SokaOnline

SokaOnline

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from SokaOnline, Sports, Dar es Salaam.

13/05/2026

FULL TIME ⏰

Alaves 1️⃣ ➖ 0️⃣ Barcelona

⚽ 45+1' Ibrahim Diabate

Barcelona hawana cha kupoteza kwasababu wameshabeba ubingwa wa La Liga 🇪🇸 msimu huu.

Ukiibetia Barcelona ya sasa unajitafutia matatizo tu 😂

12/05/2026

🚨 TAARIFA RASMI KUTOKA BARCELONA

Idara ya sheria ya Barcelona inachunguza kwa makini taarifa na shutuma za Perez.

Kauli hizo zitachambuliwa zitatathiminiwa.

Kila mtu atafahamishwa kuhusu msimamo na maamuzi yatakayochukuliwa.

12/05/2026

🗣️ Florentino Perez:

"Vyombo vya habari vinahitaji kuchambua lakini havipaswi kusema kwamba kwa sababu watu wawili wamepigana basi kuna machafuko ndani ya Real Madrid.

Wachezaji wanapigana kila mwaka, wanapigana kila siku na mambo yanaishia ndani. K**a kuna mtu ndani ya klabu ataiweka hadharani ni MBAYA kuliko mapigano yenyewe.

Tchouameni na Valverde ni marafiki, ilikuwa ni mbaya zaidi kwasababu taarifa zilivuja"

12/05/2026

🚨🗣️ Florentino Perez:

"Nimeshinda mataji saba ya ligi nikiwa na Real Madrid ambayo yangeweza kuwa 14 kwa sababu nimeibiwa sana. Tumetengeneza video kuhusu alama 18 ambazo tumepoteza kwa kunyang'anywa msimu huu."

12/05/2026

🚨 Florentino Perez:

"Wanachama wa Real Madrid wako pamoja nami katika vita vyangu dhidi ya Negreira. Sio kwamba inayoteseka ni Real Madrid tu, kuna timu nyingine pia zinaumizwa na Barça ndio wafaidika. Naamini UEFA wataingilia kati suala hili, Hii haikubaliki kabisa. Sikuja hapa ili waamuzi wapate utajiri kupitia pesa za Barcelona. Nilikuja hapa kupambana"

Sakata la Negreira analolizungumzia Perez ni kesi aliyoifungua dhidi ya José María Enríquez Negreira ambae alikuwa mwamuzi wa zamani na, muhimu zaidi, alikuwa Makamu wa Rais wa K**ati ya Waamuzi nchini Uhispania kuanzia mwaka 1994 hadi 2018.

​Kashfa yenyewe ni ipi?

​Uchunguzi wa kodi nchini Uhispania uligundua kuwa klabu ya FC Barcelona ililipa kampuni inayomilikiwa na Negreira (DASNIL 95 SL) zaidi ya Euro milioni 7 (takriban Shilingi za Kitanzania bilioni 20+) kati ya mwaka 2001 na 2018.

​Upande wa Mashtaka: Wanadai kuwa Barcelona walilipa pesa hizo ili kupata upendeleo kutoka kwa waamuzi au kuhakikisha kuwa maamuzi ya waamuzi hayawaumizi uwanjani. Hii inatazamwa k**a "rushwa ya kimichezo."

​Upande wa Barcelona: Klabu hiyo inakiri kulipa pesa hizo, lakini inadai kuwa zilikuwa ni kwa ajili ya "ripoti za kiufundi" (technical reports). Walitaka maelezo kuhusu tabia za waamuzi tofauti ili wachezaji wao wajue jinsi ya kuishi nao uwanjani (kwa mfano, mwamuzi gani anatoa kadi kwa urahisi)

12/05/2026

🚨 Florentino Perez:

"Sielewi ni kwanini vyombo vya habari vya Uhispania vimeandika kuwa Nitaondoka. Mimi sitaondoka.

Nitakuwa mwanachama wa MWISHO kuondoka. K**a kuna mtu anataka kugombea urais, hapaswi kutishia tu kugombea, wanapaswa kugombea na kuelezea jinsi watakavyofadhili. Hawapaswi kutegemea pesa za mabenki au kuuliza marais wa makampuni ya umeme k**a wanaweza kusaidia ugombea wao"

12/05/2026

🗣️ Rais wa Real Madrid 🇪🇸 Florentino Perez:

"Real Madrid ndio klabu iliyoshinda mataji mengi katika historia ya dunia. Ni Klabu yenye thamani zaidi kulingana na Forbes. Hii ni brand ya thamani zaidi.

Kwa nini waandishi wa habari wanaokosoa klabu ya kifahari yenye mashabiki wengi duniani wanataka kuingilia kazi? Sisi tuna kikosi chenye ukadiriaji wa juu zaidi kulingana na Transfermarkt. Tuna kila kitu"

12/05/2026

🚨🗣️ Rais wa Real Madrid 🇪🇸 Florentino Perez:

"Kuna kampeni ya kunipinga, Lakini sitajiuzulu, bado nipo hapa na mimi ndio rais wa klabu.

Kuna kitu kimetengenezwa dhidi yangu na Real Madrid, hatuwezi tukawa tunashinda kila siku japo hatukubaliani na hali hii.

Watu wanatumia hali hii k**a fursa ya KUNISHAMBULIA na wengine wanasema mimi ni mgonjwa, nina saratani.

Nachukua fursa hii kuwashukuru na kuwaambia watu ambao wana wasiwasi juu yangu. Mimi bado ni rais na afya yangu ni imara .

Hizi taarifa za kusema nina saratani, zimetengenezwa tu"

12/05/2026

🚨🗣️ Toni Kroos:

"Kumaliza Msimu mmoja bila kombe kwa Real Madrid ni mbaya lakini kumaliza misimu miwili mfululizo? Hiyo ni mbaya zaidi na HAIKUBALIKI"

Unakubaliana na Mkongwe Toni Kroos?

12/05/2026

🚨 Rais wa Real Madrid 🇪🇸 Florentino Perez (79) atazungumza leo saa moja kamili usiku kuhusu mwenendo wa klabu hiyo msimu huu.

Perez atajibu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari baada ya kumaliza hotuba yake.

Dunia inasubiri kauli yake baada ya kumaliza msimu wa pili bila kombe lolote.

12/05/2026

🚨 OFFICIAL: Arsenal 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 imethibitisha kuwa beki wao wa kulia Ben White atakuwa nje ya uwanja kwa mechi zote zilizobaki kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya goti.

White atarejea uwanjani kwenye maandalizi ya msimu mpya wa 2026-27

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Website

Address


Dar Es Salaam