06/05/2026
Kwa heri Kocha
Pata Taarifa mbalimbali za Michezo
06/05/2026
Kwa heri Kocha
17/02/2026
Hii hapa ratiba ya robo fainali ya kombe la Shirikisho Afrika
➡️Al Masry SC vs CR Belouizdad
➡️Olympic Club Safi vs Wydad AC
➡️AS Otohô vs Zamalek SC
➡️AS Maniema Union vs USM Alger
Nnai Unmpa Nafasi Ya Kwenda NUSU FAINALI
FABI Sports ANGLE
16/02/2026
Kocha Miguel Gamondi amesaini mkataba wa miaka 2 kuifundisha timu ya taifa ya Tanzania [ Taifa Stars ] hii ni baada ya kukaimu nafasi hiyo kwa muda kwenye AFCON iliyopita na kuifikisha Stars hatua ya 16 bora.
Kwenye Picha : Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia na Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania Miguel Gamondi wakisaini mkataba.
FABI Sports ANGLE
17/12/2025
❤️💙🏆 Paris Saint-Germain waandika historia, waibuka mabingwa baada ya kuifunga Flamengo
Paris Saint-Germain (PSG) wameandika historia kubwa katika soka la dunia baada ya kuifunga Flamengo na kutwaa FIFA Intercontinental Cup, ushindi uliowezesha klabu hiyo kukamilisha Sextuple ya kipekee msimu huu.
🏆 Mataji yote yaliyoshindwa na PSG: 🔵 Ligue 1
⚪ Coupe de France
🔴 Trophée des Champions
🇪🇺 UEFA Champions League
🇪🇺 UEFA Super Cup
🌍 FIFA Intercontinental Cup
Ushindi huu unaifanya PSG kuingia kwenye vitabu vya historia k**a moja ya klabu chache duniani zilizowahi kushinda mataji sita makubwa ndani ya msimu mmoja, mafanikio yanayoonyesha ubora, uthabiti na nguvu ya kikosi chao katika ngazi ya ndani na kimataifa.
FABI Sports ANGLE Fabius Clavery
05/12/2025
🚨 MAKUNDI YA KOMBE LA DUNIA 2026
◉ A: Mexico, South Korea, South Africa + Winner Playoff D*
◉ B: Canada, Switzerland, Qatar + Winner Playoff A*
◉ C: Brazil, Morocco, Scotland, Haiti
◉ D: USA, Australia, Paraguay + Winner Playoff C*
◉ E: Germany, Ecuador, Ivory Coast, Curação
◉ F: Netherlands, Japan, Tunisia + Winner Playoff B*
◉ G: Belgium, Iran, Egypt, New Zealand
◉ H: Spain, Uruguay, Saudi Arabia, Cabe Verde
◉ I: France, Senegal, Norway + Winner Playoff 2
◉ J: Argentina, Austria, Algeria, Jorgan
◉ K: Portugal, Colombia, Uzbekistan + Winner Playoff 1
◉ L: England, Croatia, Panama, Ghana
20/06/2025
Matokeo ya mechi zote za jana michuano ya Kombe la Dunia ngazi ya klabu
30/04/2025
LIGI Kuu ya NBC, Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika itarejea Mei 2 kwa mchezo kati ya Simba itakayokuwa mwenyeji wa timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma.
Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa KMC Complex uliopo mkoani Dar es Salaam ikiwa ni mchezo wa mzunguko wa 24 uliosogezwa kutokana na timu ya Simba kuwa na ratiba ya michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Baada ya mchezo huo timu ya Simba itakuwa na kibarua kingine ugenini katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar watakapokutana na timu ya JKT Tanzania waliyoifunga 1-0 kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza kwa bao la Jean Ahoua aliefunga kwa mkwaju wa penati dakika za nyongeza.
Mei 8 itaikaribisha timu ya Pamba katika uwanja wa KMC Complex kabla ya kwenda ugenini kuvaana na timu ya KMC kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.
