03/06/2026
Kiungo wa Yanga SC, Allan Okello amekabidhiwa medali 🥇 yake ya ubingwa ligi kuu ya Uganda ambao klabu yake ya zamani, Vipers imeutwaa..
Okello alichangia magoli 03 na assist 03 kwenye mechi 06 kabla ya kusajiliwa na Yanga kwenye dirisha dogo..
Abdulkarim Watambala ambaye ni MVP wa ligi kuu ya Uganda msimu huu ndiye aliyempelekea medali hiyo Star Boy walipokutana kwenye kambi ya timu ya taifa..
Star Boy 🥇
31/05/2026
Hilo ni parade la Arsenal wakishangilia ubingwa wa EPL hii leo 🔥🔥
Cheki hiyo nyomi ya watu...
Na tungebeba UCL 🏆 hakuna rangi mngeacha ona...🤐
31/05/2026
Wakati Young Africans wakitajwa kuwa kwenye mchakato wa kuipata saini ya winga kinda mwenye ufundi wakutosha, Juma Issa Abushiri kutoka Fountain Gate, pia taarifa zaidi zinaeleza kuwa vilabu kutoka bara la Ulaya ikiwemo klabu ya Malmo vinamfuatilia kwa ukaribu kinda huyo..
Malmo wanatajwa kumhitaji kwaajili ya majaribio kisha wakiridhika na kiwango chake watampa mkataba rasmi..
Fountain Gate..... Gate way to Europe 📌
30/05/2026
Hili tunabeba 🙂
tukutane saa moja... 🏆
29/05/2026
Kwa mujibu wa mchambuzi, Dominick Salamba... Wachezaji WA KIGENI pale Yanga SC wenye hadhi ya kuibeba timu kwenye hatua za mtoano (Kuanzia Robo Fainali) ni wawili tu..
1. Djigui Diarra
2. Yao Kouassi
Salamba anasema, wengine k**a kina Maxi, Duke Abuya watakusaidia kwenye mechi za kawaida tu mpaka hatua ya makundi na hizi za ndani.
Kuhusu nyota k**a Pacome Zouzoua, Salamba anasema bado ni miongoni mwa wachezaji ambao hawana standard ya robo final huku akisema pia umri wake umemtupa mkono...
KWA UPANDE WAKO, UNAMTAZAMO GANI?!
Ni kweli Yanga SC hawana material za viwango vya CAF
29/05/2026
Future ya Tanzania iko kwenye mikono salama...
Vijana wenye vipaji vikubwa, uthubutu na nguvu wawapo kwenye pitch...
Umri sahihi wa kukua kisoka, misingi bora ya academies zao hatimaye matunda yanaanza kuonekana..
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, U-17 (Serengeti Boys) wanatupeleka fainali ya AFCON 🔥
Hongera nyingi mno kwa vijana na technical staff 👏👏👏
Wataumana na Senegal 📌
28/05/2026
CHUKUA KUTOKA KWANGU 😎
Nipo hapa kuthibitisha kuwa, Stephan Aziz Ki kurejea Yanga SC ni suala la muda tu...
Kiungo hana mpango wa kucheza Libya msimu ujao, Yanga wapo kwenye hatua nzuri ya kumrejesha nyumbani...
Case closed 🔐
28/05/2026
Taarifa zisizo rasmi zinadai vilabu kutoka Tanzania vinavutiwa na winga wa Al Hilal Omdurman, Jean Claude Girumugisha ingawa hakuna OFA rasmi..
Akizungumza na Uyui FM, Patrick Gakumba ambaye ni wakala wa winga Jean Claude Girumugisha anasema Tanzania hakuna timu inayoweza kumsajili mchezaji wake Jean Claude Girumugisha kutokana na ada yake.
Gakumba anasema ada ya winga huyo kwa sasa ni inaanzia Tsh Bilioni 03..🔥
Hata hivyo, winga huyo amekuwa bidhaa ya moto sokoni, vilabu mbalimbali vinatarajiwa kupigana vikumbo kuiwinda saini yake...📌
27/05/2026
Kulingana na kanuni za Shirikisho la soka la Uganda, mchezaji aliyecheza walau mechi tano kwenye klabu inayoshiriki ligi kuu ya Uganda kisha akaondoka klabuni, mchezaji huyo ana haki ya kupata medali ikiwa timu yake itatwaa ubingwa..
Allan Okello atavaa medali 🥇 ya ubingwa baada ya klabu yake ya zamani,Vipers kutwaa ubingwa...
Okello aliifungia Vipers mabao 03 msimu huu (mzunguko wa kwanza) kabla ya kuondoka na kujiunga na Yanga SC.
Star boy 🥇
27/05/2026
Kwa tathmini ya haraka tu, Azam FC msimu huu wana defence nzuri..
Safu ya ulinzi inaundwa kuanzia kwa namba 6, full backs 2&3, center backs 4&5 pamoja na goli kipa..
Dimba lao la chini msimu huu limekuwa chini ya Himid Mao, mimi hupenda kumwita "Mzee Kigogo".
Himid anatoa darasa jinsi gani ya kucheza kwenye zone ile, anafanya kazi kubwa sana kupokonya mipira, anapiga pass kwa usahihi mkubwa na analinda vyema ukuta wake..
Kwenye full backs, imekuwa ni mwendelezo tu wa kile ambacho wamekuwa bora kwacho misimu kadhaa tangu wapandishwe senior team..
Captain Lusajo Mwaikenda mbavu ya kulia na Pascal Gaudence mbavu ya kushoto..🔥
Central defenders, bwana mdogo Twalib Nuru amekuja kutoa surprise kwa ma pro ambao tayari wana experience ya kutosha, ameaminiwa kucheza mechi nyingi ikiwemo za CAF pamoja na Fuentes Mendoza, huku Yoro Diaby, Landry Zouzou wakiingia pia mara chache kwenye kikosi.
Msimu bora kwao k**a idara ya ulinzi...
Golini pia wamekuwa wakigawana mechi, Aishi Manula, Zuberi Foba na Issa Fofana.
Wametoa mchango bora sana wakiihakikishia clean sheets 21 kwenye mechi 25 🔥
•Aishi Manula - 11 clean sheets
•Zuberi Foba - 09 clean sheets
•Issa Fofana - 01
Hili ni miongoni mwa maeneo ambayo Azam FC wako bora sana, hata kuwapo nafasi waliyopo sasa utagundua ni sare walizopata mechi za mwanzo kutokana na kukosa ufanisi wa kufunga..
Wakati huo bado Feisal na Iddi Nado hawaja waka k**a ilivyosasa..
Binafsi naona Azam FC watahitaji maboresho kidogo tu kwenye eneo hilo (ULINZI) kwaajili ya kuongeza nguvu zaidi📌