Dar Jogging Club

Dar Jogging Club

Share

Dar jogging club established officially 20th June 2002.

The club Founders are Samia Hujjat, Ramadhan Namkoveka, Abdulkadri Omary, Abdul Mushi, Saidi Lingamba, Pili Salehe, Selemani Ndambwe, Ahmed Ismail Ruhumba and Pili Nyamkili.

Photos from Dar Jogging Club's post 08/05/2026

MWEMBE YANGA KUTAWAKA MOTO! 🔥

Baada ya mbio za kishindo za Team One Dar zitakazohusisha vilabu nguli vya Dar Jogging Club, Haipotei, na Fanja Jogging Club, sasa tunawaletea burudani nyingine ya ziada!

Tunawaletea MECHI YA MASHEMEJI yenye upinzani wa jadi kati ya Dar Jogging Club dhidi ya Haipotei Jogging Club. Huu siyo mchezo tu, ni heshima ya mtaa!

Swali la kizushi:
Je, kicheko kitaenda kwa Katibu Mkuu wa Dar Jogging, Six? Au ndugu Gea Katibu Mkuu wa Haipotei atatisha?

Mechi hii ni May 10, 2026
Uwanja wa Mwembe Yanga
Kuanzia saa 4:00 kamili asubuhi.

Weka maoni yako hapa chini: Unampa nani ushindi siku hiyo?

07/05/2026

Klabu ya Dar Jogging inapenda kumtambulisha rasmi mwanachama wetu mpya, Asnat Said, ambaye amechagua kwa ridhaa yake kujiunga na familia hii kubwa ya michezo nchini.

Tunajivunia kuendelea kuvutia watu wenye nia ya kuimarisha afya na umoja. Karibu sana klabuni, Asnat! Safari ya afya na furaha inaanza hapa.

06/05/2026

KARIBU NYUMBANI BI. FATUMA JUMA! 🌹

Tunaendelea pale tulipoishia wiki iliyopita kwa habari njema! Klabu yetu kubwa inapenda kumtambulisha kwenu mwanachama wetu mpya, Bi. Fatuma Juma.

Tunakuomba mwanachama mwenzetu upokee upendo wetu wa dhati. Sisi ni klabu inayojengwa na misingi ya:
✅ Upendo wa kweli
✅ Ushirikiano wa dhati
✅ Kuthamini utu wa kila mwanachama

Karibu sana Bi. Fatuma, hapa ni mahali pa amani na maendeleo. Twende sawa! 🤝✨

04/05/2026

DAR JOGGING CLUB x AMAZON JOGGING: MBAGALA IMEWAKA MOTO! 🔥

BKilele cha amsha-amsha ya Jumapili hii, 03/05/2026! Tulianzia Mbagala Maji Matitu na kutokeza Saku—si mchezo, lami ilielewa kuwa wenye mji wameingia barabarani!

Hii siyo tu mazoezi, ni salamu rasmi kwa marafiki zetu wa Temeke Jogging. Tunajiwasha moto kwa ajili ya "TWENZETU KWA BABA (Season 02)" tarehe 14/06/2026.

Mbagala ilivyochafuka kwa hamasa, umoja, na afya! Kazi ndiyo kwanza imeanza!

Photos from Dar Jogging Club's post 03/05/2026

Leo Jumapili, tarehe 03/05/2026, klabu ya Amazon Jogging imepata ugeni wa bashasha kutoka kwa klabu kubwa ya Dar Jogging Club, katika mbio maalum za kuimarisha mahusiano na umoja baina ya vilabu vyetu.

Mbio hizi zimepambwa na morari ya hali ya juu kutoka kwa wanachama wa vilabu vyote viwili, zikiashiria ushirikiano mkubwa uliopo katika tasnia ya JOGGING nchini. Zaidi ya afya, mbio hizi ni sehemu ya hamasa na maandalizi kuelekea tamasha letu kubwa la "TWENZETU KWA BABA SEASON 02" linalotarajiwa kufanyika tarehe 14/06/2026.

