa soka, usikose kushuhudia historia inavyoandikwa. Jitokezeni kwa wingi kuungana nasi kwenye fainali hii ya kusisimua!
π₯ Korogwe imechagua kwa amani, sasa tufurahi soka!
21/12/2024
π FULL TIME: MATOKEO YA NUSU FAINALI!
π KDFA Post Uchaguzi Cup
π Uwanja wa Sokoni Stadium
β½ Manundu 2οΈβ£ - 1οΈβ£ Kilole
π₯ Manundu wamefuzu kwa fainali baada ya ushindi wa mabao mawili dhidi ya bao moja la Kilole katika mechi ya kusisimua! π
π Shukrani kwa mashabiki wote waliokuja kushuhudia nusu fainali hii kali. Fainali sasa ni kati ya Manundu na Mombo Mji! Jiandae kwa burudani zaidi.
π₯ Korogwe imechagua kwa amani, sasa tufurahi soka!