SMJ sports arena

SMJ sports arena

Share

Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from SMJ sports arena, Stadium, arena & sports venue, Mwanza.

12/01/2021

BBC News, SwahiliRuka hadi maelezo

Yaliyomo

Habari

Michezo

Video

Vipindi vya Redio



Tetesi za soka Ulaya Jumanne 12.01.2021: Caicedo, Militao, Winks, Gonzalez, Dembele, Buendia, Kenny

12 Januari 2021, 07:02 EAT

Imeboreshwa Saa 5 zilizopita



CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Tottenham huenda ikamsajili beki mwenye umri wa miaka 22 raia wa Brazil Eder Militao

Tottenham huenda ikamsajili beki mwenye umri wa miaka 22 raia wa Brazil Eder Militao - anayesakwa na Roma, AC Milan na Inter - kwa mkopo kutoka Real Madrid ikiwa na mbadala wa kumnunua kwa mkataba wa kudumu. (Corriere dello Sport - in Italian)

Klabu ya Jose Mourinho Tottenham Hotspurs imejiunga na Leeds na Juventus katika kumsaka winga wa klabu ya Stuttgart Nicolas Gonzalez, 22, huku mchezaji huyo wa Argentina akilengwa katika dirisha la uhamisho la majira ya joto. (The Athletic - subscription required)

Huenda pia kuna uhamisho mwengine kutoka Tottenham huku Valencia ikiwa na hamu ya kumsajili kiungo wa kati wa Spurs na England mwenye umri wa miaka 24 Harry Winks kwa mkopo . (Football London)



CHANZO CHA PICHA,GETTY IMAGES

Maelezo ya picha,

Winga wa klabu ya Stuttgart Nicolas Gonzalez

Brighton wana imani wameishinda Newcastle United katika kumsaini kiungo wa kati wa Ecuado Moises Caicedo kutoka klabu ya Indipendiente del Valle. Kinda huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa akilengwa na klabu ya Man United(Talksport)

Kiungo wa kati wa Ufaransa na mshindi wa kombe la Dunia Steven N'Zonzi huenda mkataba wake wa mkopo katika klabu ya Rennes ukakatizwa baada ya kuhusishwa na uhamisho wa Arsenal na Everton . (Foot Mercato - in French)

Mshambuliaji wa Ufaransa na Lyon Moussa Dembele, 24, anakaribia uhamisho wa kuelekea Atletico Madrid baada ya kukataa uhamisho wa West Ham. (Telefoot via Sky Sports)



CHANZO CHA PICHA,SNS GROUP

Arsenal hailengi tena kumsajili kiungo wa kati wa Norwich Emi Buendia baada ya klabu hiyo kuweka dau la £40m kumuuza mchezaji huyo wa Argentine. (Express)

Want your business to be the top-listed Gym/sports Facility in Mwanza?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Website

Address


Mwanza