30/08/2026
𝗣𝗥𝗘𝗦𝗦 🎙️ Young Africans Sports Club
“Hizi ni miongoni mwa mechi ngumu na ni muhimu sana Kushinda, tunafahamu Fountain Gate wana mwalimu mzuri ambaye amewahi kuwa sehemu ya Benchi la Yanga hivyo anajua tamaduni za klabu, Ni mzoefu na ana wachezaji wazuri, Sisi k**a Yanga tunapaswa kufanya kazi kubwa ili kushinda kesho”
“Tunafahamu wapinzani wetu wamepoteza michezo kadhaa hapo nyuma lakini jukumu letu ni kuheshimu kila mchezo, tumewaangalia Fountain Gate namna wanavyocheza na leo tunakwenda kufanya maandalizi ya mwisho ya kucheza nao, naamini tutakuwa na Mechi nzuri”
“Nawaomba sana Wananchi waje kwa Wingi, wao ni muhimu sana kwa timu, ni muhimu pia Kwangu k**a kocha kwasababu wananipa morali ya kufanya vyema kila siku, nawashukuru sana kwa sapoti yao tangu tumefika hapa nchini na nawaomba kesho waje ili tushinde pamoja”
🗣️ Manqoba MNGQITHI
28/08/2026