19/12/2025
klabu ya simba sc imemtangaza rasmi Steve Barker kuwa kocha wao mkuu atakaekiongoza kikosi icho cha msimbazi
Michezo
19/12/2025
klabu ya simba sc imemtangaza rasmi Steve Barker kuwa kocha wao mkuu atakaekiongoza kikosi icho cha msimbazi
18/12/2025
Bodi ya Wakurugenzi ya klabu ya Simba Sc imekutana leo Alhamisi Desemba 18, 2025 kwa ajili ya kikao cha kujadili mambo mbalimbali kuhusu klabu hiyo kikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Crescentius Magori.
Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), Zubeda Hassan Sakuru na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Murtaza Mangungu ni miongoni mwa waliohudhurua kikao sambamba na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi akiwemo Barbara Gonzalez.
14/11/2025
Tanzania Women’s Premier League 2025/2026
FT Simba Queens 4️⃣ -0️⃣ Bilo FC
⚽️ Aisha Juma
⚽️ ⚽️ ⚽️ Jentrix Shikangwa
14/11/2025
Tanzania Women’s Premier League 2025/2026
FT Ruangwa Queens 0️⃣-3️⃣ Yanga Princess
⚽️ Precious Onyinyech
⚽️ Aregash Tadese
⚽️ Precious Onyinyech
14/11/2025
Klabu ya Azam Fc imemtangaza Octavi Anoro k**a Mtendaji Mkuu (CEO) mpya klabuni, kwa mkataba wa miaka miwili utakaombakisha hadi 2027 akichukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa Abdulkarim Nurdin maarufu k**a Popat ambaye amepandishwa cheo na kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais.
Kwa mujibu wa taarifa ya leo Novemba 14, 2025 iliyotolewa na klabu hiyo Anoro (42) raia wa Hispania, anakuja na maarifa na uzoefu mkubwa wa kimataifa katika nyanja ya maendeleo ya utawala na biashara ya mpira wa miguu.
Aidha, Bodi pia imemteua, Rashid Seif Mohamed, kuwa msaidizi wa Mtendaji Mkuu (Assistant CEO). Rashid ni mhitimu wa Shahada ya Umahiri ya utawala wa michezo (Master’s in Sports Management) pamoja na ngazi ya pili ya ukocha kutoka chama cha soka cha England, FA.
14/11/2025
Kocha wa zamani wa Mamelodi Sundowns na Al Ahly ya Misri, Dr. Pitso Mosimane anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa Yanga Soccer School utakaofanyika kesho Novemba 15, 2025 katika kituo maalumu cha kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana cha Speedsports Muhimbili Center.
Mosimane ambaye ni mshindi mara tatu wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) k**a kocha ni mmoja wa wataalam wanaoheshimika katika maendeleo ya soka, uwepo wake unatarajiwa kutoa hamasa kwa vijana na wataalamu wa mchezo huo, sambamba na kuonyesha dhamira ya Yanga katika kuwekeza kwenye akademi ya kisasa yenye viwango vya kimataifa.
Mpango huo ambao unalenga vijana chini ya umri wa miaka 11, 13 na chini ya miaka 15 waliopo jijini Dar es Salaam wenye lengo la kuibua na kuendeleza vipaji vya vijana kwa klabu na taifa, unatajwa kuwa hatua muhimu katika kuhakikisha Tanzania inaendelea kutoa wachezaji bora na kuimarisha misingi ya soka la vijana.
26/10/2025
.. msimamo wa ligi kuu ya uingereza EPL
26/10/2025
La Liga
Full time:Real Madrid 2️⃣ vs FC Barcelona 1️⃣
26/10/2025
EPL full time
20/09/2025
TRA UNITED KUBAKI TABIRA: Serikali imewathibitishia mashabiki wa soka mkoani Tabora kwamba timu ya TRA United SC (Tabora United) haitohama katika mkoa huo k**a tetesi zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, SPA Paul John Walalasi amethibitisha hilo mbele ya k**ati ya usimamizi wa ushindi wa TRA United, katika kikao kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Tabora.
Amesema TRA imeinunua timu hiyo kutoka kwa wamiliki ikiwa ni sehemu ya kutekeleza malengo iliyokuwa imejiwekea kwamba msimu huu mpya wa ligi 2025/26 TRA iwe na timu ya NBC Premier League.
SPA Walalasi ametamba timu hiyo ya TRA United italeta ushindani mkubwa kwenye ligi msimu huu.
Katibu Tawala mkoa wa Tabora Dkt. John Mboya amesema timu hiyo itaendeshwa kwa ufanisi mkubwa kwa kuwa ipo chini ya Taasisi ya serikali, hivyo mashabiki wanapaswa kuipa ushirikiano ili ipate ushindi.
20/09/2025
Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) na kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) inaendelea tena leo Septemba 20, 2025 kwa mechi mbalimbali huku wawakilishi wa Tanzania kwenye CAFCL, Simba Sc na CAFCC, Azam FC na Singida Black Stars wakitupa karata yao kwenye hatua ya awali ya michuano hiyo.
20:00 Gaborone Utd 🇧🇼 vs 🇹🇿 Simba Sc
🏟️ Obert Itani Chilume, Francistown
19:00 Rayon Sport 🇷🇼 vs 🇹🇿 Singida Black Stars
🇷🇼 Kigali Pelé, Nyamirambo
16:00 EL Merriekh Bentiu 🇸🇸 vs 🇹🇿 Azam Fc
🏟️ Juba National Stadium
#
18/09/2025
Klabu ya Benfica ya Ureno imefikia makubaliano ya kumteua mkufunzi José Mourinho kuwa kocha mkuu klabuni hapo kuchukua mikoba ya Bruno Lage aliyetupiwa virago kufuatia kipigo cha 3-2 dhidi ya Qarabag kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya siku ya Jumanne.
Meneja huyo wa zamani wa FC Porto, Chelsea, Real Madrid, Inter Milan, Manchester United na Tottenham Hotspur amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili utakaombakisha klabuni hapo mpaka Juni 2027. na wiki ijayo atakuwa Stamford bridge kucheza na Chelsea FC katika mashindano ya UEFA champions league.