18/03/2026
CAF jamani CAF nyie
Klabu inayoshiriki Ligi Kuu Misri, Pharco FC imetangaza kususia kwa muda usiojulikana Mashindano yote yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Klabu hiyo imethibitisha kwamba imesusia michuano yote ya CAF, ikiwa ni pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika, Kombe la Shirikisho la CAF, Kombe la CAF Super Cup, na Mashindano yoyote chini ya Shirikisho la soka Afrika.
Msimamo huu mkali unakuja kutokana na uamuzi wenye utata baada ya CAF kuitangaza Morocco kuwa washindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika la 2025.
Hata hivyo, kauli hiyo tangazo hilo limeibua hisia kwa sababu Pharco FC si washiriki wa mashindano ya CAF, maelezo ambayo yamesababisha wengi kuona tangazo hilo k**a lililojaa ucheshi.
09/09/2025
09/07/2024