Soka Viwanjani

Soka Viwanjani

Share

Follow page hii kwa habari za michezo za Soka.

28/09/2022

Chelsea wana kipengele cha kumnunua tena Tammy Abraham kwa Euro milioni 80 ambacho kitaanza kutumika majira ya joto. Imeelezwa Chelsea wanamtaka tena Abraham.

Lakini Tammy ana furaha akiwa Roma chini ya Jose Mourinho.

💥

28/09/2022

Lakini jamaa ameondoka akiwa staa. Nchi nzima imeimba jina lake. Alikuja Simba account yake ikiwa na followers 8,000. Kufkia leo amekuwa na followers 71.3k na idadi inazidi kuongezeka.. hii inaonyesha jamaa alikuwa anafatiliwa sana.

Kila la heri mzungu. Ila Yanga wanaweza kumchukua January 😅

💥

28/09/2022

Wilfried Zaha ameamua kuwekeza katika nchi yake kwa kununua klabu ya soka! Amenunua klabu ya Espoir Club d'Abengourou, inayocheza ligi daraja la 4.

Zaha pia ana academy ya soka nchini kwao Ivory Coast 🇨🇮

💥

28/09/2022

Mshambuliaji wa Simba, Dejan amethibitisha kwa kuvunjwa mkataba baina yake na Simba Sc. Dejan ameandika:

"Ninathibitisha kwamba mkataba wangu wa ajira umesitishwa kwa sababu za haki kutokana na ukiukwaji wa kimsingi wa mkataba na klabu.

Asanteni mashabiki kwa support na upendo mlionipa"

Mlete mzungu si mchezaji wa Simba Tena ❌

💥

28/09/2022

2002 fainali za Kombe la Dunia kati ya Ujerumani na Brazil iliwekwa k**ari matata sana, huku German wakijivunia golikipa wao mashuhuri kwelikweli Oliver Kahn na huku Brazil wakijivunia mshambuliaji wao hatari kabisa Ronaldo De Lima.

Ikawa ni majivuno kati ya Oliver Kahn na Ronaldo De Lima. Kahn aliapa kamwe hatafungwa na Ronaldo katika fainali ni bora afungwe na mchezaji mwingine lakini sio Ronaldo. Ronaldo nae aliapia kuwa atamfunga Kahn kuanzia mabao mawili na kuendelea na k**a atafunga bao moja Basi atatoa nyumba zake na magari yake yoote ya kifahari kwa Oliver Kahn.

Kufkia mapumziko ubao unasoma 0-0 wachezaji wa Ujerumani walipongezana kwa kumdhibiti Ronaldo. Hakupiga shuti hata moja. Kipindi cha pili kilianza mpaka kufkia dakika ya 60 hakuna timu iliyoona lango la mwenzake. Hapo Kahn akaanza kejeli "zimebaki dk 30 tu unipe Mali zangu" Ronaldo akajibu "Mpira unaingia wavuni kwa sekunde moja tu, nna sekunde zaidi ya 1800"

Ikawa dakika ya 67, Ronaldo akafunga bao kali. Oliver Kahn alipiga kelele kwa mabeki zake kumuachia nafasi mshambuliaji k**a Ronaldo kupiga anavyotaka. Haikutosha dakika ya 79 Ronaldo anaingia tena kambani baada ya Rivaldo kuuacha mpira umpite tobo ndani ya 18 akijua wazi utamfkia Ronaldo ambae nae bila kujiuliza aliutungua kisawasawa ukazama wavuni, ubao ukasomeka 0-2. Oliver Kahn alilala baada ya bao la pili alilia sana. Baada ya mechi kuisha alisema:

"Dunia ina wachezaji lakini Ronaldo ni Dunia nyingine". Watu wengi waliipa ushindi German kutokana na ubora wa Oliver Kahn ambae alipewa jina na kuitwa kipa wa Dunia haikua easy kumfunga. Lakini alisarenda kwa Ronaldo De Lima.

Kuna magolikipa wengine wengi tu huwa wanakataa kufungwa na flani. Gigi Buffon robo fainali ya Uefa 2017 kati ya Juventus na Monaco alisema anaheshimu uwepo wa kinda Kylian Mbappe lakini kumfunga hawezi. Dakika ya 69 Mbappe anamfunga Buffon na Buffon anaenda kumbusu Mbappe kichwani kukubali japo Monaco walitolewa kwa agg ya 4-1.

Follow: Soka Viwanjani 💥

28/09/2022

Messi akiwa Argentina mwaka huu:

vs. Venezuela ⚽️
vs. Ecuador ❌
vs. Italy ❌
vs. Estonia ⚽️⚽️⚽️⚽️⚽️
vs. Honduras ⚽️⚽️
vs. Jamaica ⚽️⚽️

Mechi 6 mabao 10

💥

28/09/2022

Kocha wa Argentina, Lionel Scaloni ameongezewa mkataba mpya na Shirikisho la Soka Argentina mpaka June 2026.

"Najivunia kutangaza kuwa tumefikia makubaliano na Scaloni mpaka Kombe la Dunia la 2026" Rais wa AFA, Tapia

Scaloni kaiongoza Argentina tangu 2019 kwa michezo 35 bila kupoteza.

💥

Photos from Soka Viwanjani's post 28/09/2022

Wakati mechi kati ya Brazil na Tunisia ikiendelea hapo Jana, baadhi ya mashabiki walitupa ndizi uwanjani kumwelekea Richarlson:

"Hawa watu wanapaswa kuadhibiwa sio tu kuleta bla bla" Richarlson

Brazil waliibuka na ushindi wa bao 5-1 .

💥

27/09/2022

Mnamo Septemba 2016, Roma ilifungwa 2-1 dhidi ya Sampdoria na mechi ilisimamishwa kwa saa moja kutokana na mvua kubwa. Wachezaji wote, makocha na mabenchi ya ufundi wa timu zote mbili wakakimbilia vyumbani kujilinda na mvua isipokuwa Totti ambaye aliendelea kupasha pembeni ya uwanja.

Mchezo ulirudi nyuma na Totti akarudi. Kisha akatoa pasi ya uhakika kwenye bao la kusawazisha la Roma (2-2) kabla ya dakika ya mwisho kufunga bao la ushindi la Roma ambalo walishinda 3-2 👏

Francesco Totti, kiitaliano wanaita "Franshesco" Totti leo anatimiza miaka 47.

💥

27/09/2022

Leandro Paredes juu ya uhusiano wake na Kylian Mbappé:

"Mimi sio mtu wa kuzungumza juu yake. Nilikuwa na uhusiano na wale ambao nilikuwa na uhusiano nao. Lakini wale ambao sikuwa na uhusiano nao, siwezi kukuambia juu yao ". Paredes

Fabrizio Romano

💥

27/09/2022

Mshambuliaji wa Liverpool, Roberto Firmino anakaribia kuachana na Liverpool, Barcelona wakihusishwa kumsajili, Fc Porto na Juventus.

Source: Mirror

💥

26/09/2022

Beki wa Barcelona Ronald Araújo ameamua kufanyiwa upasuaji wa paja lake la mguu wa kulia na atakuwa nje kwa muda wa miezi 2-3, akikosa Kombe la Dunia.

💥

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Zambezi
Dar Es Salaam