08/05/2026
MWEMBE YANGA KUTAWAKA MOTO! 🔥
Baada ya mbio za kishindo za Team One Dar zitakazohusisha vilabu nguli vya Dar Jogging Club, Haipotei, na Fanja Jogging Club, sasa tunawaletea burudani nyingine ya ziada!
Tunawaletea MECHI YA MASHEMEJI yenye upinzani wa jadi kati ya Dar Jogging Club dhidi ya Haipotei Jogging Club. Huu siyo mchezo tu, ni heshima ya mtaa!
Swali la kizushi:
Je, kicheko kitaenda kwa Katibu Mkuu wa Dar Jogging, Six? Au ndugu Gea Katibu Mkuu wa Haipotei atatisha?
Mechi hii ni May 10, 2026
Uwanja wa Mwembe Yanga
Kuanzia saa 4:00 kamili asubuhi.
Weka maoni yako hapa chini: Unampa nani ushindi siku hiyo?
07/05/2026
Klabu ya Dar Jogging inapenda kumtambulisha rasmi mwanachama wetu mpya, Asnat Said, ambaye amechagua kwa ridhaa yake kujiunga na familia hii kubwa ya michezo nchini.
Tunajivunia kuendelea kuvutia watu wenye nia ya kuimarisha afya na umoja. Karibu sana klabuni, Asnat! Safari ya afya na furaha inaanza hapa.
06/05/2026
KARIBU NYUMBANI BI. FATUMA JUMA! 🌹
Tunaendelea pale tulipoishia wiki iliyopita kwa habari njema! Klabu yetu kubwa inapenda kumtambulisha kwenu mwanachama wetu mpya, Bi. Fatuma Juma.
Tunakuomba mwanachama mwenzetu upokee upendo wetu wa dhati. Sisi ni klabu inayojengwa na misingi ya:
✅ Upendo wa kweli
✅ Ushirikiano wa dhati
✅ Kuthamini utu wa kila mwanachama
Karibu sana Bi. Fatuma, hapa ni mahali pa amani na maendeleo. Twende sawa! 🤝✨
03/05/2026
Leo Jumapili, tarehe 03/05/2026, klabu ya Amazon Jogging imepata ugeni wa bashasha kutoka kwa klabu kubwa ya Dar Jogging Club, katika mbio maalum za kuimarisha mahusiano na umoja baina ya vilabu vyetu.
Mbio hizi zimepambwa na morari ya hali ya juu kutoka kwa wanachama wa vilabu vyote viwili, zikiashiria ushirikiano mkubwa uliopo katika tasnia ya JOGGING nchini. Zaidi ya afya, mbio hizi ni sehemu ya hamasa na maandalizi kuelekea tamasha letu kubwa la "TWENZETU KWA BABA SEASON 02" linalotarajiwa kufanyika tarehe 14/06/2026.
Tunawashukuru sana Amazon Jogging kwa kujumuika nasi. Umoja huu ndio nguzo yetu kuelekea mwezi wa sita!
Twenzetu Kwa Baba Season 02 – Sote kwa pamoja, Afya kwanza!
01/05/2026
DAR JOGGING CLUB x AMAZON JOGGING: KAZI IMEANZA! 🔥
Jumapili hii, 03/05/2026, tunaiamsha Mbagala! Ni mwendo wa hamasa kuelekea "TWENZETU KWA BABA (Season 02)". Hatuji kupiga picha, tunakuja kutuma salamu kwa Temeke Jogging!
Njia: Kuanzia Mbagala Maji Matitu hadi Saku (Ofisi za Amazon).
Lengo: Afya, Umoja, na Maandalizi ya Bonanza la tarehe 14/06/2026.
Wana-Dar Jogging na wadau wote wa michezo, tukutane barabarani. Mbagala itachafuka kwa amsha amsha! 🤜🤛
30/04/2026
"Dar Jogging Club: Zaidi ya Klabu, Sisi ni Familia! 🤝
Tunaendelea kuimarisha kikosi chetu kwa kuongeza wanachama wapya wenye nia ya kuimarisha afya na kuhamasisha jamii kufanya mazoezi.
Leo tunawapokea kwa mikono miwili:
✨ Juma Mpalule
✨ Hance Said Ndete
✨ Nadia Adnani
Hongereni kwa kuchagua upande wa afya. Mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza yanaendelea kila siku barabarani!
Kaa tayari... kesho kuna sura nyingine mpya! Je, ni wewe?
29/04/2026
DAR JOGGING CLUB: ZAIDI YA KIBABE!
Ni Klabu kubwa ya Dar Jogging inaendelea kupata nguvu mpya. Tunawakaribisha rasmi:
✅ Patrick – Fundi wa mpira, "Number 10" anayekuja kuungana na #6 na #8 Kasasy. Karibu uwanjani uoneshe ufundi wako!
✅ Asha Juma – Karibu sana kwenye klabu bingwa na kubwa kuliko zote Tanzania.
Safari ndio kwanza imeanza, katu hatusimami! Karibuni sana nyumbani.
28/04/2026
Karibu sana kwenye familia, Mimah Omary!✨
Tunafurahi kukupokea ndani ya Dar Jogging Club, mahali ambapo amani, furaha, na upendo ndio msingi wa kila hatua tunayopiga. Tunakupenda na tuko tayari kukimbia nawe kuelekea kwenye afya bora na ushirikiano wa dhati.
Karibu tujenge mwili na kudumisha undugu! 🤝💪