13/05/2026
(🏟 Airtel Stadium, Singida)
FT: Didoma Jiji 3️⃣-2️⃣ Yanga SC
⚽️⚽️ Okello 02,' 42'
⚽️ Mwamnyeto 29' (OG)
⚽️ Mwana kibuta 90'
⚽️ Waziri Jr 90+6
Journalist, Newswriter &Reporter, RedioPresenter &GraphicDesigner, DigitalContentCreator
13/05/2026
(🏟 Airtel Stadium, Singida)
FT: Didoma Jiji 3️⃣-2️⃣ Yanga SC
⚽️⚽️ Okello 02,' 42'
⚽️ Mwamnyeto 29' (OG)
⚽️ Mwana kibuta 90'
⚽️ Waziri Jr 90+6
Goli la pili la Okello dakika ya 42'. Kwa mujibu wa Sheria ni Offside au sio Offside???
13/05/2026
(Airtel Stadium, Singida)
HT: Didoma Jiji 1️⃣-2️⃣ Yanga SC
⚽️⚽️ Okello 02,' 42'
⚽️ Mwamnyeto (OG)
13/05/2026
Nguli wa zamani wa Washika Mitutu wa London Arsenal Peter Simpson, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 81.
Kwa mujibu wa taarifa ya Arsenal iliyotolewa leo inasema,
“Kila mmoja ndani ya Arsenal amesikitishwa kusikia kuwa Peter Simpson amefariki dunia akiwa na miaka 81.
Peter alikuwa sehemu kubwa ya kikosi kilichoshinda mataji mawili msimu wa 1970-71, akiwa ameichezea klabu mechi 478 wakati wake akiwa hapa.
Sote tunawafikiria wapendwa wake katika kipindi hiki kigumu.
Pumzika kwa amani, Peter.” Taarifa ya Arsenal ilisema.
Simpson alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Arsenal 1970-1971 kilichoshinda mataji mawili na alicheza karibu mechi 500 kwa klabu hiyo.
Nyota huyo alicheza k**a beki akicheza mechi 478 jambo lililomfanya kuwa mchezaji wa 10 mwenye kucheza mechi nyingi zaidi katika historia ya klabu hiyo.
13/05/2026
Kichwa cha marehemu James Temba, ambaye Mwili wake umezikwa siku chache zilizopita Moashi Mkoani Kilimanjaro baada ya kuuawa kikatili, kimepatikana katika eneo la Kitunda Kibeberu, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo imethibitishwa na baba mzazi wa marehemu, Mzee Temba, ambaye amesema walipokea taarifa za awali kutoka Jeshi la Polisi kuhusu kupatikana kwa kichwa hicho ambacho kilitenganishwa na kiwiliwili cha mwanae.
Aidha Mzee Temba amesema baada ya kukamilika kwa taratibu za kiupelelezi zinazofanywa na Jeshi la Polisi, familia itafanya maandalizi ya kuhifadhi kichwa hicho karibu na sehemu ulipozikwa mwili wa marehemu.
“Wakati wa mazishi ya awali ya kiwiliwili cha James Temba, familia iliacha nafasi maalum ya dharura iwapo kichwa kingepatikana ili kiweze kuzikwa kwa heshima stahiki pamoja na mwili wake,” amesema.
Aidha, Mzee Temba amelishukuru Jeshi la Polisi kwa juhudi za ufuatiliaji zilizosaidia kupatikana kwa kichwa hicho, akiwashukuru pia ndugu, jamaa, marafiki, Watanzania pamoja na waandishi wa habari kwa kuendelea kuwa pamoja na familia yake katika kipindi chote kigumu kwa familia yake.
13/05/2026
Rais wa Marekani, Donald Trump, rasmi amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital jioni ya Mei 13, 2026 tayari kwa ziara yake nchini humo.
Trump amepokelewa na Makamu wa Rais wa China, Han Zheng, kabla ya kuondoka kwa kutumia gari lake rasmi la rais linalojulikana k**a “The Beast.”
Ziara hiyo ya kiserikali ni ya kwanza kufanywa kwa rais wa Marekani nchini China ndani ya takriban miaka tisa, na inafuatiliwa kwa karibu duniani kote kutokana na hali ya sintofahamu na mvutano unaoikabili uchumi wa dunia.
13/05/2026
(🏟 Sokoine Stadium, Mbeya)
FT: Mbeya City 0️⃣-2️⃣ Coastal Union
⚽️ Maabad Maulid 35' (P)
⚽️ Saad Mwanza 74'
13/05/2026
Aliyekuwa kocha wa klabu ya Pedro Goncalves, ametwaa tuzo ya Kocha Bora kwa mwezi Aprili Ligi kuu Tanzania Bara (NBCPL).
Kufuatia tuzo zilozotolewa na k**ati ya tuzo za shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Goncalves amewapiku Steve Barker wa , na Etiene Ndairagije wa ambao walikuwa kwenye kinyang'anyiro hicho.
Kocha huyo ambaye amefutwa kazi siku chache zilizopita ameiongoza Yanga SC katika ushindi wa michezo mitatu akiendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, na kufunga mabao 12.
13/05/2026
Kiungo Allan Okello wa Yanga SC, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Aprili wa Ligi Kuu ya kwa msimu wa mwaka 2025/26.
Okello ameshinda tuzo hiyo mbele ya nyota Pacome Zouzoua wa na Idd Selemani wa , ambao waliingia fainali kuwania tuzo hizo kufuatia mchakato uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Rais wa Marekani, Donald Trump, wakati akiomdoka rasmi Ikulu ya White House mjini Washington DC kuelekea Beijing, nchini China kwa ajili ya kukutana na Rais wa China, Xi Jinping.
Trump ameonekana akipanda helikopta kutoka Ikulu kwenda uwanjani kabla ya kuanza safari yake kwa kutumia ndege maalum ya rais, Air Force One, kuelekea China.
13/05/2026
Ligi kuu Tanzania Bara kuendelea leo katika viwanja viwili tofauti ambapo Yanga SC, Coastal Union, Dodoma Jiji FC, na Mbeya City watakuwa dimbani leo Kuzisaka alama tatu.
Mbeya City atakuwa nyumbani akimkaribisha Coastal Union katika dimba la Sokoine jijini Mbeya ambapo mchezo utakaopigwa majira ya saa 08:00 mchana.
Kwa upande mwingine Yanga SC itakuwa Dimbani itakuwa Ugenini ikikipiga dhidi ya Dodoma jiji katika dimba la Airtel Stadium, Singida, Mchezo utakaopigwa majira ya saa 10:15 jioni.
⏰ 14:00. Mbeya City 🆚️ Coastal Union (🏟Sokoine Stadium)
⏰ 16:15. Dodoma Jiji 🆚️ Yanga SC (🏟 Airtel Stadium)
Dodomajiji