14/05/2026
Mwamba wa Lusaka πΏπ², Clatous Chota Chama aendelea kuwasha moto ndani ya Simba SC baada ya kuwa nyota wa mchezo kwa mara ya nne mfululizo. π₯ Kiungo huyo fundi amefunga mabao mawili dhidi ya Mashujaa FC na sasa amefikisha jumla ya magoli 8 kwenye NBC Premier League msimu huu. β½β½
π Goals: 08
π― Assists: 04
14/05/2026
Simba SC waondoka na pointi tatu muhimu ugenini baada ya kuibuka na ushindi mnono dhidi ya Mashujaa FC. π΄βͺ
Ni mara ya kwanza kwa Mashujaa FC kupoteza mchezo wa nyumbani msimu huu.
FT: Mashujaa FC 0-3 Simba SC
β½β½ Chota Chama
β½ Suleiman Mwalimu π₯
13/05/2026
βUnbeaten is overβ; π₯
Kwa mara ya kwanza katika historia ya mikutano yao kwenye Ligi Kuu ya NBC, Dodoma Jiji wamefanikiwa kuibuka na ushindi dhidi ya Yanga SC.
FT: Dodoma Jiji 3οΈβ£-2οΈβ£ Yanga SC
Dodoma Jiji wameivunja rekodi ya kutowahi kuifunga Yanga na kuhitimisha ubabe wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo uliopigwa kwa ushindani mkubwa.
09/05/2026
KMC Kimeeleweka Yanga SC wanasalia kileleni wakifikisha alama 54 baada ya mechi 22 wakiwa wamecheza mechi moja zaidi ya Mnyama huo akifunga mabao mawili na kutoa asisti moja ikiwa ni mchango wa magoli 12 tangu atue jangwani mwezi Januari.
FT: Yanga SC 3-0 Coastal Union
β½ 18' Okello
β½ 62' Okello
β½ Maxi (π
°οΈ Okello)
08/05/2026
| MATOKEO YA MWISHO
Kwa mara ya kwanza msimu huu wa NBC Premier League, Azam FC imepoteza mechi baada ya kuchapwa mabao 4-1 dhidi ya TRA United. β½π₯
FT: TRA UNITED 4οΈβ£ - 1οΈβ£ AZAM FC
Wafungaji wa TRA United:
β½ Ally Ng'anzi
β½β½ Ammy Mapaka
β½ Ramadhani Chobwedo
Bao la Azam FC: .
β½ Jephte Kitambala
Matokeo hayo yanafuta rekodi ya kutopoteza ya Azam FC katika ligi msimu huu.
08/05/2026
Kufukuza kocha mwenye rekodi nzuri kuliko makocha wote, mwenye matokeo mazuri kuliko makocha wote, ni ishara kuwa matokeo ya uwanjani mliyopata hayatokani na ubora wa kiufundi.
Anaandika semaji Ahmed Ally .
08/05/2026
NONDO ZA CHISANO
Mimi sifanyi kazi Yanga FM, kwa hiyo usitarajie kila siku nikiwa kwenye kipindi nitasema yanayokufurahisha, kwa sababu mimi sipo Duniani kumridhisha mtu yoyote na hata RIZIQ ninayopata haitegemei kumfurahisha mtu ndio nile.
Ikitokea Timu yoyote imefanya vizuri nitasema na ikitokea nimeona timu yoyote kwenye Ligi imefanya vibaya nitasema bila chuki na uzuri unanijua kwamba mimi sio mwandishi wa kupokea bahasha au kuna haja ya kulieleza hilo kwa upana?
Inawezekana mimi ni miongoni mwa waandishi wachache walioitabiria Yanga itabeba ubingwa msimu huu baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Simba, yaani kabla ya michezo 10 ya Ligi kuisha kutokana na ubora walionao, lakini hilo halinifanyi nishindwe kuikosoa inapofanya vibaya.
NO HARD FEELINGS, TRUTH SHALL PREVAIL...
AMEANDIKA CHISANO JR
07/05/2026
RASMI: Simba SC Yahamia KMC Complex kwa Mechi Zilizosalia za Msimu
Klabu ya Simba SC imetangaza rasmi kuhamia katika Uwanja wa KMC Complex, ambapo sasa itautumia k**a uwanja wake wa nyumbani kwa mechi zote zilizosalia katika msimu huu.Awali, Simba SC ilikuwa ikitumia Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni k**a uwanja wa muda, kabla ya kufanya uamuzi wa kuhamia KMC Complex. Hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira ya maandalizi na ushindani wa timu, ili kuhakikisha kikosi kinapata nafasi bora ya kuendelea kupambana katika michezo yake iliyobaki ya msimu.
Mashabiki wa Simba SC wataendelea kushuhudia timu yao ikicheza katika uwanja huo mpya wa muda, wakitarajia matokeo chanya na mafanikio zaidi katika mechi zilizosalia.
07/05/2026
π¨ FAINALI YA KWANZA CAF CONFEDERATION CUP KUPIGWA JUMAMOSI HII! π₯π
Jumamosi hii, Mei 9, mechi ya kwanza ya fainali ya inatarajiwa kupigwa kwa ushindani mkubwa. πβ½
watakuwa nyumbani katika dimba la Stade du 5 Juillet (STD 5 Juliet) wakiwakaribisha . π©πΏππͺπ¬
β Swali kubwa: Ni USM Alger au Zamalek SC nani ataanza kuonja harufu ya ubingwa kwenye mechi ya kwanza ya fainali? ππ₯
β½