02/11/2021
JICHO MAKINI KWENYE 90 ZA YAรGA SC NA RUVU SHOOTING.
Leo ilikuwa ni Mayele Vs Mohammed Makaka. Mashuti manne(4) ya Mayele yaliyo lenga lango yaliokolewa na Makaka Kwa ustadi mkubwa. Makaka ni miongoni mwa Magoli Kipa wazuri na wenye ubora sana kwenye hesabu.
Timu ilimmiss Khalid Aucho.Muunganiko na ushirikiano wa Yannick Bangala na Mukoko haukuwa kwenye Kiwango bora k**a ule wa Aucho na Mukoko. Aucho mara hucheza karibu sana kwenye pivot, Mukoko alicha nafasi kubwa kati yake na Bangala.
Djuma Shabani hakuwa na ufanisi Mkubwa leo hasa kabla ya kadi nyekundu ya Santos, Alipoteza pasi kadhaa. Niliamini baada ya Yanga kuongoza basi mabadiliko ya kumuingiza David Bryson yangekuwa kwa Djuma ili Kibwana aende kulia. Djuma anaonekana alitumia nishati kubwa kwenye Derby dhidi ya Azam FC.
Mkwasa alikuwa na mipango bora sana hasa kwenye alipo amua Kucheza kwenye falsafa ile ile ya umiliki wa mpira. Walifanikiwa kwa asilimia kadhaa walifanya play out from the back,walifanikiwa na build-up yao ilifia Katikati ya Uwanja. walikosa njia bora ama link-up Man kwenye kiungo na ushambuliaji.
Kadi nyekundu ya Santos Mazengo Ilibadili muelekeo kiuchezaji na mipango kiujumla (game approach) Kwa Ruvu Shooting. Baada ya kucheza kwenye total football na kurudi kufanya Low block huku wakitumia Counter Attack. Iliwarejesha Sana Yanga kwenye wepesi wa kuumiliki mchezo.
Emmanuel Mwandembwa ni miongoni mwa Waamuzi bora Nchi. Kadi nyekundu ilikuwa sahihi Kwa asilimia ๐ฏ na, pigo la huru la penati lina maswali mengi sana hasa kwenye kuligundua k**a sio ama ndiyo. Ila Kwa namna ilivyo tokea basi Mwamuzi yeyote anaweza kutoa ama kutokutoa pia. Tukio tata.
30/10/2021
Yanga SC dhidi ya Azam FC Leo pale Kwa Mkapa. Ni Ligi Kuu NBC Tanzania Bara. Inaaminisha kwamba Yanga SC wanaingia k**a dominant than Azam FC kwenye huu mchezo. Ubora wa vikosi Vyote viwili utoa picha hiyo.
Azam na Yanga Kwa pamoja zinaoneka Kuwa na wachezaji individual wana uwezo, hawapishani Sana. Kuanzia kwenye ulinzi, Kiungo hadi Idara ya ushambuliaji. Japo Katika hili Yanga inaonekana Kuwa bora sana kwenye Kiungo.
Ubora wa Kiungo cha Yanga sio dhidi ya Azam FC tu, bali Kwa michezo hii kadhaa inaonesha wao ndo wenye Kiungo bora zaidi ya timu yeyeto kwenye NBC PL. Hii imewapa nguvu Nabi na Kaze Kuwa na timu yenye uwezo wa kucheza " Out from the back"
Aina ya uchezaji inayohitaji uwe na viungo bora kufanya ujenzi wa mashambulizi kutoka kwenye lao kwenda mbele Yani Kuwa viunganishi bora wa ulinzi na ushambuliaji kwa vertical direction possession. Nguvu nyingine ya Yanga ni Kwenye winga zao, Yacouba na Jesus Moloko.
Kwenye aina ya ujenzi wa mashambulizi ya Yanga wa Out play from the back, Job na Mwamunyeto na Aucho wamekuwa wazuri kwenye kutengeneza mashambulizi hollizontal kupitia Kwa Kibwana au Djuma na kuwawapa nguvu Sogne na Moloko.