Tunawashukuru sana Amazon Jogging kwa kujumuika nasi. Umoja huu ndio nguzo yetu kuelekea mwezi wa sita!

Twenzetu Kwa Baba Season 02 – Sote kwa pamoja, Afya kwanza!

01/05/2026

DAR JOGGING CLUB x AMAZON JOGGING: KAZI IMEANZA! 🔥

Jumapili hii, 03/05/2026, tunaiamsha Mbagala! Ni mwendo wa hamasa kuelekea "TWENZETU KWA BABA (Season 02)". Hatuji kupiga picha, tunakuja kutuma salamu kwa Temeke Jogging!

Njia: Kuanzia Mbagala Maji Matitu hadi Saku (Ofisi za Amazon).

Lengo: Afya, Umoja, na Maandalizi ya Bonanza la tarehe 14/06/2026.

Wana-Dar Jogging na wadau wote wa michezo, tukutane barabarani. Mbagala itachafuka kwa amsha amsha! 🤜🤛

Photos from Dar Jogging Club's post 30/04/2026

"Dar Jogging Club: Zaidi ya Klabu, Sisi ni Familia! 🤝

Tunaendelea kuimarisha kikosi chetu kwa kuongeza wanachama wapya wenye nia ya kuimarisha afya na kuhamasisha jamii kufanya mazoezi.

Leo tunawapokea kwa mikono miwili:
✨ Juma Mpalule
✨ Hance Said Ndete
✨ Nadia Adnani

Hongereni kwa kuchagua upande wa afya. Mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza yanaendelea kila siku barabarani!

Kaa tayari... kesho kuna sura nyingine mpya! Je, ni wewe?

Photos from Dar Jogging Club's post 29/04/2026

DAR JOGGING CLUB: ZAIDI YA KIBABE!

Ni Klabu kubwa ya Dar Jogging inaendelea kupata nguvu mpya. Tunawakaribisha rasmi:

✅ Patrick – Fundi wa mpira, "Number 10" anayekuja kuungana na #6 na #8 Kasasy. Karibu uwanjani uoneshe ufundi wako!
✅ Asha Juma – Karibu sana kwenye klabu bingwa na kubwa kuliko zote Tanzania.

Safari ndio kwanza imeanza, katu hatusimami! Karibuni sana nyumbani.

28/04/2026

Karibu sana kwenye familia, Mimah Omary!✨

Tunafurahi kukupokea ndani ya Dar Jogging Club, mahali ambapo amani, furaha, na upendo ndio msingi wa kila hatua tunayopiga. Tunakupenda na tuko tayari kukimbia nawe kuelekea kwenye afya bora na ushirikiano wa dhati.

Karibu tujenge mwili na kudumisha undugu! 🤝💪

22/04/2026

"MWENYEKITI MSTAAFU WA CHAMA CHA JOGGING TEMEKE NA M***A MTULYA ASISITIZA SUALA LA NIDHAMU KWENYE MCHEZO HUU WA JOGGING"

"HII NI BAADA YA KUONA KUNA ONGEZEKO KUBWA LA VIJANA WENYE UMRI MDOGO KUSHIKA NAFASI ZA UONGOZI KWENYE CLUB ZAO HIVYO KUWASIHI WANACHAMA WAO KUWAHESHIMU VIONGOZI HAO KWASABABU WANAONGOZA KWA MUJIBU WA KATIBA YA CLUB YAKO"

21/04/2026

RASMI, Rasmi

Kazi iendelee! 🤝

Tumelipokea kwa mikono yote miwili mwaliko na ushirikiano wa BONANZA LA TWENZETU KWA BABA SEASON 02 kutoka kwa ndugu zetu wa damu kabisa Temeke Jogging

Tunaanza safari ya pamoja kuelekea tarehe 14/06/2026. Hakikisha hukosi msimu huu wa kipekee wenye burudani na afya tele.

Shukrani kwa kutuamini. Tukutane barabarani!




Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Website

Address


Chang'ombe Unubini
Dar Es Salaam

Opening Hours

Monday 15:00 - 18:00
Wednesday 15:00 - 18:00
Saturday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00