29/09/2021
Try Again afunguka baada ya kuteuliwa Simba...
NIMERIDHIA. Hiyo ni kauli ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba Salim Abdallah 'Try Again' baada ya Mohamed Dewj 'Mo' kujiuzulu nafasi hiyo.
Ni kweli Mohamed ameachia hiyo nafasi, na mimi ndiye nitachukua nafasi yake, nimeipokea kwa mikono miwili naamini kwa kushirikiana na wenzangu tutafikia malengo yetu,"amesema.
15/11/2020
Mzee kabidhi timu yao wamesha kuchoka kwanza wana sema kwanini huvai jezi ya club k**a huna size yako useme mbona Mwakalebela wame mshonea yake...Natabiri hapo yanga hauna week moja wana kuondoa kaka yangu Simon
14/11/2020
Mwakinyo anasema yeye anataka kuwa World Champions kumpiga Mtu Marekani, Twaha kiduku atafute mabondia wa kweli wa kumchallange, asituletee wauza Uyoga, sijui watu wa Comedy, sijui walevi
10/11/2020
-"Nafahamu Simba SC sio timu kubwa Afrika, lakini wana mwalimu mzuri (Sven), wanacheza soka safi sana, wanakaa na mpira na kudhibiti wapinzani kuwashambulia. Tunafahamu udhaifu wetu na ubora wetu. Tumejipanga vyema"
🗣️Abdul Mwaikaba kocha wa Plateau
06/10/2020
OCTOBA 18 YANGA ANA NAFASI ILA AFANYE HAYA
Mara ya mwisho kukutana hapo Matokeo yake yalishangaza sana, Yanga alipigwa bila huruma Goli nne kwa Moja, Yani alipigwa Nne na Akapigiwa Pira Sambusa.
Matokeo ya Mechi ijayo kiukweli anayo Mungu tu ila Sisi mashabiki tunakuwaga na uwezo wa Kuhisi tu Matokeo kutokana na Mwenendo wa Hizi timu.
Kikuweli ile Yanga iliyopigwa Nne sio hii ya msimu huu hata kidogo lakini pia ile Simba iliyopiga nne sio hii kabisa japo haijaongezeka sana.
Mechi ijayo Heshima pekee ambayo Yanga wanaisaka sasa ni kushinda huu mchezo ili kufuta ile Nne tunayoikumbuka,
Ili Yanga ashinde huu mchezo lazima kwanza afanye Yafuatayo
1. Aingie uwanjani kucheza mpira sio kulipiza kisasi.yani asiingie kwa lengo la kulipa aingie kusakata Soka safi na kutafuta Magoli
2. Ulinzi imara, kiukweli katika timu ambazo hautakiwi kuzishambulia kizembe ni Simba wana uwezo mkubwa sana wa kusak**a lango lako hasa beki zako zikiwa Zimetoka
3. Yanga wahakikishe wanaingia uwanjani wakiwa hawana makando kando nje ya uwanja (sjui mnaelewa) yani wahakikishe timu nzima inaingia na akili moja sio huyu anawaza mkataba huyu anawaza mshahara hajapewa. Watapigwa tena.
4. Hata k**a Morrison ataanza ila Yanga wasimuwaze kabisa wala wasihangaike naye, maana wanaweza kuingia wakiwaza kumkaba ili aaibike wakasahau Simba kila mtu anajua kufunga waingie na mpango wa kuizuia timu nzima.
5. Yanga mpaka sasa hawana kocha (kosa kubwa sana) Yanga ili wawe sawa wampe majukumu Mwalimu Mwambusi kwenye huo mchezo ila wakitaka kumvuruga wamletee kocha hapa katikati kabla ya Octoba 18, wataivuruga timu Kocha mpya aje baada ya hii mechi.
6. Yanga waepuke kutoa dau kwenye huu mchezo yani yale mambo ya mkishinda mnapata million kadhaa, sjui kila anayefunga anapewa million kadhaa yatawavuruga sana maana kila mchezaji anaitaka hela hawatacheza kitimu.
7. Mwisho kabisa Yanga anahitaji Kuingia na mbinu zake za siku zote ila wasije wakajaribu kuiga zile biriani za simba, zile wamezifanyia mazoezi Miaka sita nyuma ndio wanazifanya sasa.
