14/05/2022
Mtendaji wetu Mkuu Twaha Ngwambi alipokuwa akitoa neno la Ukaribisho kwa wageni waalikwa kwenye Uzinduzi wa Mashindano Makubwa ya Kimataifa ya Cambiasso & Rainbow U20 International Tournament yaliyofanyika Dar Es Salaam Serena Hotel.
🇹🇿🇰🇪🇺🇬🇧🇮🇷🇼🇿🇲🇸🇳🇨🇵
sports
14/05/2022
Rais Wa Shirikisho la Mpira wa miguu Zanzibar Abdul-Latif Ally Yasin alipata nafasi ya kuzungumza kwenye Uzinduzi wa Mashindano Makubwa ya Kimataifa ya Cambiasso & Rainbow U20 International Tournament yaliyofanyika Dar Es Salaam Serena Hotel.
🇹🇿🇰🇪🇺🇬🇧🇮🇷🇼🇿🇲🇸🇳🇨🇵
sports
14/05/2022
Kaimu Katibu Mtendaji Baraza la Michezo Taifa (BMT) Neema Msitha alikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa na kupata fursa ya kutoa nasaha kwenye Uzinduzi wa Mashindano Makubwa ya Kimataifa ya Cambiasso & Rainbow U20 International Tournament yaliyofanyika Dar Es Salaam Serena Hotel.
🇹🇿🇰🇪🇺🇬🇧🇮🇷🇼🇿🇲🇸🇳🇨🇵
sports
13/05/2022
💬 Nitoe Shukran za pekee sana kwa Cambiasso hiki wanachokifanya ni kikubwa sana. Sote hapa tunajua hakuna Shortcut kwenye Mpira, Hakuna Shortcut kwenye michezo💬
Aliyasema hayo Aliyekuwa Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Mashindano Ya Kimataifa kwa Vijana Walio chini ya Miaka 20 ya CAMBIASSO & RAINBOW U20 INTERNATIONAL TOURNAMENT ambae ni Mkurugenzi Wa Maendeleo Ya Michezo Nchini Bw. Yusuph Singo.
🇹🇿🇰🇪🇺🇬🇧🇮🇷🇼🇿🇲🇸🇳🇨🇵🏆
sports
13/05/2022
Officially Launched 🎉
Rasmi Mashindano Ya Kimataifa Kwa Vijana Chini Ya Miaka 20, Cambiasso & Rainbow U20 International Tournament yamezinduliwa Jijini Dar Es Salaam.
🎉🏆
sports
10/05/2022
Katika Jitihada za Kuzidi kutoa Fursa na kulikuza Soka La Vijana nchini, CambiassoSports tukishirikiana na RainbowSports Tunakuletea Mashindano Ya Kimataifa kwa Vijana walio chini ya Miaka 20 ya 𝘾𝘼𝙈𝘽𝙄𝘼𝙎𝙎𝙊 & 𝙍𝘼𝙄𝙉𝘽𝙊𝙒 𝙐20 𝙄𝙉𝙏 𝙏𝙊𝙐𝙍𝙉𝘼𝙈𝙀𝙉𝙏'.
Mashindano hayo yatakayojumuisha timu 12 kutoka mataifa Mbalimbali Barani AFRICA na ULAYA yanatarajiwa kutimua Vumbi hapa nchini Mnamo mwezi Julai Mwaka huu.
sports
🇹🇿⚽️
19/02/2022
💪⚽️
Vijana wakiweka Miili tayari kwa Kazi.!
🔋⚡
🇹🇿⚽️
27/01/2022
Cambiasso Sports Management inaungana na Wadau wa Soka nchini pamoja na watanzania wote kwa ujumla katika kumtakia Kheri Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan katika kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake.
M/Mungu amzidishie Ujasiri na Busara zaidi katika kulijenga Taifa Letu. 🇹🇿
22/12/2021
MAXIME AIBUA KIPAJI KIPYA ARUSHA 💫
Tukiwa kwenye mashindano ya CHIPKIZI CUP jijini Arusha, Kocha Mecky Maxime amevutiwa na KIPAJI cha hali ya juu kilichooneshwa na BEKI wa KUSHOTO kutoka timu ya FUTURE STARs U17 ya jijini Arusha.
Mwalimu Maxime alionesha nia ya kumuhitaji mtoto huyo mwenye uwezo mkubwa sana kwenye kuimudu nafasi hiyo, Hivyo basi muda si mrefu kutoka sasa KINDA huyo fundi ataungana na timu yetu ya Vijana U17.
KARIBU SANA FULL BACK YA MPIRA⚽🔥