K**a refa hakuona hili tukio la Penalty ya wazi basi tuseme it's oky ila bodi ya ligi na zile adhabu zake basi wadau wa soka wanawaangalia kwa makini
Ikumbukwe Mudathir anatumikia ban ya mechi tatu kwenye tukio k**a hili sema lina utofauti kidogo hasa kwenye dhamira.
Hii itakuwa ni ban ya mechi tano au tatu?
Michezo Online Library 24
FOLLOW UKURASA HUU KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI BILA UBAGUZI WOWOTE ULE ⚽
20/04/2026
KUWENI MAKINI NA HAWA WACHAMBUZI
Hawa siyo wachambuzi tu pia ni mashabiki wa Simba sc,
Binafsi bila kuwa upande wowote najiuliza hivi pale Tff si kuna room ya kufichua tuhuma za upangaji matokeo? Sasa kwanini wasiende kwenye vyombo husika kabla yakuchukua sheria mdomoni?
Kila taasisi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na kanuni hata mahak**ani kuna sheria na ushahidi ili kuepuka kukisia na kuvunjiana heshima hivi vyombo vipo vitumieni kabla yakuimba midomoni k**a vijiwe vya umbea ili watuhumiwa wakipatikana na hatia sisi tupate vya kuandika ila kwa sasa tukiandika na kutuhumu moja kwa moja naomba mashabiki mtupime akili
Imefika hatua sasa nafikiri pengine Yanga sc wakishinda wanaumia au pengine wanabetia ya Yanga sc mfungwe
Mechi za mwisho kwa mbeya City ni hizi ambapo hiyo ya sita bila ndiyo imewauma waungwa sana ,sasa najiuliza mbeya city ni mbovu au singida,Simba sc nao walinunua mechi
Singida black star 5-1 Mbeya City
Simba sc. 3-0 Mbeya City
Yanga sc. 6-0 Mbeya City
TFF WANASEMA K**A KUNA VIASHIRIA VYA RUSHWA AU DALILI ZENYE USHAHIDI PELEKA OFISINI KWAAJILI YA HATUA ZAIDI.
YANGA SC 6-0 MBEYA CITY
HAYA HAPA MABAO YOTE SITA
YANGA SC 6-0 MBEYA CITY
kuna mdau anasema Yanga sc walipania sana ,kosa la kwanza la mbeya city nikutaka kujifananisha na Yanga sc ,kosa namba mbili ni kutoa draw mechi ya kwanza na kosa la tatu ni Kamdomo.
Wahuni wakafunga booster.
16/04/2026
STYLE YA UCHEZAJI
Ukifuatilia Post yangu ya mwisho nilisema kiuchezaji Young Africans Sports Club wamebadilika kiuchezaji baada ya ujio wa Amoarim assistant coach mpya
Hawa Mbeya City waliopokea robo tatu wiki ndio hawa hawa waliotoa sare pale mbeya hata wangeongeza dakika 10 kulikuwa hakuna namna ya Yanga kupata bao ile siku lakini leo hata ingeongezwa sekunde ingezaa bao
YANGA WANACHEZA MPIRA WAO SASA
Kutokana na presha kubwa na kasi ya mchezo, Mbeya City walibanwa kucheza ndani ya nusu yao, wakashindwa kujenga mashambulizi yenye tija. Walilazimika kupiga mipira mirefu isiyo na mwelekeo, hali iliyowapa Yanga urahisi wa kurejesha umiliki na kuanzisha mashambulizi mapya
Yanga waliingia uwanjani wakiwa na mpango madhubuti wa kiufundi uliolenga kuudhibiti mchezo mapema kabisa.
Wakitumia mbinu ya high pressing kwa ufanisi mkubwa k**a zamani chini ya Miguel Gamondi na Ramovic Walikuwa wanapandisha presha kuanzia juu kabisa ya uwanja, wakilazimisha wachezaji wa Mbeya City kufanya maamuzi ya haraka chini ya shinikizo kubwa hakuna back pass, Israel mwenda na Mudathuri wamebadilika
Hii ilisababisha makosa mengi ya upotevu wa mipira, hasa katika eneo la ulinzi na kiungo cha chini cha Mbeya City
Baada ya kufanya mabadiliko ya wachezaji, Mbeya City walionekana kuongeza uhai wa mchezo, wakipata nguvu mpya hasa kwenye kasi na mzunguko wa pasi.
Hii iliwapa uwezo wa kusogea mbele kwa ujasiri zaidi na kupunguza presha waliyokuwa wanakabiliana nayo awali
Mbeya City waliingia uwanjani bila tahadhari ya kutosha dhidi ya Yanga, wakionekana wamerelax kupita kiasi. Hali hiyo ilifanya mchezo kuwa wazi zaidi, jambo lililoipa Yanga nafasi kubwa ya kutawala na kuumiliki mchezo kirahisi(wamestahili hiki kipigo)
Mudathili alikuwa k**a rada tu uwanjani ikiichezesha timu atakavyo kiungo wa mpira
Kilichovutia zaidi ni goli la tano la Zimbwe Jr, akimalizia kwa utulivu diagonal pass yenye ubora kutoka kwa Allan Okello—ufanisi mkubwa kwenye final third
Pillar Kelvin ni mali sana akiwa na mpira amekuwa na mchezo mzuri leo
Pacome Zouzoua 🔥 🔥 🔥 hakuwahi kuwa na show mbovu "Fantastic player" Allan Okello anajua kucheza anajua kupasi na kuasist pia 🔥 what a man, all in all six bila bao fresh tu
12/04/2026
Chukua Akaminko watu wamsahau Khalid Aucho
Conte
Andabwile
Damaro
Aucho
Hao wote hawamfikii James Akaminko, mmechelewa sana wananchi kumvuta huyu kulikuwa hakuna haja yoyote yakuangaika.
