Mjukuu wa muhozya

Mjukuu wa muhozya

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Mjukuu wa muhozya, Sport & recreation, Mwanza jiji, Ilemera.

15/12/2023

TAMTHILIYA YA LIMENIKUTA
MTUNZI: REHEMA.D.MUHOZYA
ONYESHO LA KWANZA( SIKITIKO)
Asubuhi na mapema kelele za ndege zinasikika mithili ya watoto walioachwa na mama yao aliyeelekea katika shughuli za kutafuta riziki.Muuza duka anaonekana akifanya usafi nje ya duka lake huku akiwa anaimba
" Kazi yangu ya dukani ooooh!! yaniweka matatani ooooh!! wanaonirudisha nyuma wengi ni majirani ooooh!!"( Ghafla anaonekana mama mmoja aliyevaa nguo mithili ya mwendawazimu akijongea mpaka kwenye mlango wa dukani
Muuza duka: karibu mama shikamoo
Mama: Marhaba mwanangu za mwamko?
Muuza duka: salama tunamshukuru Mungu eeh! nikuhudumie nini mama.
Mama: samahani kijana wangu mimi sina hela ila nahitaji unga wa dona kilo moja,maharage nusu na kipande kimoja cha sabuni ya magadi.Kesho nitaleta hela Yako naishi pale kwa mzee zwazwa.
Muuza duka:. Hivi mama huoni aibu asubuhi yote hii kusimama kwenye maduka ya watu kukopa kweli? Hata k**a unahitaji kukopa ndio asubuhi,samahani kwa hilo sitaweza kufanya hivyo kwasababu ndio kwanza nimefungua na sijauza hata mia mbovu

Mama: kijana wangu nisaidie tu hela nitaleta kesho wala sitakusumbua.

Muuza duka: mama mbona nimeongea kiswahili tu nimesema hivi ndio kwanza nimefungua na bado sijauza

Mama: sawa nimekuelewa,ila nakuomba unisaidie kwa leo.

Muuza duka: mama nenda usije kuniharibia " mood" yangu asubuhi yote hii, Yani Kuna watu wameubwa kuwakera wenzao

Mama: kijana wangu haya ni maisha tu Kuna kupata na kukosa.

Muuza duka: wewe mama ni mchawi mbona uko k**a kupe k**a unaona ni rahisi fungua duka lako uwe unachukua unachokitaka

Mama: sawa kijana wangu nisamehe kwa kukukwaza asubuhi yote hii ila ni shida ndio zinasababisha. Mama aliondoka dukani hapo na kushika njia ya kwenda nyumbani kwake Ili atafute njia nyingine ya kujipatia riziki kwa siku hiyo.
ONYESHO hili litaendelea kesho 16/12/2023.

13/12/2023

Wale mnaoendelea kujumuika nami karibuni sana ninatambua mchango na nafasi yenu kwangu.

07/12/2023

Wadau wapenzi wa hadithi siku ya tarehe 12/12/2023. Hadithi yetu tuliyoisubiri kwa muda itakuwa inatoka naamini mtafurahi.

27/11/2023

Wapenda muda unakaribia kaeni mkao wa kula

24/11/2023

Mnao jiunga katika ukurasa wangu karibu Sana na mjisikie mpo sehemu salama na mtajifunza vitu vizuri.

23/11/2023

Wapendwa samahani kwa usumbufu naamini mnaendelea vizuri kwa msaada wa mungu rasmi 12/12/2023.tamthiliya yetu yetu ndio inakuwa mubashara kwenu wadau kwasababu Kuna sababu za kimaandalizi zimeingiliana naamini wapendwa wangu ni waelewa.

23/11/2023

Wadau wangu pendwa katika tasnia hii ya fasihi kwa maandishi naamini mnaendelea vizuri na Leo ndio ile siku ya kuachilia tamthiliya yangu kwa jina la UBINADAMU UTATA hivyo kaeni tayari.Asanteni

22/11/2023

Kuanzia tarehe 23/11/2023.Nitaachilia tamthiliya yangu inayotambulika kwa jina la UBINADAMU UTATA wadau wangu naamini mtapata kitu kizuri.

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Ilemera?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Website

Address


Mwanza Jiji
Ilemera