Hivyo hivyo pia walifanya spread out vertical kupitia Kwa Bangala na Fei Toto akidaidiwa deep na Mayele wamekuwa wakifanya pressing kutoka Katikati au pembeni pia. Kinachowasaidi ni Kasi yao hasa dakika 45 za mwanzo.
Azam ili kuwazuia Yanga hasa Kipindi cha Kwanza ambacho wamekuwa bora sana, ni ku track back, kupitia Kwa iwe Zulu ama Nado, hasa upande wa Djuma amabaye anapanda Sana. Wakifanikiwa kuwazuia Yanga Kuanzia juua na kuwaondolea comfortability walinzi wao kuanza nyuma watafanikiwa kuwazuia.
Mkakati bora wa Kutengeneza mashambulizi baada kuzuia ni counter pressing kwenye Kasi ya Nado, anaoneka Yupo kweny top level ya Karia yake Kwa sasa. Anatengeza nafasi pia anafunga, uchezaji wake unawatengenezea space of playing wenzake kwenye mtirririko wa ushambuliaji.
Mchezo unamagoli siuoni kuisha Sare. Ni Chicken Man Vs Professor Nabi.
Robert Richard
27/10/2021
JICHO MAKINI KWENYE DAKIKA 90 ZA SIMBA SC NA POLISI TANZANIA.
Shukran Kwa Kocha Malale Hamsini wa Polisi Tanzania na Kocha Hetimana Thierry wa Simba SC, Kwa mchezo wenye hadhi ya Ligi Kuu, kiushindani,Kiufundi na Kimbinu. Ahsante Kwa wachezaji wote Kwa josho la ushindani kwenye dakika zote.
Hizi ni alama 3 muhimu zaidi Kwa Simba SC, kuliko pira biriani Yani soka la kuvutia Kwa wanamsimbazi. Siku zote timu inapojengwa hasa na Kuwa na mwalimu mpya basi ujenzi wenye kupata matokeo ndani yake huwa na mtirririko mzuri Kwa Mwalimu kufikia dhamira yake mapema.
Hetimana Leo alibadilika kwenye approach Mama ya Simba hasa kwenye kushambulia. Nguvu ya Simba kiushambuliaji huwa kutokea katikati. Hufanya high block kupitia namba 10, winga mara nyingi hufanya mikimbio ya kuingia ndani. Leo timu imefanya pressing kupitia pembeni hasa Kwa Dilunga.
Alipiga Krosi Kadha ambazo hazikutumika vema kutokana na uwepo wa idadi ndogo ya wachezaji wa Simba kwenye eneo la Polisi tofauti na Polisi mara zote walikuwa ni 4 Vs 1 yani walinzi wanne dhidi ya Kagere pekee. K**a Thierry anahamia kwenye pressing kupitia Wings atapaswa kutumia "double strike" watumie mipira ya Kros.
Larry Bwalya apunguziwe majukumu kichwani yanampoteze ufanisi. Aina ya wachezaji anaocheza nao kwenye kiungo wa hawachezi nae karibu kumpa box to box playing. K**a sio Kocha kumwambia,basi anaamini baada ya kuondoka Pacha wake Luis na Chama yeye ndiye Creator in Chief Kwa sasa.
Malale amefanya yote katika ubora mkubwa Ila ilifika wakati alihitaji kulazimisha wachezaji wake wa eneno la ushambuliaji wafanye pressing baada kufanikiwa kwenye Low block. Walikuwa compact kwenye kiungo na Ulinzi nyuma.
Unapofanikiwa kumzuia mpinzani kwa ufanisi ni unapaswa kutafuta magoli kwake. Polisi walikuwa na utulivu Mkubwa walipokuwa na mpira na bila mpira walizuia k**a timu. Tariq Seif, Adam Adam, Vitalis Mayanga na Daruweshi Saliboko walicheza taratibu sana jambo lilopelekea Simba kujipanga Kwa haraka kuzuia maeneo.
Endapo wangekuwa na Kasi na mgandamizo kuelekea kwenye box la Simba ingelazimisha makosa ya ulinzi Kwa Simba yaonekane.
Well done Mkongwe Yondan Kelvin. Polisi wana timu nzuri sana
27/10/2021
Timu 12 Kati ya 16 zilizo fuzu hatua ya makundi CAF champions League 2021/2022 zinafundishwa na Makocha Kutoka ndani ya Afrika.
Walid Regragui ๐ฒ๐ฆ-Wydad AC
Lassaad Chabbi ๐น๐ณ-Raja Casablanca
Pitso Mosimane ๐ฟ๐ฆ Al Ahly
Radhi Jaidi ๐น๐ณ-Espรฉrance de Tunis
Benni McCarthy ๐ฟ๐ฆ - AmaZulu FC
Morena Ramareboli ๐ฟ๐ฆ- Galaxy FC
Nabil Kouki ๐น๐ณ-ES Sรฉtif
Lassaad Dridi ๐น๐ณ- Etoile du Sahel
Lamine N'Diaye ๐ธ๐ณ- Horoya AC
Roque Sapiri ๐ฆ๐ด- Sagrada Esparanca
Mateus Bodunha ๐ฆ๐ด - Petro Atlรฉtico
Rhulani Mokwena ๐ฟ๐ฆ - Mamelodi Sundown
NB. Mataifa ya Tunisia na Afrika Kusini Kwa pamoja wamekuwa na idadi ya makocha 4 kila Taifa. Jumla wamechangia makocha 8 kati ya 12 watokao Afrika. Angola inafutia Kuwa na Makocha 2 huku Morocco na Guinea yakiwa na Kocha mmoja mmoja.
26/10/2021
Kwa Mujibu wa ratiba hii ya michezo ya mtoanao hatua ya pili Shirikisho Barani Afrika, iliyotoka leo Oktoba 26/2021
Simba SC ๐น๐ฟ itakutana na Red Arrows ya Zambia๐ฟ๐ฒ mbali na Simba pia ratiba inaonesha Klabu nyingine Kutoka Tanzania Bara Biashara Utd,hatima yake bado ipo mikononi mwao. Mshindi kati yake na Al Ahli Tripoli๐ฑ๐พ atakutana na Stade Malien ya Mali๐ฒ๐ฑ
ngoma bado mbichi....
26/10/2021
IT IS OVER NA KAZI IENDELEE
Klabu ya Simba imetangaza kuachana na aliyekuwa Kocha wake Mkuu Mfaransa Didier Gomezi Da Rosa.
Kocha huyo alijiunga na Simba SC mwezi January 2021 ameitumukia Klabu hiyo Kwa miezi 10, amefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, FA CUP na kuifikisha timu hiyo robo fainali ya CAF Klabu Bingwa.
Mbali na Gomezi wengine walivunjiwa kandarasi ni Kocha wa viungo Adel Zrane ๐น๐ณ na Kocha wa Makipa Mbrazil Milton Nienov ๐ง๐ท. Kwa sasa timu itabaki mikononi mwa Thierry Hetimana ๐ท๐ผ na msaaidizi wake atakuwa Selaman Matola ๐น๐ฟ
Hatua hii imekuja siku chache baada ya Simba SC kutupwa nje ya Mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika Kwa msimu wa 2021/2022, na Jwaneng Galaxy ya Botswana ๐ง๐ผ
NB. Makocha wote Duniani huajiriwa Kwa makubaliano ama malengo mahususi. (Target) Kwa Simba SC misimu ya hivi karibuni wamekuwa na target ya kufika makundi hadi nusu fainali ya CAF champions league.