09/04/2026
KAZI KAZINI
Mnyama ameshindwa kupata ushindi kwa mara ya kwanza dhidi ya Wakusanya Kodi, TRA United kufuatia sare tasa katika dimba la Sheikh Amri Kaluta Abeid, Arusha kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara.
Simba SC inasalia nafasi ya pili alama 8 nyuma ya vinara, Yanga SC wakifikisha alama 36 baada ya mechi 17 wakiwa wamecheza mechi moja pungufu ya Wananchi.
Kwingineko Waoka Mitake, Azam FC wamelazimishwa sare tasa dhidi ya Mbeya City katika dimba la Tanzanite Kwaraa, Babati Manyara.
Ubingwa upo kweli?
FT: TRA United 0-0 Simba SC
🟥 87' Nouma
FT: Mbeya City 0-0 Azam FC
08/04/2026
MBONA K**A KUNA KITU KIMEONGEZEKA
Zile back pass sijaziona halafu muda nimemuona kwenye box sio mara moja ndio maana kafunga kamba mbili
Damaro mbele
Pacome mbele
Abuya mbele
Mudathir mbele
Okelo mbele
Wote hawa ni viungo na hapa ndipo pamewaadhibu Pamba jiji
Kadri muda unavyozidi kusogea na siku zinavyozidi kwenda ndivyo ambavyo Allan Okello nae anazidi kuzoea mazingira ya ligi kuu na anaongezewa files kutoka kwa msaidizi Kocha
Leo katoa assist 3 halafu jumla ni Goli 1 na assist 4 kwenye mechi zake 2 za mwisho ni alama tosha inayoonesha kuwa kuna kitu kimeongezwa kiufundi
Alianza kwa speed ndogo sana kwenye mechi za mwanzoni, lakini hivi sasa tiyari stats zake zimeanza kuongea kwa sauti kuu mnooo.
Top talent.🇺🇬🔥
28/03/2026
KARIAKOO KARIAKOO ARE YOU READDDD.....
Mwamba huyu hapa ,dogo huyu hapa namba tisa wa kisasa kabisa mjini na mimi nikiweka mchezaji nimeweka kifaa kweli kweli atakae mpata huyu amelamba dume
Thabang Mahlangu ameweka hat-trick kwa ORBIT College katika mechi ya DDC dhidi ya AmaZulu leo.
Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Afrika Kusini chini ya umri wa miaka 20 kwa sasa yupo kwa mkopo ORBIT College akitokea Siwelele na mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu 😊
ANAJUA NYOTA HII IMEPITA WAPI?
Thabang Mahlangu amepitia kwenye timu kadhaa, ikiwa ni pamoja na:
- *SuperSport United*: Alicheza katika timu akiba ya SuperSport United na kushinda ligi ya PSL Reserve League msimu wa 2022-2023.
- *Siwelele FC*: Alijiunga na Siwelele FC baada ya SuperSport United kuuzwa, na mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu.
- *Orbit College*: Kwa sasa yupo kwa makubaliano maalumu au tuseme mkataba ORBIT College, akitokea Siwelele FC
Pia amewahi kuchezea timu za taifa za Afrika Kusini chini ya umri wa miaka 17 na 20
UNATAKA KUJUA MAFANIKIO YAKE KWA SASA?
23/03/2026
TAARIFA
MREJESHO WA KIKAO YANGA SC MANAGEMENT NA BENCHI LA UFUNDI.
MOALIN NDANI
LINATAFUTWA SOKA LA 👋
19/03/2026
NGOJENI LEO NIWATONYE YALIYOTOKEA BAADA YA AFCON
Iko hivi baada ya Senegal kubeba kombe na zile figisu zote zilizotokea ndani ya uwanja na nje ya uwanja wapo raia wengi sana wa Senegal walioshikiliwa mpaka leo hii na hili ndilo limepelekea kurudisha kombe
Watu wameshikwa kwa kesi za vurugu nje ya uwanja halafu Morocco wao wimbo wao kila siku ni kujitoa kwenye haya mashindano na ndiyo wimbo wao kila siku kuwa wao Africa ni bahati mbaya then wakabaki na watu wenu halafu kuwapiga hamuwezi na watu wenu bado wameshikiliwa jela huko sasa wewe unafikiri k**a Raisi wa nchi utang'ang'ania kombe?
Kukosa lile kombe Morocco wameumia sana na wapo tayari kufanya lolote ,wamegharamia sana sana yale mashindano na mbaya zaidi walijiaminisha hakuna wakuwafunga so wakajimaliza
Kwahiyo mnayoyaona ndugu zangu ni shinikizo na nimakubaliano maalumu kati ya serikali ya Morocco na Senegal
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam