09/09/2017
kesho ni mwendo wa mateka huko njombe
FRIENDSHIP ONLY
09/09/2017
kesho ni mwendo wa mateka huko njombe
leo wachimba ming'oko wameshinda pale nangwanda international stadium. hongera ndanda kwa ushindi mnono leo.
06/03/2016
05/03/2016
Saa 10 : 00 Alasiri pale Uwanja wa Taifa. . Moja ya Safu kali za ushambuliaji barani Afrika MTN watakuwa kiwanjani wakitekeleza majukumu yao ya kufumania nyavu.
LIKES NGAPI KWA MTN?
02/03/2016
>>>Kumeibuka tabia ya Wakenya kung'ang'ania hazina ya Taifa letu na kunadai ni mali yao.
*************** TAHADHARI*************
Tafadhalini sana Wakenya
Msije mkathubutu kusema Young Africans ni yenu, tutawafuata hadi kwenu!! Ila mkisema Simba Sports Club ni yenu tutawaletea hadi Namanga FOR FREE, gharama za usafiri zote zetu!!
Yanga ni fahari ya Taifa letu,Yanga ni hazina ya watanzania!
WANANCHI WA TANZANIA WANAIPENDA YANGA.
29/02/2016
Robo Fainali ya kombe la shirikisho (FA CUP) Yanga kucheza na Coastal Union jijini Dar katika uwanja wa Taifa!Huku Simba kusubiri mshindi baina ya Azam FC dhidi ya Panone FC.
Wakati huo huo Yanga inaendelea kujifua kisiwani Pemba kujiwinda na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam,mchezo utakaopigwa March 5.
26/02/2016
MINENO YA JERRY YAMTOA POVU HAJI MANARA AAPA KWENDA POLISI.
Baada ya Simba SC kupigwa goli 2 - 0 hii ndo ilikuwa kauli ya Murro.
"Wamchangani hawawezi kutufunga Sisi hata wachezeshe wachezaji wao 40 pamoja na viongozi wao 10 tena yule mzee wa kachumbari ya miiba (Mr . Makofia) awemo lakini hawawezi kuifunga Yanga ikiwa na wachezaji 12 pamoja na mimi. .
"Mara ya kwanza tumewalamba mbili, ikaja tena tumewalamba mbili . . Jamani kuna kubahatisha hapa??uwezo wa Thaban Kamusoko ni sawa na uwezo wa wachezaji wao viungo watatu, siongei tu kuna takwimu hapa.
"Wao wanaajiri kocha wanaenda kumpokea kwenye basi la Simba Mtoto ama Raha leo pale Ubungo,Sisi Yanga Afrika kocha wetu anapanda ndege huko Uholanzi tunampokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere. . Utawezaje kuwaweka kwenye mizania sawa?Lazima wajue kutofautisha kati ya tui na maziwa japo vyote vinafanana"Alimalizia Jerry Murro.
Baada ya kusikia hayo Haji Manara leo amemshutumu Murro kuwa ametoa kauli zenye kibaguzi na lazima ataenda kumshtaki sio TFF tena bali ni Polisi ama Mahakamani
Haya ndio majibu ya Muro
“Kwani ni uongo kusema kocha wao amekuja kwa basi na wetu amekuja kwa ndege? Si wamemsajili kutoka Coastal pale Tanga na wetu ni Mholanzi amekuja kwa ndege. K**a amaamini amedhalilishwa aende kwenye vyombo vya dola akashtaki,” alisema Muro.
YANGA NI KUSHINDA TU