Data Sports Tv

Data Sports Tv

Share

Habari za Michezo| Uchambuzi wa Mechi.

Datasports TV Tunakuletea Uchambuzi wa kina baada ya mechi, Taarifa Sahihi na Exclusive Interviews na wadau nguli wa Michezo.

06/06/2026

Nyota wa klabu ya Yanga raia wa Uganda Allan Okello ameeleza kuwa kabla ya kujiunga na Yanga aliwasiliana na Khalid Aucho kisha akafanya maamuzi ya kutua Jangwani.

"Kwanza ilinibidi niongee na Aucho (Khalid), tukajadiliana na baada ya hapo nikaongea na rais wa klabu yangu ya zamani, ili aweze kuniruhusu, hakuwa tayari kuniachia kuondoka wakati wa Januari, ilihitajika nifanye kazi ya ziada kumshawishi kukubali baadaye alikubali."

-Allan Okello, Mchezaji wa klabu ya Yanga.

✍️

05/06/2026

Tujikumbushe kidogo maisha ya Gael Bigirimana ndani ya Yanga.

-Julai 2022: Alijiunga na klabu ya Ysnga k**a Mchezaji huru akitokea Glentoran ya Ireland Kaskazini.

-Agosti 2023: Yanga ilifungiwa na FIFA kutokana na Bigirimana kudai Stahiki zake (Ada ya usajili) na kufanikiwa kushinda kesi hiyo.

-Disemba 2023: Yanga walifanikiwa kumlipa Bigirimana.

Kwa sasa Gael Bigirimana anaitumikia klabu ya Dungannon Swifts inayoshiriki Ligi kuu ya Ireland Kaskazini (NIFL Premiership).

NB: Ukiwa k**a Shabiki/Mdau wa Soka Unamkumbuka Gael Bigirimana chuma kilichowahi kucheza Ligi Kuu Soka nchini Uingereza (EPL) akiwa Newcastle United kuanzia 2012 hadi 2016?.

✍️

05/06/2026

Sababu Inayomfanya Diarra Duke Abuya Kuwa wachezaji Bora ndani ya Yanga hadi Sasa....

05/06/2026

Mchambuzi wa soka Hans Rafael ameweka wazi kuwa kwa sasa Simba ndio timu bora zaidi uwanjani kuliko Yanga.

"Na ukiuliza timu gani inaonekana bora zaidi uwanjani kwa sasa, nitakwambia Simba. Kuna mashabiki wa Yanga wanaotambua kuwa msimu huu umekuwa mgumu kidogo tofauti na ilivyokuwa awali,"

-Hans Rafael, Mchambuzi wa Soka

✍️

05/06/2026

Hatimaye Kocha Anthony Da Silva raia wa Ureno ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Mali.

Mreno huyo amewahi kufanya kazi kwenye benchi la Ufundi la timu ya taifa ya Cameroon k**a Mchambuzi wa Video "Video Analyst" akiwa chini ya Kocha Toni Canceição.

Hivyo Kocha Pedro amechukua rasmi jukumu la kukinoa kikosi cha "The Eagles" ambacho kinaundwa na nyota mbalimbali wakiwemo Aliou Dieng, Djigui Diarra,Yves Bissouma,Amadou Haidara
Mohamed Camara na wengineo wengi.

NB: Diarra kunolewa na kocha mpya...

✍️

05/06/2026

Rais wa klabu ya Yanga Eng.Hersi Said ameweka wazi kuwa msimu uliopita ulikuwa mgumu zaidi kuliko msimu uliopita ambao walihitaji kushinda mechi ya mwisho tena dhidi ya Simba ili wawe Mabingwa.

"Nadhani msimu uliopita ndio ulikuwa msimu mgumu sana kwetu maana tulihitaji hadi mechi yetu ya mwisho tushinde tena Dabi na Simba SC ndio tuwe Mabingwa, sioni k**a ubingwa wa msimu huu ni mgumu k**a ilivyokuwa msimu uliopita"

-Eng.Hersi Said, Rais wa klabu ya Yanga.

✍️

05/06/2026

WANAPENDWA NA MASHABIKI

Kuna baadhi ya wachezaji huwa wanapata bahati ya kupendwa na mashabiki wa kila timu kutokana na mtindo wao wa maisha ndani na nje ya uwanja na miongoni mwao ni Ngolo Kante,Ricardo Kaka, Luka Modric na wengineo.

Lakini kwa hapa nchini Tanzania pia wapo baadhi ya nyota haswa wanaotumikia vilabu vya Simba na Yanga ambao wamewahi kupendwa/wanapendwa na mashabiki wa vilabu vyote viwili licha ya utani wao wa jadi na miongoni mwao ni Maxi Nzengeli (Yanga) pamoja na Shomari Kapombe (Simba) bila kumsahau "FAILASUFI" Feisal Salum "Fei Toto" kutoka (Azam FC), John Bocco, Mrisho Ngassa Nk.

Haimaanishi wachezaji wengine hawapendwi au Wanachukiwa HAPANA maana mpira ni Umoja,Upendo, Mshik**ano na Amani bali ni kuonyesha upekee wa mchezaji fulani jinsi anavyokubalika kwa mashabiki wengi pasipo kujali timu anayoitumikia.

NB: Ongeza wachezaji wengine wanaopendwa zaidi na mashabiki wa timu zote mbili za Simba na Yanga...

Unasubiri Nini? Link on Bio kwa Taarifa zaidi na Mikeka ya Bure.

✍️

05/06/2026

Kwa mahitaji ya bati Bora za nyumba yako waone

Hawa ni Wazalishaji na wasambazaji wa bati za aina zote kwa Bei ya kiwandani.
✔ Bati za Migongo midogo
✔ Bati za Migongo mikubwa
✔ Bati zenye mfano wa kigae
✔ Bati zenye material ya chenga chenga

Kuanzia 30G Hadi 28G

💯 Quality ya uhakika na Warranty

Ukinunua Bati unapata MISUMARI NA USAFIRI BURE

📲 Wasiliana nao sasa kuweka order yako!
0760 684 594

04/06/2026

NB: Alikuja Tanzania, akajenga ufalme wake na kuimbwa kwa ukubwa mno.Ni miongoni mwa viungo bora kuwahi kucheza ndani ya Ligi kuu ya NBC...

Huyu ni nani?

✍️

04/06/2026

Unatafuta Pool table bora na vifaa vyake?

Basi Wasiliana na

KUFIKA KWA URAHISI KWENYE OFISI ZETU ZILIZOPO MABIBO HOSTEL.

Ukiwa unatokea buguruni Unatakiwa kushuka kituo cha Mabibo Hostel.

🚫 Usiulize 📞 Piga simu namba: 0715 528 432 / 0767 528 432.
🏃‍♂️ Subiri sekunde chache, timu yetu itakufuata hapo hapo kituoni kukupokea na kukuleta ndani ya ofisi yetu ya Tanice Pool table.

NB:Hakikisha unapata bidhaa kutoka Tanice Pool table sio sehemu nyingine ili ufurahie bidhaa Bora na za kisasa zaidi.

Quality • Bei nzuri • Huduma ya uhakika

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Address


Mabibo External
Dar Es Salaam
NON