Sportszone Tanzania

Sportszone Tanzania

Share

We give that you deserve

12/02/2025

πŸ˜‚πŸ˜‚ Nasoma Comments

04/11/2023

African Football League

Mechi ya fainali mkondo wa kwanza kupigwa kesho jumapili kwa Wydad Casablanca kuwakaribisha Mamelodi Sundowns katika dimba la Mohammed V

Msimu uliopita katika nusu fainali ligi ya mabingwa Mamelodi alitolewa na Wydad

Je, Mamelodi atalipa kisasi ama Wydad kuendeleza ubabe?

04/11/2023

Kocha Mamelodi Sundowns, Rhulani Mokwena ameijia juu klabu ya Al Ahly kwa kile alichokitaja k**a "wanalalamikia kila kitu" baada ya Mafarao hao kudai kuwa mwamuzi aliwanyima penalti katika mchezo wa mkondo wa pili wa nusu fainali ya kombe la Afrika 'AFL'.

Al Ahly ilipoteza kwa matokeo ya jumla ya 1-0 kufuatia kipigo cha 1-0 katika dimba la Loftus Versfeld, Pretoria Afrika Kusini kabla ya sare ya 0-0 kwenye marudiano Cairo. Baada ya mechi hiyo Mafarao hao walimlalamikia Mwamuzi kuwa aliwanyima penalti.

β€œNashangazwa sana na Al Ahly wanalalamikia kila kitu. Kabla ya mechi ya kwanza, Al Ahly walilalamika kwamba tulicheza saa 9:00 alasiri na bado walikuwa na uwezo wa kurekebisha mchezo kwa wakati unaofaa wakiwa kwao, lakini hautasikia malalamiko kutoka kwa Sundowns."

β€œKinachoshangaza zaidi ni kwamba Al Ahly huwa wanalalamikia waamuzi pale tu wanapopoteza. Jose Mourinho aliwahi kusema kuwa klabu kubwa inapoanza kutafuta sababu nyingine nje ya soka inaposhindwa basi ndio inaanza kupoteza hadhi yake ya kuwa klabu kubwa. Natumai sivyo ilivyo kwa AL Ahly kwa sababu ni kielelezo cha soka la Afrika."

β€œBaada ya malalamiko hayo ni nini hasa lengo lao? Kwa sababu ninaweza kupitia orodha ya matukio, ambapo waamuzi hawakufanya kile nilichofikiri ni haki kwetu. Mwishoni mwa mechi, Sundowns ilifanya faulo saba na kupata kadi mbili za njano lakini Al Ahly walifanya faulo 13 na kupata kadi moja ya njano. Nadhani k**a kuna timu ilipaswa kulalamika basi ilitakwa kuwa Sundowns.” alieleza Mokwena.

Sundowns itachuana na Wydad Casablanca katika fainali ambapo mechi ya mkondo wa kwanza wa fainali itapigwa Jumapili Novemba 5, katika dimba Mohammed V, Casablanca kabla ya kurudiana Novemba 12, 2023 katika dimba la Loftus Versfeld, Pretoria Afrika Kusini.

Mshindi wa michuano hiyo mipya kabisa atatia kibindomi kitita cha dola milioni 4, huku mshindi wa pili akitarajiwa kuchukua dola milioni 3.

04/11/2023

π— π—”π—§π—’π—žπ—˜π—’ 𝗬𝗔 π—¦π—’π—žπ—” 𝗝𝗔𝗑𝗔 π—œπ—π—¨π— π—”π—”

𝗙π—₯π—”π—‘π—–π—˜: Ligue 1
FT Paris SG - Montpellier 3:0

π—šπ—˜π—₯𝗠𝗔𝗑: Bundesliga
FT Darmstadt - Bochum 1:2

π—œπ—§π—”π—Ÿπ—¬: Serie A
FT Bologna - Lazio 1:0

π—¦π—£π—”π—œπ—‘: LaLiga
FT Las Palmas - Atl. Madrid 2:1

π—•π—˜π—Ÿπ—šπ—œπ—¨π— : Jupiler Pro League
FT St. Truiden - Eupen 1:1

𝗗π—₯ π—–π—’π—‘π—šπ—’: Ligue 1
FT Mazembe - Sanga Balende 2:0

π—˜π—šπ—¬π—£π—§: Premier League
FT Smouha - Al Ittihad 0:1
FT Ceramica Cleopatra - Pyramids 2:0
FT Zamalek - ZED 1:2