Makocha Kadhaa wamewafukuza Kwa kutokufikia lengo hilo Mama. K**a sio Kocha kufikia malengo miongoni mwa sababu nyingine ambayo hupelekea Klabu kumfukuza Kocha ni mwenendo mbovu, kiuchezaji, matokeo na mambo ya nje ya uwanja hasa nidhamu ya timu.
Je! Da Rosa alistahili kufukuzwa Kwa mujibu wa sababu tajwa hapo juu??
25/10/2021
TIMU 16 ZILIZOFUZU HATUA YA MAKUNDI TOTALCAFCL 2021/22
โข Al Ahly ๐ช๐ฌ
โข Zamalek ๐ช๐ฌ
โข Etoile Sahel ๐น๐ณ
โข Sagrada ๐ฆ๐ด
โข Al Merreikh ๐ธ๐ฉ
โข AmaZulu ๐ฟ๐ฆ
โข Petro Atletico ๐ฆ๐ด
โข Raja CA ๐ฒ๐ฆ
โข Mamelodi Sundowns ๐ฟ๐ฆ
โข Jwaneng Galaxy ๐ง๐ผ
โข Wydad AC ๐ฒ๐ฆ
โข ES Tunis ๐น๐ณ
โข Horoya AC ๐ฌ๐ณ
โข Al Hilal Omdurman ๐ธ๐ฉ
โข ES Setif ๐ฉ๐ฟ
โข CR Belouizdad ๐ฉ๐ฟ
NOTE. Timu za Al Ahly Misri, Raja Casablanca, Wydad Casablanca na Esparance ST zenyewe zitaongoza Makundi baada ya Kuwa kwenye Pot 1. Michuano hii itawakilishwa na Kanda 4 pekee Kati ya 5 za CAF na 6 zilinazotambulika kimashindano ya CAF.
Ukanda wa Kusini COSAFA umeingiza timu 5 kwenye hatua hii kupitia timu mbili kutoka Afrika Kusini ambazo ni (AmaZulu na Mamelodi Sundown),timu mbil Kutoka Angola(Sagrada na Petro Atletico) moja Botswana (Jwaneng Galaxy)
Ukanda wa Mashariki na Kati CECAFA imeingiza timu mbili (2) zote zikitoka Taifa moja Yani Sudan ambazo ni El Merreikh na Al Hilal Omdurman.
Ukanda wa Magharibi yani WAFU ONE wao wameingiza timu moja pekee Horoya AC Kutoka Guinea .
Ukanda wa Kaskazin Yani UNAF, K**a ilivyo Kwa misimu mingine umekuwa kinara kwa kuingiza timu nyingi hatua ya makundi CAF champions League. Jumla ya timu 8. Wydad na Raja Casablanca kutoka Morocco.
Zingine ni Al Ahly na Zamaleck kutoka Misri, SR Belouizdad na ES Setif kutoka Algeria na Esparance ST,Etoile du Sahel kutoka Tunisia.
23/10/2021
CAF champions League 2021/2022. Timu ambazo zimefuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo hadi sasa.
Al Ahly ๐ช๐ฌ โข
Zamalek ๐ช๐ฌ
Etoile Sahel ๐น๐ณ
Sagrada ๐ฆ๐ด
Al Merreikh ๐ธ๐ฉ
AmaZulu ๐ฟ๐ฆ
Petro Atletico ๐ฆ๐ด
Raja Club Athletic ๐ฒ๐ฆ
Bado timu nane (8) zingine ili kulamilisha idadi ya timu 16
23/10/2021
Pichani ni Waamuzi wa uliopaswa Kuchezesha Mchezo wa Al Ahli Tripoli na Biashara Utd.
Uwepo wa Waamuzi Uwanjani tafsiri yake ni kwamba mchezo ulipaswa kuwepo. Kwa mantiki hiyo Waamuzi wameipatia matokeo ya ushindi Al Ahli Tripoli kikanuni, hii ni baada ya Biashara Utd kushindwa kufika Uwanjani.
