Soka updates

Soka updates

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Soka updates, Sports, Tanga.

pata habari na taarifa zote za soka( ndani na nje nchi )
kipi kinachoendelea na kipi kinachojiri.
:Uchambuzi wa soka
:Na taarifa zote za wachezaji timu,viongozi pamoja na yale yote yanayolenga kuhusu mchezo wa soka.

02/03/2026

Kanuni ya Ligi Kuu ya Nbc kuhusu straight Red Card itamfanya Feisal Salum ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ azikose mechi mbili zijazo dhidi ya Tz Prisons na Mbeya Kwanza.

K**a ataongezewa adhabu hizi ni mechi zijazo za Azam Fc

โœ… Tz Prisons (Machi 5)
โœ… Mbeya Kwanza (Machi 8)
โœ… Dodoma Jiji (Machi 11)
โœ… Young Africans (Machi 15)
โœ… Mashujaa Fc (Machi 19)

02/03/2026

๐Ÿšจ Mbio za ubingwa katika ligi kuu Hispania LA LIGA baada ya matokeo ya leo.Je nani kuibuka kuwa bingwa msimu huu 2025/26

02/03/2026

๐Ÿšจ ๐๐‘๐„๐€๐Š๐ˆ๐๐†: Mashabiki wa REAL MADRID wanaimba na kutaka kujiuzulu kwa raisi wa klabu hio FLORENTINO PEREZ ndani ya uwanja wa BERNABEU. โšช๏ธ๐Ÿ˜ฑ

02/03/2026

Hali tete BERNABEU kwa wapenzi na mashabiki wa REAL MADRID wamepotea alama 3 nyumbani dhidi ya GETAFE FC

02/03/2026

NDANI YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE:
2016-real madrid kamtoa Manchester city
2020-manchester city kamtoa real madrid
2022-real madrid kamtoa Manchester city
2023-manchester city kamtoa real madrid
2024-real madrid kamtoa Manchester city
2025-real madrid kamtoa Manchester city
2026?

02/03/2026

๐Ÿšจ๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡น Klabu ya Manchester United imeanza kufanya mawasiliano ya awali na wawakilishi wa viungo wawili nyota, Bruno Guimarรฃes na Sandro Tonali, kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la Hispania la michezo, Diario AS.

Chanzo hicho kinaeleza kuwa mawasiliano hayo bado ni ya kiwango cha chini (informal contact), yakilenga kupima uwezekano wa usajili siku zijazo. Hadi sasa hakuna makubaliano rasmi yaliyofikiwa kati ya pande husika.

02/03/2026

๐Ÿšจ๐‡๐€๐๐€๐‘๐ˆ ๐Œ๐๐˜๐€: Kocha wa mipira ya adhabu (set-piece) wa Arsenal, Nico Jover, ana kipengele maalum kwenye mkataba wake kinachompa bonasi kila timu inapofunga bao kupitia set-piece.

The Athletic

02/03/2026

ANAANDIKA ALLY KAMWE.

Kwanza ilikuwa OFFSIDE.. Pili, AKASHIKA. Move ikaruhusiwa kuendelea k**a hakijatokea kitu.

Sitaki kabisa kukumbusha kuwa Mchezaji huyu alitakiwa kufungiwa MECHI 5 kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa Dodoma Jiji โ€ฆ

Sitaki kuwakumbusha, kuwa Waamuzi walishatishiwa kufungiwa Maisha kimpira na kupelekwa JELA kuhusu mechi hii

Turidi uwanjani, Watu hawa baada ya mazoezi ya mwisho siku moja kabla ya mchezo, wakagoma kuondoka uwanjani Usiku.. Wakafanya Ushirikina na vurugu za kila aina.. Wakaja kutolewa kwa msaada wa Polisi

Hawakumaliza, Siku ya mechi wametumia mlango wa VVIP kuingia uwanjani. Wakavunja mlango wa chumba cha Waandishi wa Habari

Muda wa Pitch Feeling, wakautumia kuzunguka uwanja na kufanya vitendo vya Kishirikina bila wasiwasi wote

Hapa Najaribu kuwaonyesha kwa uchache tu NGUVU iliyotumika hadi Makolo wamepata POINTI 1 kwenye Derby

Kimsingi, kwa mtu anayejua Mpira vizuri atakubaliana na mimi.. JANA SIMBA wamethibitisha ni WADOGO SANA KWA YANGA na watatumia miaka mingi sana kuja kushinda Derby

Nguvu yote kubwa sana Ilitumika ndani na nje ya uwanja haijaweza kufuta Uteja wao. Wana kikosi chenye wachezaji machachari na Viongozi wenye mihemko

K**a isingekuwa mambo ya kupelekana JELA, ikapigwa FAIR, Prince Dube angewaweka ile chuma ndio mngeona mengi zaidi jana..

Wanazuga Kulalamika na kutukana watu leo ili kuficha Vitu vya hovyo walivyofanya na Wameshindwa kupata Ushindi .. Hii inawauma sana

KULIWA MARA 6 Imebaki pale pale na POINTI 5 ZIMESIMAMA VILEVILE ๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ๐Ÿ™Œ๐Ÿฝ

02/03/2026

Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

02/03/2026

๐Ÿšจ ๐—•๐—ฅ๐—˜๐—”๐—ž๐—œ๐—ก๐—š: Sheria Mpya nne zitakazotumika kombe la Dunia

1. Mchezaji akifanyiwa mabadiliko anatakiwa atumie Sekunde 10 tu awe tayari ametoka Njee akizidisha hata sekunde 1 itamalzimu Mchezaji anayeiingia Kusubiri Njee angalau dakika 1 ndio ataingia.

2. Ikiwa Mchezaji kaumia na anaitaji matibabu atatakiwa kutolewa Uwanjani kwa dakika 1 akizidisha timu yake ikapewa adhabu.

3. Ikiwa Mwamuzi ataona muda unapoteza kwenye mpira wa kona au mpira wa kurusha kwa zaidi ya Sekunde 5 Mwamuzi ataamua Timu Pinzani kupewa Faida ya kutumia Nafasi hiyo.

4. VAR Itatumika kuangalia kadi ya Njano ya Pili na Mpira wa Kona

02/03/2026

๐Ÿšจ Michezo Miwili Ijayo ya Aston Villa Kutetea kubakia Top 4. ๐Ÿซฉ

๐ŸŸ Aston Villa FC โš”๏ธ Chelsea FC

๐ŸŸ Manchester United โš”๏ธ Aston Villa FC

โœ๏ธ Ikiwa Aston Villa atapoteza yote atajikuta yuko nafasi ya 6. ๐Ÿ™„

02/03/2026

๐Ÿšจ Arsenal bado wakiwa juu ya msimamo wa EPL!

Mbio za ubingwa zikiendelea na Manchester ctiy...NANI KUWA BINGWA WA EPL 2025/26?๐Ÿ†๐Ÿ‘€

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Tanga?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address

Tanga