ALL IN ALL CHAMA NA KONDE BOY MPAKA SASA NI WAZIMA WA AFYA
10/07/2020
Yanga wajichimbia kuiwinda simba
.
Kocha wa yanga Lic Eymael akiwaelekeza mbinu za kiwafunga simba julai 12 pale taifa..
08/07/2020
DIMBA LA MAJALIWA: Maandalizi yote yamekamilika kuelekea mchezo kati ya Namungo FC dhidi ya mabingwa Simba SC pamoja na sherehe za kukabidhi kombe. Tayari mashabiki wameshaanza kuingia.
Mechi ni saa 9:00 alasiri
07/07/2020
Rostam Kaka Tuchat Remix
Azam: Oi oi naona mtandao unakatika uko kimya sana Yanga au nguvu zimekuisha??
Yanga: Na utanyooka raundi hii na hivi huwezi bila mimi??
Azam: FA unajiona bingwa kwani Nusu Fainali lini??
Yanga: Kaka huku Simba yupo alikufunga Robo Fainali umesha sahau tayari??
Azam: Na raundi hii ikimbie mechi hiyo alikutafuta amekupata na safari hii utamkoma!!
Yanga: Mmmhh basi kumekucha msimamo vipi nipe matokeo kati yako na Singida??
Azam: Nimeipiga wiki na nafac ya pili nimekutoa.
Yanga: Umemshusha daraja??
Azam: Simba nimewavulia kofia walimpiga nane ila me nimeshindwa kufikia.
Yanga: Simba habari ya mjini japo nina pinga ila ukweli naujua, Simba kila mtu lake analijua Lui Mik alimzungusha Kangwa nilishangilia japo niliumia!
Azam: Simba kila mtu anapiga tobo sijui nani kawafundisha??
Yanga: Huku kwangu hadi Kocha kaukubali huo mziki.
Azam: Leo tuuseme ukweli Robo Fainali ulibebwa??
Yanga: Sio hilo tu timu NNE Caf wao ndio chanzo, hapa nawaza bila wao sijui Soka la Bongo lingekuwaje..........??
15/06/2020
Sven ndani Simba Sc.
:
Kupitia ukurasa mnamo Dec 11, 2019 Simba Sc walimtambulisha Kocha Sven.
:
Waliandika hivi!Sven Vanderbroeck mbeligiji aliyewahi kufundisha timu ya taifa ya zambia ndiye kocha mpya wa mabingwa wa soka wa taifa hili Simba Sc.
:
Kocha huyo kijana pia alishinda ubingwa wa afrika ( AFCON) akiwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Cameroon mwaka 2017.
:
Klabu inaamini kocha Sven ataleta matokeo chanya kwetu na inaahidi kumpa kila ushirikiano ili kutumiza malengo ya klabu yetu .
:
NB: Katika utambulisho huo Simba Sc haikuanisha mkataba ni wa muda gani wamempatia Kocha Sven.
:
Kwa mujibu wa "Transfermarkt" inaonyesha Sven alisaini mkataba December 12, 2019 mara baada
ya kutambulishwa na ukomo wa mkataba wake ni June 30, 2020.
Kwa mtazamo wako sven apewe mkataba mpya au simba watafute mwalimu mwingine
Like, share ili uwe wa kwanza kupata habari mpya
12/06/2020
Walioko juu wamesafiri kwa Ndege!
Walioko chini wamesafiri kwa Bus haya maisha haya bana dah
Halafu huyu Nugaz safari ya Siku 1 unabeba begi kubwa hivyo la nini? Au amekuwa mtunza vifaa wa team? Nawaza tu kwa sauti ya chini hapa
08/06/2020
Mimi ni msemaji mwenye maono na mwenye kuijua timu na klabu yangu,,sasa nasema hivi, back 2 back siyo kumi tena ni ISHIRINI,,Dadadeki 😀Haji Manaraa msemaji wa simba
Like, share ili uwe wa kwanza kupata habari mpya
07/06/2020
Sio Kweli, Wanatuficha Tu Yaan Sisi LA LIGA Tufungwe 3 na KMC?, Hawa Wachezaji Kuna Kitu Wameongezeka Sio UZITO pekee .......😁😂🤣😀