Ikumbukwe Biashara imeshindwa kusafiri kuelekea Libya ikitajwa sababu za kiusafiri.
Mchezo wa awali iliopigwa Tanzania Biashara Utd ilishinda magoli 2 Kwa 0.
21/10/2021
TUZO ZA TFF VPL MSIMU WA 2020/2021
Golikipa bora Aishi Manula (Simba SC)
Beki bora Mohammed Hussein (Simba)
Kiungo Clatous Chama (Simba SC)
Mfungaji bora John Bocco (Simba SC)
Mchezaji Chipukizi Abdul Sopu (Coastal)
Mchezaji Muungwana Kibwana Shomari (Yanga SC)
Kocha bora- Didier Gomezi )Simba SC)
Mwamuzi bora Ramadan Kayoko(Dar Es salaam
21/10/2021
Timu ya Taifa Tanzania "Taifa Stars" imepanda nafasi mbili (2) kwenye viwango vya FIFA Kwa mwezi wa Kumi (October). Tanzania imepanda hadi nafasi ya 130 kutoka 132 na Ikumbukwe miezi mitatu iliyopita Tanzania ilikuwa nafasi ya 137.
Kwa upande wa Afrika Tanzania imepanda hadi nafasi ya 36 Kati ya Mataifa Wanachama 50.
Ukanda wa Mashariki na Kati Yani CECAFA Orodha ni k**a ifuatavyo.
1 Unganda ๐บ๐ฌ FIFA 82
2 Kenya ๐ฐ๐ช FIFA 104
3 Sudani ๐ธ๐ฉ FIFA 124
4 Tanzania ๐น๐ฟ FIFA 130
5 Rwanda ๐ท๐ผ FIFA 133
6 Ethiopia ๐ช๐น FIFA 137
7 Burundi ๐ง๐ฎ FIFA 141
8 S.Sudan ๐ธ๐ธ FIFA 167
9 Djibouti ๐ฉ๐ฏ FIFA 188
10 Somalia ๐ธ๐ด FIFA 195
11 Eritrea ๐ช๐ท FIFA 203
20/10/2021
JICHO MAKINI NDANI YA DAKIKA 90 ZA TWIGA STAR ๐ NA NAMIBIA
Vijana wa Mjini wanasema Ulaya haidanganyi. Yani Ulaya ni Ulaya tu! Pichani ni nyota wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Namibia Zenatha Coleman na mfungaji wa magoli 2 Kwa timu hiyo.
Zenatha anacheza Klabu ya Sevilla ya Wanawake inayoshiriki Primera Division kule Nchini Hispania. Akiwa na Sevilla atyari ameshafunga magoli 8 Kwenye michezo 38. Amepita Zaragoza CFF, Valencia ya Wanawake zote za Hispania.
Hakuwa na hatari kwa macho ya kawaida Ila kiufundi alikuwa hatari sana. Kocha anajua ubora wake ndiyo maana alimuweka mbele pekee ili kupokea counter attack zote.
Alifanya hivyo Kwa ufasini na ameonesha ukomavu Mkubwa, mipira yote iliyofika kwake iliwapa shida Twiga Start. Nafasi chache alizopata ndizo alizotumia pia
Namibia hawakuwa na presha walipopoteza Mpira, wana miili mikubwa na walizuia Mikimbio yote ya Aisha Masaka, Opa Clement na Mwanahamis Omary. Bench la Ufundi la Namibia inaoneka kuwasoma zaidi Twiga Start.
Twiga Stars hawakuweza Kwenye Ubora ule uliozoweleka. Muda mwingi wakionekana Kucheza individual. Pia hali ya uchovu umeonekana kuwasumbua zaidi. Licha ya Ubora wao wa kuzuia bado Twiga Start hawa kufanya High press with higj intensity.
AFCON QW2022 MOROCCO
Twiga Stars 1-2 Namibia