13/05/2026
“Florian Wirtz atarejea kikosini, na ninaamini ataanza katika mchezo huo. Nimeelezwa kuwa tatizo la tumbo lililomfanya akose mchezo wa mwisho dhidi ya Chelsea sasa limepona, na tayari amerejea mazoezini,”
James Pearce akizungumza kwenye kipindi cha Walk On Podcast.
12/05/2026
💥HABARI MPYA .. Kwa mujibu wa Tuttosport ya Italia, Alisson Becker tayari ameonyesha nia yake ya kujiunga na Juventus pekee, akiamini kuwa huu unaweza kuwa usajili wake wa mwisho mkubwa katika soka la kiwango cha juu.
Hata hivyo, Liverpool bado hawajaridhika na kiasi cha fedha kinachotolewa. Inaelezwa kuwa klabu hiyo haitaki kumuuza kwa chini ya euro milioni 15 hadi 20, licha ya umri wake na historia ya majeraha.
10/05/2026
Kwa mujibu wa Le10Sport, bado hajafanya maamuzi kuhusu mustakabali wake ndani ya .
Mchezaji huyo anavutiwa na wazo la kucheza England, hasa kujiunga na . Barcola anataka kupata nafasi kubwa zaidi ya kucheza, kwani kwa sasa si chaguo la kwanza chini ya kocha .
✍️Ripoti hiyo inaeleza kuwa Liverpool wanaweza kurejea tena kwa dau jipya majira haya ya kiangazi, na safari hii dili linaweza kufanikiwa.
10/05/2026
Kwa mujibu wa gazeti la L'Équipe, klabu ya Liverpool FC inaendelea kufuatilia kwa karibu hali ya kiungo wa AS Monaco, Lamine Camara (22).
Wakati huo huo, Newcastle United FC ambao wamekuwa wakimvutiwa kwa muda mrefu, bado wapo kwenye mbio za kuwania saini ya nyota huyo wa kimataifa wa Senegal dirisha hili la majira ya kiangazi.
09/05/2026
Arne Slot kuhusu kumtoa Rio Ngumoha:
“Sidhani k**a ilikuwa baadhi tu ya mashabiki — kulikuwa na wengi ambao hawakukubaliana na mabadiliko hayo, jambo ambalo linaeleweka kabisa.
Alikuwa na matatizo ya misuli, na nilipomuuliza aliniambia hakuwa na uhakika k**a angeweza kuendelea kucheza. Nilijua kabisa kuwa kutakuwa na hisia k**a hizo kwa sababu yeye ni mchezaji mzuri sana.
Mara nyingi kwenye soka, watu hawajui kila kitu. Mimi ndiye kocha, na ni lazima nifanye maamuzi.
Kujua sababu halisi kunawasaidia watu kuelewa zaidi.” (TNT)
image
09/05/2026
Rekodi ya Liverpool msimu huu dhidi ya Arsenal, Chelsea, Man City na Man United kwenye Premier League:
⚽️Mechi 8
💥 Ushindi 1
🤝Sare 2
😔Vipigo 5
Msimu wa mateso na maumivu ya mara kwa mara kwa mashabiki wa Liverpool. Kiwango hiki hakikubaliki kwa timu yenye historia na ukubwa wa Liverpool FC.
Mabadiliko yanahitajika na yanahitajika haraka iwezekanavyo maana msimu ujao kila timu itajiandaa vilivyo.
09/05/2026
FT Liverpool 1-1 Chelsea.
Liverpool tumelazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Chelsea ndani ya Anfield… Matokeo ambayo kwa kweli hayakuridhisha kabisa
Licha ya kuwa na baadhi ya vipindi vizuri vya mchezo, bado tumeshindwa kutumia nafasi zetu na kupata ushindi muhimu nyumbani.
Slot bado kwenye swala la ufundi na Plan B hamna anachoweza kufanya, ni mgumu sana kumsoma mpinzani
Slot na mapenzi ya Gapko yataharibu mfumo mzima aa maamuzi ya msingi
09/05/2026
HT: Liverpool F.C. 1-1 Chelsea F.C.
Tunaenda mapumziko tukiwa sare baada ya uzembe wa ulinzi kwenye free-kick ya Chelsea.
Mmeionaje first half ?
07/05/2026
🚨 Liverpool wamefuta mpango wa kuongeza bei za tiketi kwa miaka mitatu mfululizo. Badala yake, kutakuwa na ongezeko la asilimia 3 pekee kwa tiketi za kawaida za msimu wa 2026/27, kisha bei zitabaki zilezile msimu wa 2027/28.
Mazungumzo zaidi yataendelea kati ya klabu na Bodi ya Mashabiki kuhusu misimu ijayo. Mashabiki walikuwa wameonyesha kupinga ongezeko la bei za tiketi.
(Paul Joyce)
06/05/2026
Wachezaji kadhaa wa Liverpool FC walikosekana kwenye mazoezi ya leo kuelekea mchezo wao ujao dhidi ya Chelsea FC, kulingana na Sky Sports.
05/05/2026
Kwa mujibu wa chombo cha habari cha Ureno, Record, klabu ya Liverpool FC inaendelea kufuatilia kwa karibu kipaji kikubwa cha FC Porto, Oskar Pietuszewski, ambaye ana kipengele cha kuvunjwa kwa mkataba (release clause) kinachofikia pauni milioni 52.
Chanzo :