Tanzania Football Federation
19/04/2025
BASHUNGWA AFUNGUA LIGI YA DK. SAMIA & KYOMBO - MISSENYI
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb), amezindua Mashindano ya Mpira wa Miguu ya Dk. Samia & Kyombo Cup 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Bunazi, wilayani Missenyi, mkoani Kagera, leo tarehe 19 Aprili 2025.
Mashindano hayo yameandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Missenyi, Dkt. Florent Laurent Kyombo, na yanatarajiwa kushirikisha timu 20 kutoka kila kata ya wilaya hiyo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Bashungwa amesema kuwa mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji vya michezo kwa vijana, kuimarisha afya, kuendeleza mshik**ano na kudumisha upendo miongoni mwa vijana na wakazi wa Wilaya ya Missenyi.
“Mhe. Mbunge kwa kushirikiana na Madiwani wameonyesha dhamira ya dhati katika maendeleo ya michezo ndani ya Wilaya ya Missenyi. Ligi hii siyo tu burudani bali pia ni fursa kwa vipaji chipukizi. Naomba vijana kutoka kata zote 20 mshiriki kwa moyo wa upendo na mshik**ano,” alisema Mhe. Bashungwa.
Aidha, Waziri Bashungwa ametoa wito kwa waamuzi na wasimamizi wa mashindano hayo kuhakikisha wanatenda haki wakati wa michezo yote, ili ligi hiyo imalizike kwa amani na kutimiza malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Missenyi, Dkt. Florent Kyombo, amesema kuwa mashindano hayo yanalenga kuimarisha mahusiano na mshik**ano kati ya vijana na wananchi wa kata zote 20 za wilaya hiyo.
Katika hafla ya uzinduzi, ambayo ilizikutanisha timu za kata za Kyaka na Mtukula, timu zote shiriki zilipatiwa vifaa mbalimbali vya michezo, ikiwemo jezi, mipira, vifaa vya mazoezi, pamoja na fedha kwa ajili ya maandalizi ya mechi.
18/04/2025
MAFUNZO YA VAR
Kozi maalum ya Teknolojia ya Msaidizi wa Video (VAR) iliyofanyika kwa takribani siku 5 kwenye ukumbi wa uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es salaam imefungwa rasmi leo Aprili 18, 2025 ikijumisha waamuzi 20 kutoka Tanzania Bara na Visiwani ikiwa ni mwendelezo wa Kozi hiyo yenye jumla ya moduli 6 mpaka kuhitimisha.
Kozi hiyo ambayo ni sehemu ya mkakati wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuhakikisha nchi inakuwa na waamuzi waliobobea kwenye matumizi ya teknolojia hiyo ya kisasa inayotumika kusaidia kutoa maamuzi sahihi uwanjani imefungwa rasmi Kwa awamu ya pili na Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa TFF Boniface Wambura ambaye pia ndio msimamizi Mkuu wa Kozi hiyo inayowezeshwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Akizungumza baada ya kufunga rasmi awamu ya pili ya Kozi hiyo Mkurugenzi wa Sheria, Habari na Masoko wa TFF, Boniface Wambura aliwapongeza waamuzi waliomaliza mafunzo hayo na kuwataka kwenda kutumia vyema ujuzi walioupata kwa maendeleo ya soka la Tanzania.
Aidha Wambura alieleza kuwa Kozi hiyo ni mwendelezo na kwamba TFF itaendelea kuwekeza kwenye teknolojia hiyo Kwa kutoa elimu Kwa waamuzi wengi zaidi na hata kuzalisha wakufunzi wazawa ili kuhakikisha usimamizi wa mechi nchini unaendana sawa na mabadiliko kulingana na wakati Kwa kufuata viwango vya kimataifa.
“Tunahitaji kuona mabadiliko chanya kwenye usimamizi wa mechi nchini, hivyo kupitia VAR tunaamini tutapunguza malalamiko dhidi ya waamuzi.
Ikumbukwe kozi hiyo ni hatua muhimu kuelekea maandalizi ya matumizi rasmi ya VAR katika mechi za ligi kuu ya NBC na mashindano mbalimbali yatakayofanyika ndani ya Tanzania.
Tanzania Football Federation
16/04/2025
VIKOSI MECHI ZA LEO
Real Madrid C.F. VS Arsenal
Inter VS