14/06/2026
Yanga Whatsapp Makao Makuu
Ni Tawi La YANGA WHATSAPP SUPPORTERS MAKAO MAKU. Call 0685188679
Support Yako Kwa Ajili Ya Tawi
NMB
14/06/2026
14/06/2026
TAARIFA YA UCHAGUZI 2026
Tarehe 25 Juni 2026
TAWI LA YANGA WHATSAPP SUPPORTERS – MAKAO MAKUU
Tawi la Yanga WhatsApp Supporters – Makao Makuu linapenda kuwatangazia wanachama wote kuwa uchaguzi wa Kamati ya Uongozi wa Tawi utafanyika hivi karibuni. Wanachama wenye sifa na nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wanakaribishwa kuwasilisha maombi yao kwa kuzingatia masharti na taratibu zilizoainishwa hapa chini.
NAFASI ZITAKAZOGOMBEWA
Mwenyekiti
Makamu Mwenyekiti
Katibu
Katibu Msaidizi
Mweka Hazina
Wajumbe (Wanne)
SIFA ZA MGOMBEA
Ili mwanachama aweze kugombea nafasi yoyote ya uongozi, anatakiwa kukidhi vigezo vifuatavyo:
i) Awe mwanachama hai wa Tawi kwa kipindi cha angalau miaka mitatu (3) mfululizo.
ii)Awe na elimu ya kuanzia darasa la saba (7) na kuendelea.
iii)Awe na maadili mema na kuheshimika ndani ya Tawi na jamii kwa ujumla.
iv)Awe tayari kutimiza majukumu ya nafasi anayoigombea kwa weledi na uwajibikaji.
ADA YA KUGOMBEA NAFASI MBALIMBALI
Nafasi
Ada (Tsh)
Mwenyekiti
30,000
Makamu Mwenyekiti
30,000
Mweka Hazina
30,000
Katibu
20,000
Katibu Msaidizi
20,000
Mjumbe wa Tawi
15,000
TARATIBU
Wagombea wanatakiwa kulipa ada husika wakati wa kuchukua fomu.
Malipo yatalipwa kwa katibu wa kamati ya uchaguzi Wakhda Ramadhan 0759327514
Majina ya wagombea yatatangazwa rasmi kwa wanachama wote kabla ya siku ya uchaguzi.
Uchaguzi utafanyika kwa njia ya kura za siri/wazi (kulingana na maelekezo ya Kamati ya Uchaguzi).
Uchaguzi utafanyika tarehe 25 mwezi wa 6
Muda wa kuchukua fomu kuanzia tarehe 14 mwezi wa 6 na kurudisha fomu mwisho tarehe 21 mwezi wa 6
Kampeni zinaanza tarehe 22 mwezi wa 6 hadi tarehe 24 mwezi wa sita.
Kwa maswali au maelezo zaidi, wanachama wanaombwa kuwasiliana na Kamati ya Uchaguzi ya Tawi.
Mwenyekiti Mpingwa Duma
Katibu: Wakhda Ramadhan
Daima Mbele Nyuma Mwiko– YANGA SC!
13/06/2026
𝐇𝐓’|
Mashujaa FC 0🆚1 Young Africans SC
Young Africans hii club bhana ina raha sana, hii clab ndo inaongoza kwa kupigwa mawe, hii hutokana na ubora uliopo ndani ya watu wake
Viongozi
Watendaji
Wanachama
Mashabiki wote mara nyingi tunakuwa kwenye msitari mmoja, hii inawapa ugumu sana wapinzani wetu kuweza kutusambaratisha
Daima Mbele, Nyuma Mwiko ipo kwa vitendo nadhani aliyetuchagulia hii slogan alipata ilham kutoka kwa Mungu
Click here to claim your Sponsored Listing.
Location
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
Dar Es Salaam
1550