06/06/2026
Nyota wa klabu ya Yanga raia wa Uganda Allan Okello ameeleza kuwa kabla ya kujiunga na Yanga aliwasiliana na Khalid Aucho kisha akafanya maamuzi ya kutua Jangwani.
"Kwanza ilinibidi niongee na Aucho (Khalid), tukajadiliana na baada ya hapo nikaongea na rais wa klabu yangu ya zamani, ili aweze kuniruhusu, hakuwa tayari kuniachia kuondoka wakati wa Januari, ilihitajika nifanye kazi ya ziada kumshawishi kukubali baadaye alikubali."
-Allan Okello, Mchezaji wa klabu ya Yanga.
✍️
05/06/2026
Tujikumbushe kidogo maisha ya Gael Bigirimana ndani ya Yanga.
-Julai 2022: Alijiunga na klabu ya Ysnga k**a Mchezaji huru akitokea Glentoran ya Ireland Kaskazini.
-Agosti 2023: Yanga ilifungiwa na FIFA kutokana na Bigirimana kudai Stahiki zake (Ada ya usajili) na kufanikiwa kushinda kesi hiyo.
-Disemba 2023: Yanga walifanikiwa kumlipa Bigirimana.
Kwa sasa Gael Bigirimana anaitumikia klabu ya Dungannon Swifts inayoshiriki Ligi kuu ya Ireland Kaskazini (NIFL Premiership).
NB: Ukiwa k**a Shabiki/Mdau wa Soka Unamkumbuka Gael Bigirimana chuma kilichowahi kucheza Ligi Kuu Soka nchini Uingereza (EPL) akiwa Newcastle United kuanzia 2012 hadi 2016?.
✍️
05/06/2026
Mchambuzi wa soka Hans Rafael ameweka wazi kuwa kwa sasa Simba ndio timu bora zaidi uwanjani kuliko Yanga.
"Na ukiuliza timu gani inaonekana bora zaidi uwanjani kwa sasa, nitakwambia Simba. Kuna mashabiki wa Yanga wanaotambua kuwa msimu huu umekuwa mgumu kidogo tofauti na ilivyokuwa awali,"
-Hans Rafael, Mchambuzi wa Soka
✍️
05/06/2026
Hatimaye Kocha Anthony Da Silva raia wa Ureno ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Mali.
Mreno huyo amewahi kufanya kazi kwenye benchi la Ufundi la timu ya taifa ya Cameroon k**a Mchambuzi wa Video "Video Analyst" akiwa chini ya Kocha Toni Canceição.
Hivyo Kocha Pedro amechukua rasmi jukumu la kukinoa kikosi cha "The Eagles" ambacho kinaundwa na nyota mbalimbali wakiwemo Aliou Dieng, Djigui Diarra,Yves Bissouma,Amadou Haidara
Mohamed Camara na wengineo wengi.
NB: Diarra kunolewa na kocha mpya...
✍️
05/06/2026
Rais wa klabu ya Yanga Eng.Hersi Said ameweka wazi kuwa msimu uliopita ulikuwa mgumu zaidi kuliko msimu uliopita ambao walihitaji kushinda mechi ya mwisho tena dhidi ya Simba ili wawe Mabingwa.
"Nadhani msimu uliopita ndio ulikuwa msimu mgumu sana kwetu maana tulihitaji hadi mechi yetu ya mwisho tushinde tena Dabi na Simba SC ndio tuwe Mabingwa, sioni k**a ubingwa wa msimu huu ni mgumu k**a ilivyokuwa msimu uliopita"
-Eng.Hersi Said, Rais wa klabu ya Yanga.
✍️
05/06/2026
WANAPENDWA NA MASHABIKI
Kuna baadhi ya wachezaji huwa wanapata bahati ya kupendwa na mashabiki wa kila timu kutokana na mtindo wao wa maisha ndani na nje ya uwanja na miongoni mwao ni Ngolo Kante,Ricardo Kaka, Luka Modric na wengineo.
Lakini kwa hapa nchini Tanzania pia wapo baadhi ya nyota haswa wanaotumikia vilabu vya Simba na Yanga ambao wamewahi kupendwa/wanapendwa na mashabiki wa vilabu vyote viwili licha ya utani wao wa jadi na miongoni mwao ni Maxi Nzengeli (Yanga) pamoja na Shomari Kapombe (Simba) bila kumsahau "FAILASUFI" Feisal Salum "Fei Toto" kutoka (Azam FC), John Bocco, Mrisho Ngassa Nk.
Haimaanishi wachezaji wengine hawapendwi au Wanachukiwa HAPANA maana mpira ni Umoja,Upendo, Mshik**ano na Amani bali ni kuonyesha upekee wa mchezaji fulani jinsi anavyokubalika kwa mashabiki wengi pasipo kujali timu anayoitumikia.
NB: Ongeza wachezaji wengine wanaopendwa zaidi na mashabiki wa timu zote mbili za Simba na Yanga...
Unasubiri Nini? Link on Bio kwa Taarifa zaidi na Mikeka ya Bure.
✍️
04/06/2026
NB: Alikuja Tanzania, akajenga ufalme wake na kuimbwa kwa ukubwa mno.Ni miongoni mwa viungo bora kuwahi kucheza ndani ya Ligi kuu ya NBC...
Huyu ni nani?
✍️