π—˜π—‘π—šπ—Ÿπ—”π—‘π——: Championship
FT Leicester - Leeds 0:1

π—₯π—ͺ𝗔𝗑𝗗𝗔: Premier League
FT Police - Gorilla 1:0

π—¦π—”π—¨π——π—œ 𝗔π—₯π—”π—•π—œπ—”: Saudi Professional League
FT Al Fateh - Al Hilal 0:2
FT Al Taee - Al Feiha 3:3
FT Al Shabab - Al Ittihad 1:0

π—§π—”π—‘π—­π—”π—‘π—œπ—”: Ligi Kuu Bara
FT Kinondoni MC - Dodoma Jiji 1:2
FT Mtibwa Sugar - JKT Tanzania 1:2
FT Kagera Sugar - Tanzania Prisons 2:1

𝗧𝗨π—₯π—žπ—˜π—¬: Super Lig
FT Galatasaray - Kasimpasa 2:1

04/11/2023

DAR ES SALAAM: KOCHA wa Yanga Miguel Gamondi amesema hana rekodi yoyote ya kuvunja dhidi ya Simba kwani hajawahi kupoteza dhidi ya timu hiyo.
-
Kocha huyo amesema katika mchezo mmoja aliocheza dhidi ya Simba alipata sare lakini wapinzani wake walifaidika kwa changamoto ya mikwaju ya penati kitu ambacho yeye anaaminini alimaliza kazi yake ndani ya dakika 90.
-
Ameongeza kuwa kinachokwenda kutafutwa uwanjani kesho ni heshima ya Klabu ya Yanga na sio ya kocha wa Yanga.

Una maoni usisite kutuandikia

04/11/2023

Hivi ndivyo tulivyolala jana. Wanasimba tiketi zinakatika hizo tufanye kuwahi kununua tiketi ili kesho uwanja ujae nyekundu na nyeupe.

04/11/2023

YANGA YATUPIWA LAWAMA MCHEZO WA SIMBA SC NA YANGA SC

Bodi ya ligi kuu Tanzania (TPLB) imesema haipendezwi na tabia ya timu mgeni kwenye Mchezo wa Kariakoo Derby kutoifanyia promo mechi hiyo na kuachia jukumu hilo kwa timu mwenyeji pekee.

Akizungumza na kituo cha Clouds fm radio msemaji wa bodi ya ligi, Karim Boimanda amesema mchezo huo si tu kwa ajili ya mapato ni Mchezo mkubwa Nchini na Afrika mashabiki hivyo vilabu vyote viwili (2) vinapaswa kuipromoti mechi hiyo.

"Hii inatokana na kanuni ya kuwa timu mwenyeji ndio atapata mapato yote ndio maana timu mgeni hafanyi promo, bodi ya ligi hatufurahishwi na jambo hilo tutalifanyia kazi suala hilo. Mechi hii sio tu kwa ajili ya mapato ni mechi ya hadhi ya Nchi"

πŸ—£οΈ Karim Boimanda

04/11/2023

β€œSijawahi kupoteza mchezo dhidi ya Simba, tulitoka suluhu hivyo sina rekodi yoyote ya kuvunja na kitu kikubwa kwangu ni timu kushinda,sio rekodi nimewaandaa wachezaji k**a mechi zingine, mpira ni mchezo wa makosa yule atakayefanya makosa basi ataukuta mpira kwenye wavu” - GamondI

04/11/2023

β€œWapinzani wangu wana wachezaji wazuri sana eneo la Kiungo, nami nataka niwazuie wasicheze kutoka eneo hilo, nitachagua wachezaji sahihi wa kazi hiyo, kesho watacheza wachezaji wangu bora eneo hilo” Coach Robertinho, Simba SC.

10/08/2023

SIMBA SC vs SINGIDA FG: Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kwamba Simba SC imewasilisha vibali vya wachezaji 11 wa kigeni huku Singida Fountain Gate ikiwasilisha vibali vya wachezaji 10.

Kinachosubiriwa sasa ni moto kuwasha ndani ya dimba la Mkwakwani Tanga.

Mechi itakuwa LIVE kuanzia saa 1:00 usiku

09/08/2023

Taarifa kwa umma kutoka Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania kwenda kwa Vilabu vya Yanga SC, Simba SC na Singida Fountain Gate FC.

Toa maoni yako

22/07/2023

MIQUISSONE ATAMBULISHWA SIMBA SC

kwao

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Ilala?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Category

Telephone

Address


Ilala